DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama cha Mapinduzi CCM Kenani Kihongosi , amesema Taifa linahitaji upinzani uliokomaa na wenye kuzingatia maadili ya kisiasa, badala ya siasa za kushangilia misiba na kuhamasisha chuki.
Akizungumza kwenye Kikao cha Shina Namba Moja, Singida Mjini leo Januari 19, 2026, Kihongosi amesema haipendezi kuona chama cha siasa au mwanasiasa akishangilia kifo cha mtu, akisisitiza kuwa siasa za namna hiyo hazina tija kwa maendeleo ya nchi.
“Leo mtu anafariki, eti mtu anashangilia halafu hicho ni chama cha siasa. Tunahitaji upinzani uliokomaa. Ndiyo maana Chama cha Mapinduzi tutaendelea kuwalea hawa watu tutawalea Chadema wakue, CUF wakue, ACT wakue, hawa wote ni watoto wetu, tunawalea bado,” amesema.
Akizungumza kwenye Kikao cha Shina Namba Moja, Singida Mjini leo Januari 19, 2026, Kihongosi amesema haipendezi kuona chama cha siasa au mwanasiasa akishangilia kifo cha mtu, akisisitiza kuwa siasa za namna hiyo hazina tija kwa maendeleo ya nchi.
“Leo mtu anafariki, eti mtu anashangilia halafu hicho ni chama cha siasa. Tunahitaji upinzani uliokomaa. Ndiyo maana Chama cha Mapinduzi tutaendelea kuwalea hawa watu tutawalea Chadema wakue, CUF wakue, ACT wakue, hawa wote ni watoto wetu, tunawalea bado,” amesema.