karv
JF-Expert Member
- Dec 26, 2019
- 1,799
- 3,221
Nawasalimu kwa jina la jamuhuri
Binafsi nimekuwa mfuatiliaji mkubwa sana hasa wa maswala haya yahusuyo ndoa lakini kwa upande wangu nimeona ndoa kwa mujibu wa dini ya kiislamu wapo vizuri sana hasa katika swala zima la:-
1)Ndoa kwa ujumla
2)Talaka
NDOA KWA UJUMLA
-Hapa napenda kuzungumzia swala zima la kuoa mke zaidi ya mmoja ama kwa hakika hii kitu ni nzuri sana. Maana licha ya kwamba tamaa ipo kwa mtu mwenyewe lakini pia kuoa mke zaidi ya mmoja inasaidia kupunguza swala zima la michepuko. Pia ukipata wake wazuri kwa kushirikiana nao kwa pamoja unaweza kufika mbali hasa katika swala zima la maendeleo
Lakini changamoto kubwa iliyopo hapa pindi mume anapofariki watoto kuanza kugombania mali hivyo naamini nyie ni mashuhuda kwa baadhi ya familia.
TALAKA
Sasa hapa kwenye talaka ndio wamepatia kabisa yani haiwezekani mke wangu nimfumanie ugoni halafu niambiwe kitatutenganisha kifo huo ni uongo. Haiwezekani mke awe na tabia zisizofaa ikiwemo kudharau ndugu zangu halafu niendelee kumkumbatia kisa kifo ndio kitatutenganisha. Kama mke kakosea umemuadhibu mara mbili ya tatu bado anafanya kosa lile lile talaka ndio halali yake.
Hii sheria ya kwamba kifo kitutenganishe imewaponza watu wengi sana hadi kupelekea wengine kuona ndoa zao ni chungu na kukimbilia kutafuta tulizo nje kisiri (mchepuko) maana wanaona maovu ya wenza wao lakini wanashindwa kuwapa talaka kwa kisingizio cha hadi kifo kitutenganishe.
Kama wewe si muislamu basi funga ndoa hata ya kiserikali lakini uweke kipengele cha kuongeza mke mwingine hapo hatokuwa na jeuri ya kuringa maana kwenye ndoa ya kiserikali hata talaka zipo. Kwa kumalizia kwenye swala la kuoa mke zaidi ya mmoja waislamu mmeupiga mwingi sana
Kumbuka kuoa sio lazima pia ndoa ndoano
Naomba kuwasilisha
Binafsi nimekuwa mfuatiliaji mkubwa sana hasa wa maswala haya yahusuyo ndoa lakini kwa upande wangu nimeona ndoa kwa mujibu wa dini ya kiislamu wapo vizuri sana hasa katika swala zima la:-
1)Ndoa kwa ujumla
2)Talaka
NDOA KWA UJUMLA
-Hapa napenda kuzungumzia swala zima la kuoa mke zaidi ya mmoja ama kwa hakika hii kitu ni nzuri sana. Maana licha ya kwamba tamaa ipo kwa mtu mwenyewe lakini pia kuoa mke zaidi ya mmoja inasaidia kupunguza swala zima la michepuko. Pia ukipata wake wazuri kwa kushirikiana nao kwa pamoja unaweza kufika mbali hasa katika swala zima la maendeleo
Lakini changamoto kubwa iliyopo hapa pindi mume anapofariki watoto kuanza kugombania mali hivyo naamini nyie ni mashuhuda kwa baadhi ya familia.
TALAKA
Sasa hapa kwenye talaka ndio wamepatia kabisa yani haiwezekani mke wangu nimfumanie ugoni halafu niambiwe kitatutenganisha kifo huo ni uongo. Haiwezekani mke awe na tabia zisizofaa ikiwemo kudharau ndugu zangu halafu niendelee kumkumbatia kisa kifo ndio kitatutenganisha. Kama mke kakosea umemuadhibu mara mbili ya tatu bado anafanya kosa lile lile talaka ndio halali yake.
Hii sheria ya kwamba kifo kitutenganishe imewaponza watu wengi sana hadi kupelekea wengine kuona ndoa zao ni chungu na kukimbilia kutafuta tulizo nje kisiri (mchepuko) maana wanaona maovu ya wenza wao lakini wanashindwa kuwapa talaka kwa kisingizio cha hadi kifo kitutenganishe.
Kama wewe si muislamu basi funga ndoa hata ya kiserikali lakini uweke kipengele cha kuongeza mke mwingine hapo hatokuwa na jeuri ya kuringa maana kwenye ndoa ya kiserikali hata talaka zipo. Kwa kumalizia kwenye swala la kuoa mke zaidi ya mmoja waislamu mmeupiga mwingi sana
Kumbuka kuoa sio lazima pia ndoa ndoano
Naomba kuwasilisha