Kauli mbiu ya Lowassa ina utata!

Kauli mbiu ya Lowassa ina utata!

walonge

Member
Joined
Aug 1, 2010
Posts
25
Reaction score
3
Wadau, nimejaribu kuidadisi na kuichambuwa kwa kina kauli mbiu ya Mh. Edward Lowasa kuwa "ANAUCHUKIA UMASIKINI" nahisi ina utata na pengine ni ishara ya kumjuwa ukweli wa moyo wake.

Hebu tujiulize kwa kiswahili sahihi mtu akichukia umasikini ni vigumu kumpenda masikini sababu umasikini ni hali anayokabiliwa nayo mtu masikini. Sasa utawezaje kumsaidia mtu unayemchukia?

Ikiwa kinyume cha umsikini ni utajiri je, kauli hiyo ya kuuchukia umasikini wa masikini walio wengi Tanzania, haitoshi kua​mini kwamba anaupenda Utajiri wa matajiri walio wachache Tanzania?

Watanzania tumshukuru mungu walau hili lowasa kaliweka sawa na tumefunuliwa yaliomoyoni mwake.
 
Siasa ni utaratibu wa maisha mtu anavyoamua yawe kwake na,kujalibu kushawishi wengine waishi maisha anayotaka yeye kwa leo mm nimefafanua siasa ni nn ila kuhusu uyu mzee na kauli zake ni moja ya siasa utakuwa na jibu zuri sasa
 
Kuna tofauti kubwa sana Kati ya maskini na umaskini, mwasisi wa taifa la India alishawahi kusema hate the sin, love the sinner hii ni katika kutofautisha dhambi na mdhambi, hoja yako dhaifu mno
 
Masikini na Umasikini ni vitu viwili tofauti sana. Moja ni mtu na la pili ni hali. Ila swali lako la msingi linabaki palepale mkuu.

Je anawapenda masikini ? na ameshafanya nini kwa hao maskini over past 15 years. Toa ule miaka baada ya kufukuzwa uwaziri mkuu.
 
unatofautishaje kati ya mtu masikini na hali yake ya umasikini?
 
Masikini na Umasikini ni vitu viwili tofauti sana. Moja ni mtu na la pili ni hali. Ila swali lako la msingi linabaki palepale mkuu.

Je anawapenda masikini ? na ameshafanya nini kwa hao maskini over past 15 years. Toa ule miaka baada ya kufukuzwa uwaziri mkuu.

huna hoja na nina wasiwasi na akili yako!!!
 
Mleta uzi nikuulize wewe binafsi unaupenda umaskini? Kama jibu lako ni ndio unamatatizo kichwani na kama ni hapana uzi wako ni uharo mtupu.
Kwa kifupi hakuna anayependa umaskini
 
Wadau, nimejaribu kuidadisi na kuichambuwa kwa kina kauli mbiu ya Mh. Edward Lowasa kuwa "ANAUCHUKIA UMASIKINI" nahisi ina utata na pengine ni ishara ya kumjuwa ukweli wa moyo wake.

Hebu tujiulize kwa kiswahili sahihi mtu akichukia umasikini ni vigumu kumpenda masikini sababu umasikini ni hali anayokabiliwa nayo mtu masikini. Sasa utawezaje kumsaidia mtu unayemchukia?

Ikiwa kinyume cha umsikini ni utajiri je, kauli hiyo ya kuuchukia umasikini wa masikini walio wengi Tanzania, haitoshi kua​mini kwamba anaupenda Utajiri wa matajiri walio wachache Tanzania?

Watanzania tumshukuru mungu walau hili lowasa kaliweka sawa na tumefunuliwa yaliomoyoni mwake.

Unataka achukie utajiri acha ujinga mawazo mgando ya kiongozi bora ni maskini ni upumbavu uliofanya kenya na rwanda watuache mbali...lowasa anapenda kitu kzur tuliona miaka yake michache alivyofunika udhaifu wa serikali ya awamu ya nne kabla kna membe hawajaanza kudanganya JK kwa interest zao za kutaka uongozi ambao atauskia kwenye bomba. ...lowasa ndan ya mda mfupi shule za kata zilijengwa cz is a commanding leader na anaogopeka naamini akiwa rais mchakamchaka wa maendeleo utakua safi kumbuken wakat wa utawala wa mkapa watu wa juu walkula ila wananchi walipata maendeleo sana na kpato bnafsi kilipanda ata marekani walaji wapo ila nchi inaenda
 
Mnashangaa nini..??Kuhusu kauli zake..!!!! Kama mgombea binafsi angekubaliwa...Tungepata mtu muadlifu anayekubaliwa na watu Wengi na msafi...!!!!
 
Wadau, nimejaribu kuidadisi na kuichambuwa kwa kina kauli mbiu ya Mh. Edward Lowasa kuwa "ANAUCHUKIA UMASIKINI" nahisi ina utata na pengine ni ishara ya kumjuwa ukweli wa moyo wake.

Hebu tujiulize kwa kiswahili sahihi mtu akichukia umasikini ni vigumu kumpenda masikini sababu umasikini ni hali anayokabiliwa nayo mtu masikini. Sasa utawezaje kumsaidia mtu unayemchukia?

Ikiwa kinyume cha umsikini ni utajiri je, kauli hiyo ya kuuchukia umasikini wa masikini walio wengi Tanzania, haitoshi kua​mini kwamba anaupenda Utajiri wa matajiri walio wachache Tanzania?

Watanzania tumshukuru mungu walau hili lowasa kaliweka sawa na tumefunuliwa yaliomoyoni mwake.
Rais wetu ni Lowassa kwa muda mfupi lowasa alipokua madarakani alifunika udhaifu wa serikali ya awamu ya nne ...shule za kata zilijengwa kila kona...folen zlipungua na alkua anahamia kwenye zahanati ambazo zmewashnda kna pnda. ..kina membe walipofanikiwa kumdanganya JK kuwa lowasa anajipanga kuchukua urais 2010 ndio awamu ya nne ilipoyumba ila rais wetu ni Lowassa watake wasitake...ata kipindi cha mkapa viongozi walikula ela ila wananchi wa kpato cha chini walipata ela ata marekani ela inaliwa ila maskini anapata ahuen kuptia obamacare etc lowasa anapenda ktu kzur ata watu wake wa karbu wa kila maendeleo tutayapata...dspensary zilizowashnda kna pnda ataziinua ndani ya miez sta cz lowasa is a commanding leader na anaskka
 
Kwa jinsi ulivyoijenga hoja ni sawa na mtu kuuchukia ugonjwa iwe ni kumchukia mgonjwa...hii sio kweli..ukiuchukia ugonjwa utatibu na kuzuia sawa na kauli ha EL na umaskini...
 
Back
Top Bottom