Kauli za TPDC zaonyesha Katibu Mkuu Nishati katumbuliwa kwa kutetea sheria ya manunuzi

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,468
911,184
TPDC walilalama zoezi la zabuni za vitalu vya gesi asilia liliingiliwa na Waziri husika Muhongo kinyume na sheria ya manunuzi.

Huyu katibu mkuu aliyetumbuliwa alikuwa msimamo mmoja na TPDC kuwa sheria ya manunuzi iheshimiwe na Muhongo aache kuingilia.

Muhongo ana kampuni ya kichina anayotaka ipewe ugali huo na sasa wapinzani wake wameanza kung'olewa kuwapisha wateule wapya watakaohakikisha wachina wanalamba asali!

Ukiukwaji wa sheria ya manunuzi ni matumizi mabaya ya madaraka na yanaashiria harufu kali ya ufisadi.

Uongozi mzima wa TPDC sitashangaa ukitumbuliwa ili kupisha madudu haya ya hawa walaji.

Huyu Muhongo pamoja na kugubikwa na kashfa kibao leo anaonekana ni jembe sasa nimeanza kujua sababu kumbe ni kulinda Milo ya wakubwa serikalini.

Halafu hawa hawa wanatumbua wasiyo na hatia kumbe wao ndiyo wanapaswa kutumbuliwa!
 
TPDC walilalama zoezi la zabuni za vitalu vya gesi asilia liliingiliwa na Waziri husika Muhongo kinyume na sheria ya manunuzi.

Huyu katibu mkuu aliyetumbuliwa alikuwa msimamo mmoja na TPDC kuwa sheria ya manunuzi iheshimiwe na Muhongo aache kuingilia.

Muhongo ana kampuni ya kichina anayotaka ipewe ugali huo na sasa wapinzani wake wameanza kung'olewa kuwapisha wateule wapya watakaohakikisha wachina wanalamba asali!

Ukiukwaji wa sheria ya manunuzi ni matumizi mabaya ya madaraka na yanaashiria harufu kali ya ufisadi.

Uongozi mzima wa TPDC sitashangaa ukitumbuliwa ili kupisha madudu haya ya hawa walaji.

Huyu Muhongo pamoja na kugubikwa na kashfa kibao leo anaonekana ni jembe sasa nimeanza kujua sababu kumbe ni kulinda Milo ya wakubwa serikalini.

Halafu hawa hawa wanatumbua wasiyo na hatia kumbe wao ndiyo wanapaswa kutumbuliwa!


Weka ushahidi hapa, kuandika kila mtu anaweza!
 
Shikamoo JPM!

Kama maelezo haya ni ya kweli basi upo sahihi kwa 100%... nakuunga mkono kumtumbua huyo kimbelembele!

Wewe ndo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania! Wewe ndie kioo na watendaji wote wanatakiwa kufuata yale unayofanya wewe na kutenda kinyume ni kama kukupinga!!

Huyo Katibu Mkuu si profesa huyo?! Au ni profesa wa mitishamba?! Au kwavile wewe Mtukufu Rais sio profesa ndo akaamua kukudharau?!

Haiwezekani! Narudia; HAIWEZEKANI kwamba profesa mzima hakufahamu uliponunua Bombardier 2 sheria ya kilofa ya manunuzi uliitupa kapuni!

Sasa yeye ni nani hadi afanye kinyume na afanyavyo rais wa nchi?! Ikiwa rais wa nchi ananunua midege ya mabilioni ya pesa bila kufuata sheria ya manunuzi; sasa yeye ni nani hata atende kinyume na rais?! Ni huo uprofesa wake; au? Au lengo lake ni nini hasa?! Ni nini hiyo kama sio uchochezi wa kutaka kujionesha yeye ni smart ndo maana anafuata sheria na rais ni nanii ndo maana kapiga kanyaga twende!!

Tia adabu huyo... Mchochezi Mkubwa wa mwezi March!
 
Wachina! Wachina! Daah kila kitu Wachina!
Nahisi hawa ndo baadaye watakuwa wale malaika wa kutufungia social media..!
 
Shauri yenu nyie mnaowaamini wanasi-hasa....wanasi-hasa wote sirini wanapiga hasa huku Africa....ubunge ni expensive hela inabidi itafute ku maintain ubunge...labda wale ambao ni wafanyabiashara matajiri....well sasa hivi ni zamu yao hivyo tulieni tuu!
 
Back
Top Bottom