BM X6
JF-Expert Member
- Nov 24, 2020
- 1,360
- 4,149
Hello Wazito hope wote ni wazima...
Jana bhana katika story za hapa na pale na rafiki yake blaza ametokea mbeya amekuja Dar likizo akawa ananikumbushia hustle walizopitia kipindi hicho na Kaka yangu kabla hawaja pata kazi za kueleweka,
Kaka yangu na rafiki yake chuo walichukua Bachelor of Arts with Education (BAEd) Kazi anayoifanya blaza angu inafanana na alichokisomea yani ni mwalimu, huyu rakifi yake sasa ndio anafanya kazi tofauti na alichokisomea, Sasa huyu bro jana (rafk yake bro angu) akawa ananiambia "Mdogo wangu hadi utoboe kwenye haya maisha yanahitaji kujituma na uvumilivu wa hali ya juu sana pamoja na kuishi na watu vizuri, pia kubaliana na chochote kile kinachotokea kwenye maisha yako, haya maisha yanaweza kukupeleka sehemu ambayo hata hukuiwazia na ikawa ina neema kuliko Ile uliyoiwazia" aliendelea kunambia "kwanza kama sio kaka yako Mimi nisingekua hapa Leo yani nafasi niliyopo alitakiwa kuichukua kaka yako lakini aliikataa na kuniconnect Mimi, sikufichi mdogo wangu hii kazi ninayofanya ina maslahi makubwa na posho za kutosha, Yani kama vigezo sio vyeti basi hata mtu aliyeishia Darasa la Saba anaweza elekezwa na akaifanya vizuri tu, twenzetu tukapark gari kwanza naona bro ako ni kama harudi leo" mwisho wa kunukuu, Honestly, maelezo ya huyu rafiki yake na bro yalinisisimua sana
Ukiangalia maisha ya hawa watu wawili, Blaza angu ameachwa hatua nyingi sana, Kaka yangu mm kikubwa anachomiliki ni kiwanja na Toyota IST, rafiki yake Sasa ana gari mbili Toyota IST na Crown athlete na nyumba mbili moja ipo Dar nyingine ipo huko huko mbeya anapofanyia Kazi pamoja na kiwanja, in short Sasa hivi jamaa anakula mema ya nchi kiasi kwamba najiuliza ilikuaje bro akaiachilia hii nafasi, Cha ajabu ni kwamba bro anasema hata ikitokea nafasi nyingine bado atam recommend mtu mwingne badala yake
Sasa kilichofanya nianzishe Uzi huu ni kutaka kujua ni kazi gani ambazo kama sio vyeti vya shule basi hata mtu aliyeishia Darasa la Saba anaweza kuifanya vizuri tu kwa maelezo, Najua kuwa wengine humu ndio mnazozifanya hizo kazi ebu tuelezeeni hapa pamoja na changamoto zake.
Jana bhana katika story za hapa na pale na rafiki yake blaza ametokea mbeya amekuja Dar likizo akawa ananikumbushia hustle walizopitia kipindi hicho na Kaka yangu kabla hawaja pata kazi za kueleweka,
Kaka yangu na rafiki yake chuo walichukua Bachelor of Arts with Education (BAEd) Kazi anayoifanya blaza angu inafanana na alichokisomea yani ni mwalimu, huyu rakifi yake sasa ndio anafanya kazi tofauti na alichokisomea, Sasa huyu bro jana (rafk yake bro angu) akawa ananiambia "Mdogo wangu hadi utoboe kwenye haya maisha yanahitaji kujituma na uvumilivu wa hali ya juu sana pamoja na kuishi na watu vizuri, pia kubaliana na chochote kile kinachotokea kwenye maisha yako, haya maisha yanaweza kukupeleka sehemu ambayo hata hukuiwazia na ikawa ina neema kuliko Ile uliyoiwazia" aliendelea kunambia "kwanza kama sio kaka yako Mimi nisingekua hapa Leo yani nafasi niliyopo alitakiwa kuichukua kaka yako lakini aliikataa na kuniconnect Mimi, sikufichi mdogo wangu hii kazi ninayofanya ina maslahi makubwa na posho za kutosha, Yani kama vigezo sio vyeti basi hata mtu aliyeishia Darasa la Saba anaweza elekezwa na akaifanya vizuri tu, twenzetu tukapark gari kwanza naona bro ako ni kama harudi leo" mwisho wa kunukuu, Honestly, maelezo ya huyu rafiki yake na bro yalinisisimua sana
Ukiangalia maisha ya hawa watu wawili, Blaza angu ameachwa hatua nyingi sana, Kaka yangu mm kikubwa anachomiliki ni kiwanja na Toyota IST, rafiki yake Sasa ana gari mbili Toyota IST na Crown athlete na nyumba mbili moja ipo Dar nyingine ipo huko huko mbeya anapofanyia Kazi pamoja na kiwanja, in short Sasa hivi jamaa anakula mema ya nchi kiasi kwamba najiuliza ilikuaje bro akaiachilia hii nafasi, Cha ajabu ni kwamba bro anasema hata ikitokea nafasi nyingine bado atam recommend mtu mwingne badala yake
Sasa kilichofanya nianzishe Uzi huu ni kutaka kujua ni kazi gani ambazo kama sio vyeti vya shule basi hata mtu aliyeishia Darasa la Saba anaweza kuifanya vizuri tu kwa maelezo, Najua kuwa wengine humu ndio mnazozifanya hizo kazi ebu tuelezeeni hapa pamoja na changamoto zake.