Kendrick Lamar is overrated

Habari ya mjini ni
Big shaq na man's not hot
Ile style hakunaga chini ya jua
 
Mshkaji wangu flan WA karibu Sana ,,anampenda Kendrick kupita kawaida,album ya DAMN kaninunulia,ukitaka kumshawishi mtu apende unachopenda tumia lugha nzuri,mifano,facts,sasa jamaa yako kaja anani attack kama tuna ugomvi..tell him to calm his nerve ,this is not even freestyle battle..haha
Sawa, jaribu kumpa facts kidogo pengine anataka kuona wats more abt Kendrick, if you were going through this thread kuna sehem he said akijua the goodness we see in Kendrick he will be happy so let's spit facts basi, we're all hip hop commentators.
 
AB SOULana
kendrick ni sawa na Ney wa mitego. Alianza kwa cypher kali sasa anarukaruka kama maharage robo kwenye sufuria ya sherehe!
Kila nkisema hivi wananitukana..nna uhakika wameanza kumjua Kendrick juzi juzi..kama kweli unamjua jamaa kipindi kile cha cypher..,WA Leo utamuona anazingua
 
Ab soul fundi mno..ana mstari wake kwenye ngoma flani yupo na Kendrick..mstari huo naupenda Sana..anasema "I been killing this since Cam Made ooh Boy,ooh boy am grown now" hahaha TDE hawakosei
 
Watumia auto tunes, T Pain, Lil Wayne, Future kwa kipindi kile ndiyo walisababisha Nas aseme hip hop is dead. Traditional hip hop ilikua inaenda omega sasa hivi wameibuka kina Desiigner, Migos, Travis, Lil Uzi wanazidi kuwakera wakongwe.
Kundi la migos sielewagi wanachoimba sielew wana wimbo gani unaohit
 
AB SOULana
Kila nkisema hivi wananitukana..nna uhakika wameanza kumjua Kendrick juzi juzi..kama kweli unamjua jamaa kipindi kile cha cypher..,WA Leo utamuona anazingua

Kendrick was hot but leo hii anabebwa na heshima aliyojijengea nyuma kabla ya kufika hapo.Kuna mashabiki bado wapo naye kupitia muziki wake wa awali na pia amepata mashabiki wapya kupitia music anaofanya sasa ndio maana anazidi kuchukua tuzo na kung’aa.Siwezi kukataa kuwa Kendrick kabadili lakini pia kubadilika kwake hakubadilisha ukweli kuwa zile albums za mwanzo alifanya yeye so heshima yake ya mwanzo na hapo alipo itabaki mikononi mwake.Tusubiri aje mwingine wa kumpoteza kisha tutakubaliana na wakati.POETIC JUSTICE
 
Kendrick kweli ukimfikiria kwa mashavu anayopewa inaleta ukakasi sana lakini ukijiuliza kwa game ya sasa ilivyo nina anaweza kumfunika jamaa utakosa jibu au utakuta unawataja tena wakina Drake

Lakini ukimtazama kwa kumlinganiaha na wakali kama Jay z, Kanye West, Nas au Eminem na wengineo utamuona anapea sana.

Uhalisia ni kwamba game imechange sana na wakali hao niliowataja kwa sasa hawakazi tena kama walivyokua wanafanya zamani, trust me bro Jay Z sio yule tena ukichambua album yake mpya utachagua baadhi ya ngoma utazozielewa kama The story of OJ na nyingine chache tu sio kama ilivyokua zamani, au Kanye nae mambo ya familia na mitindo ndio sana nae sio yule tena.

Sasa Kandrick game ya sasa ndio yupo na kina Migos unadhani nini kitatokea kama sio kuvikwa crown tu? Ona tuzo anavyozikomba peke yake eti tuzo kama Gramy anazikodia kirikuu kizipeleke nyumbani jinsi zilivyo nyingi(joking)

Game imechange sana na wakati huu Kendrick anastahili kuwakimbiza kiukweli
 
Safi sana mkuu nimeelewa sana uchambuzi wako na ninaunga mkono...

YOU CAN SEE NEW PEOPLE ARROUND ME JUST WANNA BE FAMOUS, YOU CAN SEE THE MY CITY FOUND ME AND PUT ME ON THE STAGE..
B... dont kill my vibe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…