Kauli ya Rais Samia kuhusiana na umuhimu wa katiba, imethibitisha haya...

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,559
41,077
Kauli ya Rais kuhusiana na umuhimu wa katiba, imethibitisha yafuatayo:

1) Rais wetu hajui maana wala kuelewa uzito wa Katiba ya Nchi

2) Rais wetu haelewi kuwa kinachowekwa kwenye kitabu kinachoitwa katiba ni maamuzi ya Wananchi wa nchi husika juu ya utawala wa nchi. Hivyo kitabu hicho hakipewi heshima kwa sababu ni kitabu bali kwa sababu ni rejea ya yale wananchi waliyoyaamua kuhusiana na utawala wa nchi kuanzia taratibu za kuwapata watawala wa wa nchi, bamna muundo wa utawala unavyotakiwa kuwa, namna ya upatikanaji wa sheria, n.k.

3) Rais wetu hajui kuwa bila katiba, hata yeye binafsi, hana tofauti na Khadija Kopa au karani wa kiwanda cha konyagi.

4) Rais hajui kuwa bila katiba, yeye siyo Rais wala siyo kiongozi yeyote. Bila katiba hana uwezo wa kumpa madaraka mtu yeyote.

Naamini mtu anayetakiwa kupewa shule ya nguvu kuhusiana na katiba ni Rais wetu.

Bahati nzuri au mbaya nchi yetu inavumilia kila aina ya uozo. Ingekuwa ni nchi ambazo wananchi wake hawavumilii uozo wa aina yoyote, ofisi ya Rais ingekuwa katika wakati mgumu sana baada ya Rais kutoa kauli inayoashiria kuwa katiba aliyoapa kuulinda si chochote na si lolote, ni kitabu tu kama cha Abunuwasi. Na fikra hizi ndizo zinazowafanya watawala wetu kutoheshimu katiba. Wakati kiuhalisia Rais kutoheshimu katiba ni uhaini dhidi ya umma.

Rais kama hajui uzito wa katiba, kwa kweli ni hatari kubwa sana. Wahusiaka wampeleke darasani Rais wetu haraka sana ili asiendelee kutamka mambo ya ajabu yanayofisha Taifa na nafasi yake.
 
Katiba Mpya ni baada ya Elimu hayo mengine ni kujifariji

Watu wanahitaji Katiba Mpya ila wanahitaji zaidi maendelea kuliko hiyo Katiba Mpya maana haileti ugali mezani.
Ni fikra za kijinga kabisa kufikiria kuwa mahitaji ya Watanzania ni ugali tu.

Ni punguani pekee ambaye hawezi kuoanisha maisha ya kila siku, ikiwa ni pamoja na mahitaji ya lazima kwa wananchi, na mifumo ya utawala wa nchi ambayo inaunda sera za kiuchumi na kusimamia haki za kijamii.
 
Ni fikra za kijinga kabisa kufikiria kuwa mahitaji ya Watanzania ni ugali tu.

Ni punguani pekee ambaye hawezi kuoanisha maisha ya kila siku, ikiwa ni pamoja na mahitaji ya lazima kwa wananchi, na mifumo ya utawala wa nchi ambayo inaunda sera za kiuchumi na kusimamia haki za kijamii.
Kwa Sasa mahitaji ya ugali ndio kipaombele Ili watu wawe na Lishe ndio waweze kujadili hiyo Katiba.

Kwa Kaa Kwa kutulia, maendeleo ni muhimu kuliko hayo makaratasi mnaita katiba Mpya.
 
Ni fikra za kijinga kabisa kufikiria kuwa mahitaji ya Watanzania ni ugali tu.

Ni punguani pekee ambaye hawezi kuoanisha maisha ya kila siku, ikiwa ni pamoja na mahitaji ya lazima kwa wananchi, na mifumo ya utawala wa nchi ambayo inaunda sera za kiuchumi na kusimamia haki za kijamii.
Ni fikra za kijinga kabisa kufikiria kuwa mahitaji ya Watanzania ni ugali tu.

Ni punguani pekee ambaye hawezi kuoanisha maisha ya kila siku, ikiwa ni pamoja na mahitaji ya lazima kwa wananchi, na mifumo ya utawala wa nchi ambayo inaunda sera za kiuchumi na kusimamia haki za kijamii.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Katiba Mpya ni baada ya Elimu hayo mengine ni kujifariji

Watu wanahitaji Katiba Mpya ila wanahitaji zaidi maendelea kuliko hiyo Katiba Mpya maana haileti ugali mezani.
22d9b01d375df1d50d67f38c924cda3c.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kasemaje tena huko mkuu?
Rais kasema kuwa katiba ni kitabu. Na kitabu hakileti maendeleo.

Kwa kauli yake hii, kwake yeye katiba siyo muhimu, nchi inaweza kwenda bila katiba.

Nadhani baadaye atakuja kusema hata sheria siyo muhimu kwa sababu ni makaratasi. Na makaratasi hayawezi kuzuia chochote.

Hivyo tuishi kama ngiri wa porini. Kila mmoja aishi kwa kadiri ya urefu wa kamba yake.
 
Mosi, hata Wafanyeje Katiba haiwezi kuwa mpya itakuwa ni hii hii ila imerekebishwa pakubwa

Kama Wananchi hawajui hata namna ya kuchagua Wabunge na Madiwani na kuwaacha Wapite bila kupingwa kinyume kabisa cha Katiba unadhani Wananchi hao wanaweza kutengeneza Katiba?!

Mwisho utengenezaji wa Katiba na Mbio za Mwenge lazima ziende opposite direction 😂😂🔥
 
Kwa Sasa mahitaji ya ugali ndio kipaombele Ili watu wawe na Lishe ndio waweze kujadili hiyo Katiba.

Kwa Kaa Kwa kutulia, maendeleo ni muhimu kuliko hayo makaratasi mnaita katiba Mpya.
Ndiyo maana nasema wewe ni mjinga kupindukia kwa sababu hujui hata maana ya maendeleo, kwa sababu hujui kuwa mataifa yanatengeneza katiba nzuri ili kupata maendeleo.

Katiba ndiyo kiwezeshi kikuu cha maendeleo ya kichumi, kiutamaduni na kijamii.
 
Back
Top Bottom