Marehemu Mwl Julius Kambarage Nyerere wakati wa uhai wake alitoa kauli kubwa mbili
1. "Watanzania wanataka mabadiliko... wasipoyaona.. wasipoyapata ndani ya CCM watayatafuta nje ya CCM".
Kauli hii ni tata kwakua haikuweka wazi ni kwanamna gani watayatafuta mabadiliko hayo nje ya CCM. Lakini pia Mwalimu hakuonesha kama endapo tutayatafuta mabadiliko nje ya CCM tutafanikiwa kuyapata
2. "Rais wa Tanzania atatokea kwenye chama chochote, ila Rais bora wa Tanzania hawezi kutoka nje ya CCM"
Hii kauli iko wazi kabisa kuwa kuna tofauti kubwa kati ya Rais na Rais Bora, kama tutaamua kumchagua Rais nje ya CCM atakuwa tu Rais wetu lakini si Rais bora.
Kauli hizi mbili zikijumlishwa kwa pamoja tunapata majibu makubwa mawili
1. Kumchagua Rais nje ya CCM ni kumchagua Rais asiye bora na asiye na faida kwa maendeleo na mustakabali wa nchi yetu
2. Mabadiliko yatakayopatikana toka kwa kiongozi wa nje ya CCM hayatokuwa mabadiliko bora, au kwa lugha nyingine tunasema kuwa yatakuwa mabadiliko hasi
KUMBE: Kwa mujibu wa kauli hizi za Mwl. Nyerere ni kuwa tunatakiwa kumchagua Rais anayetangaza mabadiliko ndani ya CCM kwakuwa ndiye atakayekuwa Rais bora wa Tanzania na ndiye atakayeleta mabadiliko chanya kwa Watanzania
ASANTE SANA BABA WA TAIFA KWA WOSIA WENYE MANUFAA KWA MAISHA YETU YA SASA NA YA BAADAE
1. "Watanzania wanataka mabadiliko... wasipoyaona.. wasipoyapata ndani ya CCM watayatafuta nje ya CCM".
Kauli hii ni tata kwakua haikuweka wazi ni kwanamna gani watayatafuta mabadiliko hayo nje ya CCM. Lakini pia Mwalimu hakuonesha kama endapo tutayatafuta mabadiliko nje ya CCM tutafanikiwa kuyapata
2. "Rais wa Tanzania atatokea kwenye chama chochote, ila Rais bora wa Tanzania hawezi kutoka nje ya CCM"
Hii kauli iko wazi kabisa kuwa kuna tofauti kubwa kati ya Rais na Rais Bora, kama tutaamua kumchagua Rais nje ya CCM atakuwa tu Rais wetu lakini si Rais bora.
Kauli hizi mbili zikijumlishwa kwa pamoja tunapata majibu makubwa mawili
1. Kumchagua Rais nje ya CCM ni kumchagua Rais asiye bora na asiye na faida kwa maendeleo na mustakabali wa nchi yetu
2. Mabadiliko yatakayopatikana toka kwa kiongozi wa nje ya CCM hayatokuwa mabadiliko bora, au kwa lugha nyingine tunasema kuwa yatakuwa mabadiliko hasi
KUMBE: Kwa mujibu wa kauli hizi za Mwl. Nyerere ni kuwa tunatakiwa kumchagua Rais anayetangaza mabadiliko ndani ya CCM kwakuwa ndiye atakayekuwa Rais bora wa Tanzania na ndiye atakayeleta mabadiliko chanya kwa Watanzania
ASANTE SANA BABA WA TAIFA KWA WOSIA WENYE MANUFAA KWA MAISHA YETU YA SASA NA YA BAADAE