Kero kwa Bank ya CRDB

Kero kwa Bank ya CRDB

Super mega

JF-Expert Member
Joined
Nov 21, 2023
Posts
1,177
Reaction score
2,361
Wakuu hivi naomba kuuliza hivi CRDB BANK wanakata malipo ya huduma ya kutunza fedha kila siku na kwa kila muamala unaoingia mana dah sio kwa haya makato yanayoendelea yani hela ikiingia tu wanakata 4000,au 5000,kisha unapotoa wanakata sio chini ya 10000 hapo ni kwa amount kwanzia Mil.1 chini ya Mil wanakata 10000.hii imekaaje wakuu tena tukipata majibu kutoka kwao itakua vyema zaidi.asante


Wakuu kwa sasa hata ukitaka upitishie pesa yako kwa account ya wakala nao wanakataa wanasema wanaogopa kukogombana na wateja benki ina makato ambayo hayaelleweki hata kumwambia mteja unashindwa uanzie wapi dah hii ni balaa.
 
Wakuu hivi naomba kuuliza hivi CRDB BANK wanakata malipo ya huduma ya kutunza fedha kila siku na kwa kila muamala unaoingia mana dah sio kwa haya makato yanayoendelea yani hela ikiingia tu wanakata 4000,au 5000,kisha unapotoa wanakata sio chini ya 10000 hapo ni kwa amount kwanzia Mil.1 chini ya Mil wanakata 10000.hii imekaaje wakuu tena tukipata majibu kutoka kwao itakua vyema zaidi.asante

A Amount gani iliyoingia na amount ipi? Bila kusema hayo andiko lako halina uhalali
 
CRDB, Wana makato makubwa sana..
Nafikiria miamala ya mara kwa mara nifanyie Bank nyingine
Tatizo sijui haya malalamiko hawayasikii ?
 
Wakuu hivi naomba kuuliza hivi CRDB BANK wanakata malipo ya huduma ya kutunza fedha kila siku na kwa kila muamala unaoingia mana dah sio kwa haya makato yanayoendelea yani hela ikiingia tu wanakata 4000,au 5000,kisha unapotoa wanakata sio chini ya 10000 hapo ni kwa amount kwanzia Mil.1 chini ya Mil wanakata 10000.hii imekaaje wakuu tena tukipata majibu kutoka kwao itakua vyema zaidi.asante
Mkuu ulifungua akaunti ya aina gani?
Sema ndio hivyo wabongo tumekariri benki ni NBC,CRDB na NMB tu.
Kuna benki kama Stanbic ni nzuri sana ni waaminifu na hata ukienda benki yao kwenda kuchukua pesa hukuti foleni unahudumiwa kama VIP ila watu wengi hawaifahamu
 
Mkuu ulifungua akaunti ya aina gani?
Sema ndio hivyo wabongo tumekariri benki ni NBC,CRDB na NMB tu.
Kuna benki kama Stanbic ni nzuri sana ni waaminifu na hata ukienda benki yao kwenda kuchukua pesa hukuti foleni unahudumiwa kama VIP ila watu wengi hawaifahamu
Tatizo kwa sie wa vichochoroni hizo bank zingne hazina mawakala,pia hata matawi madogo hakunaaa
 
Nilienda kurudisha akaunti yangu ilikuwa dormant zaidi ya mwaka, wakaniambia nitoe Hela 10,000 na namba, nikawapatia wakasema nirudi baada ya masaa mawili akaunti itakuwa tayari.

Narudi nakuta bado wakasema ni mtandao ila akaunti imeisharudishwa, nikaenda nyumbani kesho yake naenda kuweka pesa kwa wakala anasema akaunti bado haifunguki.

Narudi tawini naambiwa akaunti yangu ni dormant sana haiwezi kufunguka Tena nifungue nyingine nawaambia wafungue wanasema NIDA imekataa ni akaunti Moja TU kwa Kila NIDA.

Nawauliza kwahiyo siruhusiwi kufungua akaunti Tena? ..wakajibu NDIYO!

Basi naombeni msimbazi wangu, wakasema wao hawajui ilipo kama Nina ushahidi wa niliyemwachia nitoe, siku hiyo hakuwepo yule mdada mwenye Rasta, mnene mweusi niliyemkuta Jana ila alikuwepo jamaa mwingine TU mrefu mweupe.

Sasa ushahidi gani jamani na wakati ata simu hawaruhusu.

Kifupi "Nilidhurumiwa na CRDB tawi la MASASI" shilingi elfu kumi.
 
Wakuu hivi naomba kuuliza hivi CRDB BANK wanakata malipo ya huduma ya kutunza fedha kila siku na kwa kila muamala unaoingia mana dah sio kwa haya makato yanayoendelea yani hela ikiingia tu wanakata 4000,au 5000,kisha unapotoa wanakata sio chini ya 10000 hapo ni kwa amount kwanzia Mil.1 chini ya Mil wanakata 10000.hii imekaaje wakuu tena tukipata majibu kutoka kwao itakua vyema zaidi.asante
Bora hao wapo wengine wanaitwa Postal Bank unaweza kukaa mwaka mzima wanakuambia machine ya kuprint ATM card haifanyi kazi
 
Kimbia mkuu,..hiyo bank ni waizi sana

Kila mtu anailalamikia hiyo bank-kuna thread kibao hapa JF za malalamiko kuwahusu.
Mkuu hii ni hatari na hawafanyii kazi hili na wana page yao rasmi hapa jukwaani dah shida sana.
 
Tatizo kwa sie wa vichochoroni hizo bank zingne hazina mawakala,pia hata matawi madogo hakunaaa
Sijajua unakaa maeneo ya wapi ila kwa Dar ina matawi kadhaa na Atm kila mahali kwa ambayo nayafahamu ni Posta,Kariakoo na Kinondoni
 
Mimi nimelimwa 40k jana ,zaidi ni kwamba nilitoa pesa kadhaa na wakakata hapo ila jana tu imetoa shwaa ..Nikavuta bank statement mtandao unasumbua.
Na jana na leo network karibia za benki ya NMB NA CRDB network iko chini sana na ndo wanakata hela hawa CRDB toka jana na nadhani wanakat hela kila siku hawa hii bank hapana sio nzuri.
 
CRDB, Wana makato makubwa sana..
Nafikiria miamala ya mara kwa mara nifanyie Bank nyingine
Tatizo sijui haya malalamiko hawayasikii ?
Ni kama hawasikii mkuu nimeona kuna wadau wengi tumelalamikia hili swala lakini Kadri siku zinakwenda makato ndo yanaongezeka
 
Back
Top Bottom