ntamaholo
JF-Expert Member
- Aug 30, 2011
- 12,906
- 6,909
Wednesday, April 25, 2012
Mwenyekiti wa Wakuu wa Majeshi ya Polisi Nchi za Mashariki mwa Africa ambaye pia ni Inspekta Jenerali wa Polisi Rwanda, Emmanuel Gasana (kushoto) akisaini kitabu cha wageni katika ofisi za wizara ya Mambo ya Ndani jana jijini Dar es Salaam aliopo nchini katika ziara ya kufuatilia utekelezaji wa maazimio ya mkutano wa kumi na tatu wa wakuu wa Majeshi ya Polisi wa EAPCCO, mkutano uliofanyika nchini Rwanda mwezi septemba 2011. Ziara hii ni pamoja na kuimarisha ushirikiano baina ya Majeshi ya nchi za mashariki mwa Afrika. Kulia ni Kamishna wa Operesheni, Paul Chagonja.
Mwenyekiti wa Wakuu wa Majeshi ya Polisi Nchi za Mashariki mwa Africa ambaye pia ni Inspekta Jenerali wa Polisi Rwanda, Emmanuel Gasana (kulia) akipokea zawadi kutoka kwa Kamishna wa Operesheni wa Jeshi la Polisi Tanzania, Paul Chagonja kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania jana jijini Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Dar es Salaam. IGP wa Rwanda yupo katika ziara ya kufuatilia utekelezaji wa maazimio ya mkutano wa kumi na tatu wa wakuu wa Majeshi ya Polisi wa EAPCCO, mkutano uliofanyika nchini Rwanda mwezi septemba 2011. Ziara hii ni pamoja na kuimarisha ushirikiano baina ya Majeshi ya nchi za mashariki mwa Afrika.
[h=3]Who's Online[/h]
We have 91 guests online
[h=3]News and Events[/h]
Copyright © 2012. Tanzania Police Force.
TANGAZO LA AJIRA Jeshi la Polisi liko katika mchakato wa kuajiri vijana kujiunga na Jeshi kupitia mashuleni. Tumeamua kuurudia utaratibu ambao ulikuwepo zamani wa kuajiri moja kwa moja toka mashuleni ambao ulikuwepo siku za nyuma kutokana na mahitaji halisi ya Jeshi la Polisi kwa sasa. Hivi sasa Jeshi la Polisi linakabiliwa na changamoto mbalimbali zinazotokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia, ongezeko la uhalifu mpya kama vile wizi wa kutumia mtandao, usafirishaji haramu wa binadamu na kadhalika. Wahalifu wanaohusika na matukio kama hayo, wamekuwa wakitumia mbinu mpya na utaalamu wa hali ya juu. Aidha, Jeshi la Polisi linaendelea na Programu yake ya maboresho. Maboresho haya yanalenga kulifanya Jeshi kuwa la Kisasa zaidi ambalo litatelekeza majukumu yake kwa Weledi huku likiwa karibu zaidi na raia katika utendaji wake wa kila siku. Kutokana na changamoto hizo, Jeshi la Polisi linahitaji kuajiri, vijana wasomi, wenye utashi, ari na nia ya kufanya kazi za Polisi na wenye fikra na mtazamo unaoendana na dunia ya sasa. Vijana hawa watakuwa viongozi na chachu katika kuleta mabadiliko yanayokusudiwa ndani ya Jeshi la Polisi. A: SIFA/VIGEZO VYA MWOMBAJI
|
[h=3]Who's Online[/h]
We have 91 guests online
[h=3]News and Events[/h]
- PERFORMANCE AUDIT REPORT ON THE MANAGEMENT OF TRAFFIC INSPECTIONS AND SPEED LIMITS
- Hospitali ya Kilwa Road yaanza kutibu Magonjwa ya akina mama
- Tender for supply of minbus and motorcycle
- TANGAZO LA AJIRA B 2012
- Japan yatoa msaada kwa serikali ya Tanzania
- BP yamwaga msaada kwa kikosi cha usalama barabarani
- Shirikisho la Upelelezi la Ujerumani latoa msaada
Copyright © 2012. Tanzania Police Force.