Kenya Kujenga mji wa teknolojia

Kenya Kujenga mji wa teknolojia

Msema yote

JF-Expert Member
Joined
Mar 19, 2013
Posts
448
Reaction score
301
Habari wadau!..
Vugu vugu la ukuaji wa teknolojia kwa nchi afrika wenzetu kenya wameamua kufanya kwa vitendo, Wakenya wote kwa pamoja wameweka tofauti zao za kiasiasa pembeni na kushiriana na serikali yao kuhakikisha maadhimio yao ya kuwa na mji wa kisasa wa teknolojia unakamilika ndani ya wakati.

Mji huu ambao umepewa jina la Sillicon Savannah utakuwa mji wa teknolojia, kama ulivo mji wa Sillicon Valley wa Marekani ambapo makampuni yote makubwa ya teknolojia yanapatikana hapo, kuanzia Google, facebook, ebay, Amazon, Octopus, Twitter, Instagram, whatsAap, Yahoo, eblogger, hp, YouTube, Android, Cisco, Intel na mengine mengi.

Mji wa wa Sillicon Savannah pia unategemewa kuwa na makumpuni kama hayo pia kutakuwa na sehemu na vituo vikubwa vya kuhifadhi nyaraka (Data Center), sehemu za kujifunzia na kukutana na wataalam mbali mbali (Hub), sehemu za kurudisha nyaraka mbali mbali zilizopotea (Data Recovery Store), Makampuni ya kutengeza program (Software Companies) ,Vyuo vikuu vya teknolojia, Shule za kimataifa (Internation Schools) Hospitali kubwa na za kisasa, Mahoteli Makubwa Viwanda vya kugundua na kuunda bidhaa mbali mbali za teknolojia kama octopus na intel za sillicon valley marekani.

Sillicon Savannah unategemewa na serikali ya kenya kufungua fursa za kiabiashara na ajira kwa wakenya, kwani mradi huu unategemwa kutoa ajira 200,000 (Laki mbili) ukikamilika, Mradi huu ni tumaini kwa wakenya wengi sana hasa watu wa fani za sayansi.

Mradi huu unajengwa kilomita 60 toka mji wa Nairobi unategemewa kuwa kituo kikubwa cha teknolojia afrika, serikali ya kenya inategemea kukamilika kwa mradi huu mwaka 2030 na shughuli zote kuwa tayari, ikiwa ni pamoja na uwepo wa taasisi kubwa za utafiti wa sayansi

PICHA MJI WA SILLICON SAVANAH UTAVOKUWA

1.jpg
2.jpg
4.jpg
2.jpg
1.jpg


VIDEO MJI WA SILLICON SAVANNA UTAVOKUWA





Maoni: Ni wakati sasa kwa wataalam wataalam wa fani mbali mbali za sayansi tanzania kushirikiana, kuungana na kusihirikisha serikali ili tuwe na mipango madhubuti, tuwe na makampuni yanayotambulika kimataifa, tufanye vitu serius, serikali ishirikishe wadau mbali mbali katika hili kwani lengo ni kujenga Tanzania nzuri leo na kesho kwa vizazi na vizazi
 

Attachments

  • 5.jpg
    5.jpg
    26.5 KB · Views: 46
  • 6.jpg
    6.jpg
    118.5 KB · Views: 106
hizo ni concept tu, na silicon sio future tena, kila siku zinavyokwenda inazidi kuwa haina maana, pengine mpaka huo mji ukikamilika tutakuwa tunaongea organic au quantum au material mengine
 
hahaha wakenya kwa misifa bhanaaa
badala ya kupeleka umeme vijijini wao wanaiga tu
 
hizo ni concept tu, na silicon sio future tena, kila siku zinavyokwenda inazidi kuwa haina maana, pengine mpaka huo mji ukikamilika tutakuwa tunaongea organic au quantum au material mengine

Mkuu wewe ndo unaona ni concept tu, em tafakari miaka 50 ijayo itkuwaje kwa uchumi wa kenya? Itakuwaje kwa teknolojia ya kenya, ifike pahala sisi watanzania tukubali jitihada za wenzetu na tuige mifano yao nasi tujiibidishe, tusiwe watu wa kupuuza kila jema
 
hahaha wakenya kwa misifa bhanaaa
badala ya kupeleka umeme vijijini wao wanaiga tu

Umeme vijijini ndio suluhisho kwa wakenya mkuu? Kwani huu mradi ukimalika hautainufaisha kenya? hautaleta changamoto ya kiuchumi na kuifanya kenya kuwa nchi ya kwanza afrika kwa teknolojia?
 
Wao wanafikiria miaka 30 sisi tunafikiria miaka -30
Ni kweli mkuu wakenya wanawaza mbali sana, wanawadira ya nchi yao miaka 30 mbele sisi hata miaka 5 mbele tu hatuna, tujitafakari kwa kweli, ni wakati wa vitendo na siporojo
 
Mkuu wewe ndo unaona ni concept tu, em tafakari miaka 50 ijayo itkuwaje kwa uchumi wa kenya? Itakuwaje kwa teknolojia ya kenya, ifike pahala sisi watanzania tukubali jitihada za wenzetu na tuige mifano yao nasi tujiibidishe, tusiwe watu wa kupuuza kila jema
ingekuwa sio concept tungeona majengo halisi, siku ikikamilika hio project na tukaona hayo maji na majengo na mimi nitaamini kweli kenya wamejenga huo mji. lakini hizo computer generated graphics zitabaki tu kuwa concept.
 
hahaha wakenya kwa misifa bhanaaa
badala ya kupeleka umeme vijijini wao wanaiga tu

last mile project inahakikisha umeme umeingia hadi kijijini kule mbali kabisa, a million connections a year, tuko njiani mkuu.

 
Safi sana, hii ndio Africa tunayoitaka. Cha msingi waangalie kwenye utekelezaji wake watu wasije kutumia fursa kupiga hela za huo mradi
 
Safi sana, hii ndio Africa tunayoitaka. Cha msingi waangalie kwenye utekelezaji wake watu wasije kutumia fursa kupiga hela za huo mradi

Ni kweli mkuu hilo ni tatizo sana kwa nchi za afrika watu ni wajanja wajanja sana
 
ingekuwa sio concept tungeona majengo halisi, siku ikikamilika hio project na tukaona hayo maji na majengo na mimi nitaamini kweli kenya wamejenga huo mji. lakini hizo computer generated graphics zitabaki tu kuwa concept.
Umesomeka mkuu ila tuwapongeze hata kwa wazo na utayari maana wameonesha wana dhamira, wasi wasi wangu pia ni kuwa watu wachache wapiga dili wanaweza ukwamisha huo mradi
 
Umesomeka mkuu ila tuwapongeze hata kwa wazo na utayari maana wameonesha wana dhamira, wasi wasi wangu pia ni kuwa watu wachache wapiga dili wanaweza ukwamisha huo mradi
na mimi pia wasiwasi wangu upo hapo hapo unaweza google hizi project za kenya
-magari ya nyayo made in kenya
ELEPIC.jpg

-uwanja wa ndege jomo kenyata ambao walisema utakuwa kama wa london wenye lane 3 ila ulipokamilika ukawa wa kawaida tu na lane moja

jamaa ni kawaida kenya wanapenda ku hype mambo mengi lakini hawayatekelezi. mpaka nione ukamilike kwanza nitaamini
 
na mimi pia wasiwasi wangu upo hapo hapo unaweza google hizi project za kenya
-magari ya nyayo made in kenya
ELEPIC.jpg

-uwanja wa ndege jomo kenyata ambao walisema utakuwa kama wa london wenye lane 3 ila ulipokamilika ukawa wa kawaida tu na lane moja

jamaa ni kawaida kenya wanapenda ku hype mambo mengi lakini hawayatekelezi. mpaka nione ukamilike kwanza nitaamini


Nimekupata vema mkuu, nimegoogle hayo magari nimejifunza kitu kikubwa sana, shukrani kwa mchango wako umenifunza jambo hapa
 
Back
Top Bottom