Nilienda kurudisha akaunti yangu ilikuwa dormant zaidi ya mwaka, wakaniambia nitoe Hela 10,000 na namba, nikawapatia wakasema nirudi baada ya masaa mawili akaunti itakuwa tayari.
Narudi nakuta bado wakasema ni mtandao ila akaunti imeisharudishwa, nikaenda nyumbani kesho yake naenda kuweka pesa kwa wakala anasema akaunti bado haifunguki.
Narudi tawini naambiwa akaunti yangu ni dormant sana haiwezi kufunguka Tena nifungue nyingine nawaambia wafungue wanasema NIDA imekataa ni akaunti Moja TU kwa Kila NIDA.
Nawauliza kwahiyo siruhusiwi kufungua akaunti Tena? ..wakajibu NDIYO!
Basi naombeni msimbazi wangu, wakasema wao hawajui ilipo kama Nina ushahidi wa niliyemwachia nitoe, siku hiyo hakuwepo yule mdada mwenye Rasta, mnene mweusi niliyemkuta Jana ila alikuwepo jamaa mwingine TU mrefu mweupe.
Sasa ushahidi gani jamani na wakati ata simu hawaruhusu.
Kifupi "Nilidhurumiwa na CRDB tawi la MASASI" shilingi elfu kumi.