Kauli za Rais zinavunja moyo watendaji wake

Kauli za Rais zinavunja moyo watendaji wake

boyson onlye

JF-Expert Member
Joined
Sep 13, 2015
Posts
1,108
Reaction score
1,404
Nakumbuka haya maneno
Mwanangu ukiwa na furaha usiahidi Maana utashindwa kutimiza ahadi zako furaha ikiisha, pia ukiwa na hasira usihukumu maana utakuja jutia maamuzi yako.

Muheshimiwa kauli uliyotoa ungetafakali Mara mbili, kiongozi unapomwambia kama hautaki achia Ngazi, unawapa kiburi hawa anaowaongoza na kumfanyia vitu vya makusudi, kauli uliyotoa kwa viongozi juu ya machinga ni kauli ambayo inavunja moyo kwa watendaji wako,

Leo hii kiongozi gani mwenye ujasiri wa kumtoa machinga barabarani? Kiongozi gani wa kuja kukueleza juu ya shida zinazosababishwa na machinga? Mkuu unatakiwa kufahamu mwananchi kulalamika ni kawaida yake, wanalalamika Ushuru wa parking umepamda ila gari mjini hazijapungua, Leo hii machinga wamekuwa Kero yaani wanafanya makusudi kabisa kwa sababu Raisi amesema, Barabara wamefunga, wanafanya biashara mbele ya duka la mtu na mengineyo mengi, sasa nani atalikomesha hili, swala la machinga halijaanza leo wala jana, kumbuka mkuu hawa machinga hawalipi kodi ya aina yeyote, sasa andaeni mkakati wa machinga Walipe kodi
 
morali chini, machinga watajaa barabara zote, wenye maduka watafaulisha bidhaa zao kwa machinga, kodi 0.tutaendelea siku tutakayoamua kwa dhati kutenganisha siasa na utendaji. creativity ya watumishi itakua kubwa wakipewa nafasi. kwa hali ya sasa watu wametulia tu wanasubiri maagizo ndo wafanye
 
Ukipita na gari inabidi uende taratibu na hakuna parking, hili agizo halijakaa sawa
 
morali chini, machinga watajaa barabara zote, wenye maduka watafaulisha bidhaa zao kwa machinga, kodi 0.tutaendelea siku tutakayoamua kwa dhati kutenganisha siasa na utendaji. creativity ya watumishi itakua kubwa wakipewa nafasi. kwa hali ya sasa watu wametulia tu wanasubiri maagizo ndo wafanye
Nafikili baada ya miongo kadhaa kupita
 
Ukweli lile onyo kutoka kwa mkuu kwa kuutangazia uma halikukaa sawa, limewapa nguvu wamachinga kuliko watanzania wengine wenye haki. Barabarani sasa hivi ni kero kabisa kwa kweli, hata wagonjwa watafia kwenye magari kwa kishindwa kuwahi hospitali. Naamini mkuu hakushindwa kuwapa maelekezo kimyakimya hawa viongozi kwamba wawaache hao machinga bila wao kujua kwamba kuna amri hiyo, wangetulia tu maana wangeona hawasumbuliwi tena., au lilikuwa na maana gani?
 
Ukweli lile onyo kutoka kwa mkuu kwa kuutangazia uma halikukaa sawa, limewapa nguvu wamachinga kuliko watanzania wengine wenye haki. Barabarani sasa hivi ni kero kabisa kwa kweli, hata wagonjwa watafia kwenye magari kwa kishindwa kuwahi hospitali. Naamini mkuu hakushindwa kuwapa maelekezo kimyakimya hawa viongozi kwamba wawaache hao machinga bila wao kujua kwamba kuna amri hiyo, wangetulia tu maana wangeona hawasumbuliwi tena., au lilikuwa na maana gani?
Ni shida ya kupenda kusifiwa
Angewaambia viongozi angesifiwa na nani
 
Yaani mjini kumekuwa vururuvururu..!, watu wanapanga vitu katikati ya barabara bila uoga wa aina yoyote ile, tena anapanga mbele ya duka la mtu anaelipa kodi lukuki na kumfungia kabisa njia ya wateja kwenda dukani kwake.., hii hapana kwa kweli, watz hatuwezi kukubali uonevu huu wa waziwazi. Pia wamachinga ni mwanya unaotumiwa na wafanya biashara wakubwa kukwepa kodi
 
Kwa matamko ya Mungu wa DSM acha mh Rais awanyooshe tu maana alizidi sifa za kijinga
 
Mhe Rais inabidi ashauriwe upya tena, machinga ni tatizo.
Nani alikwambia kuwa Bwana yule anashaurika?

Na ukithubutu tu kumshauri, atakupiga mkwara kuwa usimjaribu........

Na ataviagiza vyombo vyake vya usalama ufunguliwe mashitaka ya uchochezi!
 
Back
Top Bottom