Kazi za tanesco Northern zone.

Kazi za tanesco Northern zone.

Naomba kuuliza majina ya watu waliofanya interview ya written kanda ya kaskazini yameshatoka? Kama yametoka mtu ambae haishi Tanga anapataje taarifa kwamba anatakiwa kwenda kwenye oral?
 
Naomba kuuliza majina ya watu waliofanya interview ya written kanda ya kaskazini yameshatoka? Kama yametoka mtu ambae haishi Tanga anapataje taarifa kwamba anatakiwa kwenda kwenye oral?
Majina yamebandikwa ofisi za Mikoa ya Kanda ya Kasikazini, Pia waliokidhi vigezo wamepigiwa simu na kutumiwa ujumbe mfupi
 
Yaan ndo naona hizi conversations na kuhusu PDF ya customer relations officer iwekeni hapa naona interview ni kesho sijapata majina yaliyoitwa
 
Ila sijajua mpaka leo kwanini taasisi zingine zinaachwa kuendelea na uhuni kama TANESCO; wakati wa kutangaza kazi wanaweka tangazo kwenye tovuti ila wakati wa kuita watu kwenye usahili wanabandika kwenye ofisi zao na kupiga simu na bosheni ya email.

Mimi nilishawahi kufanya usaili TANESCO mwaka 2013; cha kushangaza tunaingia kwenye usaili bado wanajiuliza kama kuna watu wengine simu zao zilishapatikana au laa! yaani hawajui kua Alex anaweza kuona jina la Amina kwenye tovuti na kumjulisha wakati Amina anaweza kua nje ya mtandao wa simu na asipatikane.
 
Waliokidhi vigezo wameshapigiwa simu na kutumiwa ujumbe wa tarehe ya kufanyiwa usahili
Simu wamepiga ila ujumbe kwa kweli hawajatuma, tungeomba mtume ujumbe maana mlipopiga simu wengine walikuwa kwenye kelele lakini seemu ya kufanyia ndo ilikuwa ngumu kuielewa.
 
Tuhuma zako zilizojengwa kwa hisia tumezipokea, Waliokidhi wote wamepigiwa simu na majina yamebandikwa ofisi ya Mikoa ya Kanda husika.waliba wote na kukidhi vigezo wamepigiwa simu na kutumiwa ujumbe na zoezi limefanyika kwa uadilifu mkubwa sana.Unapotoa tuhuma za hisia unatusikitisha sana.Tunaomba jina lako na nafasi uliyoomba tukupatie majibu kamili badala ya kututuhumu
Sawa tunashukuru simu tumepigiwa ila ujumbe hatujapata na sehemu ya usaili hatujaishika vizuri. 0714712474 Naomba kujuzwa pls.
 
Hivi unapofanya usaili kuwa muda mrefu yaani karibu wiki ya pili bado kuna usaili unaendelea maana yake nini.Kanda ya Tanga TANESCO mnawezaje kuwakalisha watu muda mrefu hivyo eti kusubiri "usaili wa mahojiano" hivi mnafahamu kuwa watu wametoka maeneo mbali mbali na hawana pesa za kujikimu.Angalieni namna bora ya kukamilisha michakato ambayo haitaleta walakini LAKINI siyo kwa style ambayo mnaendelea nayo
 
Hivi unapofanya usaili kuwa muda mrefu yaani karibu wiki ya pili bado kuna usaili unaendelea maana yake nini.Kanda ya Tanga TANESCO mnawezaje kuwakalisha watu muda mrefu hivyo eti kusubiri "usaili wa mahojiano" hivi mnafahamu kuwa watu wametoka maeneo mbali mbali na hawana pesa za kujikimu.Angalieni namna bora ya kukamilisha michakato ambayo haitaleta walakini LAKINI siyo kwa style ambayo mnaendelea nayo
Tumepokea lalamiko lako tutaliwasilisha kwa idara yetu ya rasilimali watu
 
Ivi izi ajira mnazota za Temporary wa mwaka mmoja mmoja ambazo watu mnawafanyia usaili,je mwisho wa siku uko baadae inakuwaje hapo,yaani mnakuja kuwapa ajira za Permanent uko baadae ama mnawamwaga
 
Wanamwagwa aisee
Ivi izi ajira mnazota za Temporary wa mwaka mmoja mmoja ambazo watu mnawafanyia usaili,je mwisho wa siku uko baadae inakuwaje hapo,yaani mnakuja kuwapa ajira za Permanent uko baadae ama mnawamwaga
 
Mi naomba TANESCO mbadilike ktka saili zenu syo mtu matokeo ya mchujo anasubiria siku mbili mzima wakat kuna taasisi siku Moja mnapga usaili kada tatu na majibu ni sku hyo hyo ,yani mtu unalala Hali ya kuwa unafahamu kuwa kesho AsubuhI ni STENDI au Kwenye ORAL.
 
Sawa tunashukuru simu tumepigiwa ila ujumbe hatujapata na sehemu ya usaili hatujaishika vizuri. 0714712474 Naomba kujuzwa pls.
Nilipigiwa simu kualikwa kwenye usaili tar 26 June 2019, nikatoka Dar tar 25 nikafika Tanga, asubuhi naenda kwenye eneo la usaili naambiwa usaili ulifanyika tangu tar 24, tulikuwa watu kadhaa tukaambiwa tumechelewa. Sasa tukawa tunajiuliza kwann tulidanganywa tarehe? Na kama walibadilisha tarehe ya usaili kwann wasipige simu kwa watu wote?
Kwakweli TANESCO mlinikwaza sio mm tu hata watu wengine waliumia maana wengine walitoka Mbeya tumetumia nauli na tumelala nyumba za wageni. TUNAOMBA MUWE MAKINI
 
Back
Top Bottom