Kauli Mbili Muhimu za Mwalimu Nyerere

Kauli Mbili Muhimu za Mwalimu Nyerere

Wanaomsapot lowasa wengi wao wanywa viroba

Ningekuwa mm ccm
Ningetumia 80million kununua viroba nchi nzima
Ili vigawiwe bure kuanzia tarehe 23-26
Hapo najua wanywa viroba wengi ambao n wana ukawa asilimia80
Wangekuwa wapo kwenye usingiz mzto wa viroba
Hivyo kushindwa kumpigia jambaz kura

Hongera sana usiyekunywa VIROBA,ngoja wanywa viroba tuwaonyeshe basi,maana siku hiyo hakutakuwa na KIROBA dukani tuavinunua vyote ili tunywe tarehe 27 October 2015.

Ila kwa ushauri tu,waliomuangusha Mbunge wa CCM Mbeya mwaka 2010,ni hao unaowaita wanywa VIROBA.Ambao ni sisi wapiga kura tuliompigia KURA Mbilinyi badala ya Mwalimu wa sekondari aliyeamua kutuletea vilabu vya pombe badala ya shule.

Kamuulize vizuri nadhano hadi leo anasumbuka na kauli kama yako.

Ila sisi wanyaviroba,ninakuhakikishia ndiyo wapiga kura wengi
 
Umesahau Kiongozi yeyote anayevunja katiba aliyoapa kuilinda HATUFAI hata kidogo.Na Magufuli pamoja na anyemaliza Muda wake ni wavunja katiba na sheria wazuri sana hivyo hawatufai hata kidogo.

Umesahahu viongozi wanaotoa RUSHWA ili wachaguliwe hawatufai,leo 99% ya wagombea UBUNGE kwa ticketi ya CCM hawatoi RUSHWA bali wana mwaga pesa kama hawana akili nzuri ili tu wapate uongozi.

Tumeona jinsi nguvu kubwa ya pesa ikimnadi Magufuli najiuliza kwa ajili ya nini hii rushwa kubwa ya fedha kwa kiasi hiki,basi napata majibu MAGUFULI hatufai hata kwa chembe
 
Kauli za Mwalimu zisitumike kama hirizi.Je tunayaishi aliyoyahubiri Mwalimu?Watanzani wa sasa wanajitambua

Ndugu yangu tunaenzi maneno tu tena wakati wa kusaka kura,maana wanaotutawala hawataki kutoka sababu wameshika vyanzo vyote vikuu vya uchumi,ndiyo maana wanakuwa waoga wakutoka,wanatumia pesa nyingi mradi tu wasitoke.

Wameharibu ELIMU yetu mradi tu wasitoke,wanatumia nguvu kubwa ya jeshi kutisha wapinzani mradi tu wasitoke.Wako busy kupotosha umma mradi tu waitoke kwenye madaraka.
 
Baada ya hizo kauli za Nyerere kukuchanganya naona ndo umejichanganya zaidi, unamtenganisha vipi Magufuli na CCM ? Kutokana na ulivyonukuu kwamba mabadiliko yatatoka nje ya ccm.

Umejitahidi kwa uwezo wako wa kuelewa na ni haki ya kila mmoja kuamini na kufafanua falsafa katika mtizamo wake, Summary ya yote tukutane 25 October 2015, huko hakunaga longolongo wala ushabiki wa JF although kuna wataoshawishiwa kutokana na ujengaji na ushawishi kutoka kwa wanajf.

Pamoja Daima.
 
Salaam ndugu zangu

Hii tabia ya kumnukuu Mwalimu vipisi vipisi inakera sana.

Mwalimu alisema, kuamini na kusimamia mengi sana. Tuache unafiki.

respect !!!
 
Kauli 3 muhimu za mwalimu Nyerere!!

1. CCM si baba yangu wala mama yangu.

2. Watanzania wanataka mabadiliko, wasipoyapata ndani ya CCM watayatafuta nje ya CCM.

3. Msidhani mnaweza kupata ushindi mkipuuza maoni ya wananchi, msikae na kuteua wenyewe mkadhani mnachagua katibu wa chama! mnachagua mtu wa kuongoza Jamhuri ya muungano wa Tanzania.
 
mwadilifu kwanza, mabadiliko bora Dr magufuli pekee atakae weza kuyaleta hakuna mwengine.
 
ni kweli mabadiliko bora hayawezi kuletwa na kiongozi nje ya ccm, ikulu sio pango la walanguzi
 
Marehemu Mwl Julius Kambarage Nyerere wakati wa uhai wake alitoa kauli kubwa mbili
1. "Watanzania wanataka mabadiliko... wasipoyaona.. wasipoyapata ndani ya CCM watayatafuta nje ya CCM".
Kauli hii ni tata kwakua haikuweka wazi ni kwanamna gani watayatafuta mabadiliko hayo nje ya CCM. Lakini pia Mwalimu hakuonesha kama endapo tutayatafuta mabadiliko nje ya CCM tutafanikiwa kuyapata

2. "Rais wa Tanzania atatokea kwenye chama chochote, ila Rais bora wa Tanzania hawezi kutoka nje ya CCM"
Hii kauli iko wazi kabisa kuwa kuna tofauti kubwa kati ya Rais na Rais Bora, kama tutaamua kumchagua Rais nje ya CCM atakuwa tu Rais wetu lakini si Rais bora.

Kauli hizi mbili zikijumlishwa kwa pamoja tunapata majibu makubwa mawili
1. Kumchagua Rais nje ya CCM ni kumchagua Rais asiye bora na asiye na faida kwa maendeleo na mustakabali wa nchi yetu

2. Mabadiliko yatakayopatikana toka kwa kiongozi wa nje ya CCM hayatokuwa mabadiliko bora, au kwa lugha nyingine tunasema kuwa yatakuwa mabadiliko hasi

KUMBE: Kwa mujibu wa kauli hizi za Mwl. Nyerere ni kuwa tunatakiwa kumchagua Rais anayetangaza mabadiliko ndani ya CCM kwakuwa ndiye atakayekuwa Rais bora wa Tanzania na ndiye atakayeleta mabadiliko chanya kwa Watanzania

ASANTE SANA BABA WA TAIFA KWA WOSIA WENYE MANUFAA KWA MAISHA YETU YA SASA NA YA BAADAE

Hayati Baba wa Taifa Mwl. JK Nyerere naye kama binadamu aliongea kwa wakati wake kulingana na muktadha uliokuwepo ndani ya nchi na ccm kwa nyakati zile..
Baada ya Mwalimu kung'atuka na kukaa pembeni alikuwa hafuraishwi na mwenendo ndani ya ccm... Ilikuwa dhahiri kuwa alikuwa mpinzani wa yaliyokuwa yakifanyika ndani ya ccm.

Angekuwa hai mpaka leo (RIP Mwl.) ni wazi kuwa angekuwa UKAWA...

Dhana kuwa rais bora hawezi kutoka ccm ilijengwa kipindi cha Mrema... Mrema amelidhihirishia taifa hili kuwa hakuwa na hajawai kuwa bora...

Lakini pia tumeshuhudia marais kadhaa kutokea ccm baada ya Mwl. JK Nyerere ambao kwa kiwango kikubwa walikuwa wanatimiza tu utaratibu kuwa ni lazima nchi iwe na rais. Walipwaya sana.. Mbona walishindwa kuwa bora pamoja na kuwa wao ni ccm...??

Ni upuuzi kufikiria kuwa mabadiliko wanayohitaji watanzania ni lazima yaletwe na ccm...!!
Kwa taarifa yako...ccm yenyewe inahitaji mabadiliko hivyo hatuwezi kuitegemea ijibadilishe alafu ndo ilete mabadiliko kwene maisha ya watanzania..

Mwl. Nyerere aliona mbali sana.... nyie wengine ni vipofu mnatumia kauli zake tu kwa maslahi yenu binafsi!!
 
"Raisi bora atatoka ndani ya CCM" hii ndio kauli ambayo inaenda kutimia karibuni. Raisi bora ni lazima atoke ndani ya CCM aende upinzani agombee huko na awe raisi. Ndani ya CCM kumejaa mambo mengi machafu na mfumo mbovu. mtu akitaka kuwa raisi atoke ndani ya ccm.Tanzania imekosa raisi bora kwa muda mrefu sasa inaenda kupata raisi bora "aliyetoka ndani ya ccm" na kwenda chadema. Nyerere hakusema Raisi bora lazima awe ndani ya CCM bali atatoka ndani ya CCM

Safi sana..!
 
Kwani huyu rais anaye tuongoza kuwa maskini, wajinga na tufe kwa magonjwa yanayotibika ametokea chama gani eti!! ni CHUMA, CHAUSTA, ACT au ni lichama ambalo halijulikani popote duniani?
 
Mimi nakuona wew ni mtu ni waajabu kutoa nukuu za baba wa taifa leo hii, umesahau kuwa ccm ilokuwepo kipindi nyere yupo hai ni tofauti na ccm ya leo?? Ebu tafakari kwanza mawazo yako kabla hujaandika

Kutafuta mabadiliko nje ya ccm haina maana kuyatafuta kwa ukwawa pekee yasipopatkana ukawa watayatafuta act na kwingineko,,,,ebu tafakari tena

Hata ivo nyerere naye ni binadamu tu km ulivo wewe, waweza ukafafanua sana nukuu zake kutoa maana kulingana na interest zako ila yeye anaweza kuwa hakumaanisha maana yoyote kati ya hizo maana zako
 
Kauli 3 muhimu za mwalimu Nyerere!!

1. CCM si baba yangu wala mama yangu.

2. Watanzania wanataka mabadiliko, wasipoyapata ndani ya CCM watayatafuta nje ya CCM.

3. Msidhani mnaweza kupata ushindi mkipuuza maoni ya wananchi, msikae na kuteua wenyewe mkadhani mnachagua katibu wa chama! mnachagua mtu wa kuongoza Jamhuri ya muungano wa Tanzania.

well said
 
Wanaomsapot lowasa wengi wao wanywa viroba

Ningekuwa mm ccm
Ningetumia 80million kununua viroba nchi nzima
Ili vigawiwe bure kuanzia tarehe 23-26
Hapo najua wanywa viroba wengi ambao n wana ukawa asilimia80
Wangekuwa wapo kwenye usingiz mzto wa viroba
Hivyo kushindwa kumpigia jambaz kura

Umeona ee! wazo nzuri.
 
Back
Top Bottom