komasalonde
JF-Expert Member
- Sep 9, 2024
- 2,743
- 3,516
Baada ya Rais Idd Amin wa Uganda kuiteka ndege iliyokuwa imewabeba waisraeli na kuilazimisha kutua katika uwanja wa Entebe, kuna uokoaji uliandaliwa na askari wa kikosi kazi huko Israel.
Haya yamo kwenye kile kitabu kiitwacho " ninety minutes at Entebe.
Moja ya simulizi ya kuvutia ni sehemu inayosema wakati ndege ya kijeshi ya uokoaji inatua uwanja wa Entebe, waziri mkuu wa Israel wa wakati huo alimpigia simu Idd Amin akijinyenyekeza kumuomba awaachie mateka wale kumbe makomandoo saa hiyo wako tayari Entebe kwa kazi maalum.
Sehemu nyingine ya kitabu, inasema ndege ya uokoaji ilitambaa kimo cha maji ya ziwa Victoria ili isionekane na rada ( za wakati huo).
Tukio lingine kitabu kinasema, liliandaliwa gari la Rais wa Uganda, kwa rangi Ile ile na kila kitu mpaka plate no, na wakaingia nayo na askari wakadhani ni Rais ameingia kumbe makomandoo wa Israel.
Katika mpambano huo walimpoteza askari mmoja tu aliyechelewa nje ya ndege na maiti yake iliingizwa ndani ya ndege wakaondoka naye, ila wakamuuwa aliyempiga risasi.
Yako mengi. Waliokisoma wengine watajazia...
Haya yamo kwenye kile kitabu kiitwacho " ninety minutes at Entebe.
Moja ya simulizi ya kuvutia ni sehemu inayosema wakati ndege ya kijeshi ya uokoaji inatua uwanja wa Entebe, waziri mkuu wa Israel wa wakati huo alimpigia simu Idd Amin akijinyenyekeza kumuomba awaachie mateka wale kumbe makomandoo saa hiyo wako tayari Entebe kwa kazi maalum.
Sehemu nyingine ya kitabu, inasema ndege ya uokoaji ilitambaa kimo cha maji ya ziwa Victoria ili isionekane na rada ( za wakati huo).
Tukio lingine kitabu kinasema, liliandaliwa gari la Rais wa Uganda, kwa rangi Ile ile na kila kitu mpaka plate no, na wakaingia nayo na askari wakadhani ni Rais ameingia kumbe makomandoo wa Israel.
Katika mpambano huo walimpoteza askari mmoja tu aliyechelewa nje ya ndege na maiti yake iliingizwa ndani ya ndege wakaondoka naye, ila wakamuuwa aliyempiga risasi.
Yako mengi. Waliokisoma wengine watajazia...