Mkuu, mjitahidi pia pamoja na kuripoti matukio (jambo ambalo ni zuri) muwe na innovations!
Jitahidini kuanzisha mijadala ya hoja inayofikirisha. Aidha, msimuachie kiongozi wa chama peke yake ndio awe anaibua hoja kila siku. Wengine mbona hamuanzishi hoja ?
Kukosoa wengine kosoeni, ila fanyeni zaidi ya hapo. Kama chama kuweni wabunifu, fanyeni mambo ambayo ni unique! Hayajawai kufanywa kwenye nchi hii.
Kukosoa tu haitoshi, kukosoa ni kazi rahisi isiyohitaji kutumia akili nyingi na kila mtu anaweza kuifanya. Tunataka tuone kama chama mna innovate nini?. Tunataka tuone humo kuna watu wengi wanajenga hoja madhubuti kila mara na sio kumuachia zito tu.Kuweni wabunifu. Kuongeza ufanisi, ombeni ushauri kwa jamii kwamba mfanye nini ili kuwa chama bora kuliko vyama vingine.Halafu pale mnapokwama, msione aibu kujishusha ili mpate support. Jikubalini mlivyo pamoja na udhaifu wenu na uimara wenu.
Kwa sasa ACT bado ni changa mno, wekezeni nguvu kwenye kujenga competent human resources kwenye chama. Andaeni viongozi bora na hakikisheni wanakuwa motivated. Msisubirie kugombea from no where na ishu nyingine kama hizo. Msimtegemee zitto peke yake, ninyi ni chama.