Katika hili, Rais Magufuli ni moja ya “Smartest people” Tanzania

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,172
7,428
1571921325037.png
Kwanza, Watanzania tunajuana vile tulivyo na tayari tuna uhakika kwamba hivi tulivyo ndivyo tulivyo. Kama tutabadilika baadae; hilo linawezekana lakini ni suala linalohitaji mjadala wa peke yake.

Jambo la pili ambalo ni “Mujarab” ni kwamba; miongoni mwa watanzania ambao ni “Smartest” ni Rais wetu Mh. Magufuli. Katika muktadha wa mada hii, hoja hii inajengwa kwa sababu moja kubwa. Mheshimiwa ni moja ya watanzania wachache sana ambao wana uthubutu wa kusimamia kile wanachoamini kwa gharama yoyote ile. Yaani yeye anachoamini kuwa ni sahihi; atakisimamia kwa uwezo wake wote. Hii ni sifa kuu ya kwanza kabisa ya mtu “Smart”

Miongoni mwetu, kuna watu wanaoamini au wanaodai kuwa ni “Smart” na wengine wanadai ni wasomi lakini ni vigumu kufahamu wanaamini nini au hawaamini nini na wanasimamia nini hasa. Wao hawa, hata kutoa mawazo yao (wanayoamini ndio sahihi) hadharani wanaogopa; achilia mbali kuyasimamia au kuyatekeleza, na wale wanaotoa wengi wao mawazo watakayotoa leo na watakayotoa kesho kwenye jambo lile lile yanakinzana.

Sasa unajiuliza, hivi ni mtu gani ambaye ni “smart” au anayedai kuwa msomi lakini anashindwa tu kuelewa concept rahisi kwamba mawazo ambayo yako ndani ya kichwa cha mtu lakini hayajatolewa na kuwa “Shared” kwa jamii na wala hayafanyiwi kazi na mtu yoyote akiwemo aliyenayo; mawazo hayo hayana maana yoyote?

Kuna hoja kuwa, hata watu wakitoa mawazo waliyo nayo hayafanyiwi kazi. Sasa swali la kujiuliza, kama kweli wewe ni “Smart” kwa nini wewe usitoe hayo mawazo yako halafu ukaanza kuyafanyia kazi katika level yako kulingana na kile kilichopo ndani ya uwezo wako ili angalau kuonesha mfano?

Halafu pia tunafikiri tuko “Smart” lakini tunashindwa kuelewa jambo moja muhimu na rahisi sana kueleweka kuwa,ili kufanikiwa; haihitajiki mawazo yako yote ya kubalike. Inahitajika wazo lako moja tu likubalike hata kama umetoa mawazo 10,000.

Ikumbukwe kuwa hata kama unaomba kazi kwa mfano, huhitaji kupata kila kazi unayoomba, unahitaji kupata kazi moja tu kati ya mamia ya kazi unazoomba. Utakuwa mtu wa ajabu kama utaomba kazi 400 halafu unataka upate zote muda huo huo unadai wewe ni “Smart” halafu usipopata unaacha.

Unatoa ushauri mara tatu, halafu ushauri wako wenyewe umechanganya na matusi humo humo, ushauri unaoutoa wewe mwenyewe ungeweza kuanza kuufanyia kazi katika level yako lakini hujafanya kitu, halafu unaancha unadai sasa husikilizwi utafanyaje? Hivi kama tunakata tama kirahisi hivyo, ikitokea siku ukipewa majukumu yeye controversies kibao unafanya nini?

Tunasahau kuwa hata wanasayanisi waliofanya uvumbuzi wa aina mbali mbali, walifanya majaribio yaliyofeli mara maelfu lakini walihitaji jaribio moja tu lilikubali na kuibadili dunia na wamefanikiwa mara nyingi?. Kwa hiyo kama wewe kwa mfano una wazo ambalo unadhani ni zuri, halafu kwa kuwa ulishalifanyia kazi mara moja ukashindwa kasha ukaacha, au ulishatoa ushauri mara moja ukakataliwa ukakata tamaa nab ado unajiaminisha kuwa wewe ni mtu “smart” Ujue unajidanganya. Sifa ya kwanza ya mtu yoyote smart ni kusimamia anachoamini katika shida na raha.

Ni kweli tuna changamoto nyingi ila ili tutoke tulipo na kupiga hatua, ni lazima tutambue hasa mzizi wa tatizo ni nini na kushughulika na mzizi, kuja na majibu marahisi rahisi hakuwezi kuwa na faida ya maana.

Ikumbukwe, wewe ukidhani uko “Smart” au ni “msomi” lakini hutekelezi wala kusimamia mawazo yako; wale ambao unawaona sio smart watasimamia na kutekeleza mawazo yao, na kwa msingi huo, wao ndio smart hata kama wewe unawaona kinyume chake.

Kama una mawazo ambayo unaamini ni mazuri lakini huna ujasiri wa kuyatoa hadharani, wenye mawazo ambayo wewe unadhani ni mabaya watayatoa na yatafanyiwa kazi, na kwa kuwa hamna mbadala; hayo yatakuwa ndio mawazo bora zaidi katika eneo na muktadha huo.

Jambo hili la kusimamia kile mtu anachoamini kwa uwezo wake wote ni jambo muhimu. Kwa hiyo ni vyema tukajifunza jambo hili jema kutoka kwa Mheshimiwa.Hata hivyo, ni muhimu Zaidi kuendelea kujifunza ili kujiridhisha kama yale tunayoamini ni sahihi maana wakati mwingine pia unaweza kuamini jambo na baadae ukagundua ulichoamini hakikuwa sahihi.
 
Pia, kuna dhana ambayo pengine inahitaji utafiti Zaidi, kwamba moja ya vitu vinavyoathiri mfumo wetu wa kufikiri; ni aina ya meditation ambayo wengi wetu hufanya. Wakati wengine wakifanya meditation kama vile Yoga, sisi tuna meditate na puli. Mwisho wa wa siku, hiyo inaathiri mfumo wetu mzima juu ya vile tunavyoitizama dunia na changamoto zinazojitokeza.
 
nilitegemea kuona ilo wazo ila nimetoka kapa

ko kwako mtu smart ni yule anayesimamia jambo analo amini haijarishi liko sawa ama hapana,yule anayekomaa na aaminilo hata kama lina mapungufu/madhara kwa watu.

unamtaka mtu kufanyia kazi ushauri angalau kwa level yake hapa umeonesha hujui usemalo mf. mtu atoe ushauri naona ya kuongeza/kudhibiti mapato bandarini katika level yake ataanza ufanyia kazi kwenye bandari ya kwake ama.
 
ko kwako mtu smart ni yule anayesimamia jambo analo amini haijarishi liko sawa ama hapana,yule anayekomaa na aaminilo hata kama lina mapungufu/madhara kwa watu
Hili unalouliza limeelezwa vizuri kwenye mada ya msingi. Mtu hawezi kuleta impact yoyote kama hatekelezoi anachoamini na kama mtu hana impact hawezi kudai yeye ni smart kwa namna yoyote ile. Kama hoja hii si sahihi unaweza kuiweka sawa.

Kuhusu hoja ya usahihi au kutokuwa sahihi kwa kile mtu anachoamini au kufikiria, huu ni mjadala mpana sana na wa peke yake, lakini kwa kuanzia ndio maana hapo juu kwenye mada ya msingi, inasisitizwa kwamba ni muhimu tukajitahidi kujifunza zaidi na kupata taarifa zaidi kwa sababu mtu unaweza kuamini kitu kwa wakati fulani lakini baadae ukabaini haukuwa sahihi, ama kwa kutokuwa na taarifa sahihi, kutokuwa na taarifa za kutosha juu ya jambo fulani au mazingira. Hata hivyo haina maana kwamba wakati unaendelea kutafuta taarifa Zaidi au kujifunza Zaidi ili kuchuja unachoamini, usifanye kitu hadi utakapomaliza, kwa sababu zoezi hilo halina mwisho hadi unakufa.

Ndio maana hata watu waliokuwa na uwezo mkubwa wa kifikra kama kina Albert Einstain walikufa bado wanatafuta ukweli na usahihi wa mambo mbalimbali.
 
unamtaka mtu kufanyia kazi ushauri angalau kwa level yake hapa umeonesha hujui usemalo mf. mtu atoe ushauri naona ya kuongeza/kudhibiti mapato bandarini katika level yake ataanza ufanyia kazi kwenye bandari ya kwake ama.
Mfano ulioutoa, mtoa ushauri hawezi kutekeleza. Hata hivyo haina maana kwamba kwa kuwa kwa mfano wako hauwezi kutekeleza, basi kila jambo halitekelezeki. Kudai kwamba wewe au mimi hatuna wajibu wa kutekeleza bali watu wengine tu ndio wenye wajibu juu yetu, hilo ni moja ya tatizo kubwa la kifikra ambalo linatusumbua watanzania wengi na linatuadhiri vibaya.

Moja ya athari ya tatizo hilo, unaweza ukaliona hata kwenye urafiki wetu. Unakuwa na Rafiki anataka umkopeshe, ukimkopesha halipi, usipomkopesha anaona humtendei haki.
Unatakiwa uelewe una wajibu kama wengine walivyo na wajibu.
 
Eti mpaka waende kuyatolea Ikulu!
Kwa mfano tuchukulie hili jukwaa lingekuwa ni bunge, wachangiaji hapa ni ndio wabunge, hebu jaribu kupima uzito wa kile tunachochangia na kwamba kinasaidia kutatua tatizo gani? na kama mawazo yetu si bora hao wenye mawazo bora wako wapi? na kama hayo mawazo yapo kwenye kichwa cha muhusika ni kwa faida ya nani? au ni nani kakatazwa kutoa maoni yake hapa?
 
Hata hivyo, ni muhimu zaidi kuendelea kujifunza ili kujiridhisha kama yale tunayoamini ni sahihi maana wakati mwingine pia unaweza kuamini jambo na baadae ukagundua ulichoamini hakikuwa sahihi, kutokana na kuwa na taarifa zisizo sahihi, kutokuwa na taarifa za kutosha juu ya unachoamini, au Imani iliyosababishwa na mazingira uliyokulia

Lakini pia njia bora Zaidi ya kujifunza ni ku share unachoamini ni sahihi ili kama sio sahihi watu wengine watakuambia lakini pia kutekeleza ili ukikosea utajifunza namna ya kujisahihisha lakini kuamua kutoamua, au kulalamikia wengine tu ni tatizo kubwa.
 
Kama hivyo ndivyo, basi Amber Rutty na James Delicious watakua ma"jinias"!
Tanzania ya vi-"wonder"!
Kama wewe una dai kuwa mtu mwema lakini huna unachofanya, unaamka asubuhi unakuja jf unalaumuuuu jioni unalala hivyo hivyo, yule anayeamini juu ya mambo kadhaa bila kujali ubora wake lakini akayatekeleza na kuyasimamia kwa nguvu zake zote, yuko sahihi kukuzidi.

Kumbuka hao unaowasema wao wanasababisha wanayoamini ni sawa na muhimu, wewe kazi yako kuwafuatilia wanavyosababisha na kulalamika huku ukidai hakuna unaloweza kufanya.
 
Kwa mfano tuchukulie hili jukwaa lingekuwa ni bunge, wachangiaji hapa ni ndio wabunge, hebu jaribu kupima uzito wa kile tunachochangia na kwamba kinasaidia kutatua tatizo gani? na kama mawazo yetu si bora hao wenye mawazo bora wako wapi? na kama hayo mawazo yapo kwenye kichwa cha muhusika ni kwa faida ya nani? au ni nani kakatazwa kutoa maoni yake hapa?
Wenye mawazo bora awapewi nafasi katika jamii,ungeweka contact zako teuzi zisikupite
 
Mbona Unatoa mada unaendelea kuchangia wewe Mwenyewe.. Ebu pozi kidogo tusome na mawazo ya wengine...over..
Usisome tu, nawe pia changia mawazo yako ili wengine wasome. Au wewe unataka tu kunufaika toka kwa wenzako lakini hutaki wengine wanufaike toka kwako? bu the way, kwa mimi kuchangia, kunakuzuiaje wewe au mtu mwingine kuchangia?au wewe huchangii ila pia usingependa kuniona mimi nachangia licha ya kwamba kwa kufanya hivyo wewe hupungukiwi na kitu?
 
Natoa wazo kila ajengae nyumba ajenge na mitaro mifereji ya kutolea maji eneo lake ili jirani yake nae afanye hivohivo itasaidia mitaa kuwa na mitaro ya kutiririsha maji yasituhame mabarabarani na kujaza madimbwi yazalizayo mbu,kuliko kusubiria mabeberu watuchimbie mitaro.Wazo hizo je mmi ni smart
 
Wenye mawazo bora awapewi nafasi katika jamii,ungeweka contact zako teuzi zisikupite
Nishatoa contact zangu tayari.

kwa mfano kwenye hili jukwaa nani kanyimwa nafasi ? au hatutaki kutumia tulicho nacho tunataka tusichokuwa nacho?
 
Kwanza, Watanzania tunajuana vile tulivyo na tayari tuna uhakika kwamba hivi tulivyo ndivyo tulivyo. Kama tutabadilika baadae; hilo linawezekana lakini ni suala linalohitaji mjadala wa peke yake.

Jambo la pili ambalo ni “Mujarab” ni kwamba; miongoni mwa watanzania ambao ni “Smartest” ni Rais wetu Mh. Magufuli. Katika muktadha wa mada hii, hoja hii inajengwa kwa sababu moja kubwa. Mheshimiwa ni moja ya watanzania wachache sana ambao wana uthubutu wa kusimamia kile wanachoamini kwa gharama yoyote ile. Yaani yeye anachoamini kuwa ni sahihi; atakisimamia kwa uwezo wake wote. Hii ni sifa kuu ya kwanza kabisa ya mtu “Smart”

Miongoni mwetu, kuna watu wanaoamini au wanaodai kuwa ni “Smart” na wengine wanadai ni wasomi lakini ni vigumu kufahamu wanaamini nini au hawaamini nini na wanasimamia nini hasa. Wao hawa, hata kutoa mawazo yao (wanayoamini ndio sahihi) hadharani wanaogopa; achilia mbali kuyasimamia au kuyatekeleza, na wale wanaotoa wengi wao mawazo watakayotoa leo na watakayotoa kesho kwenye jambo lile lile yanakinzana.

Sasa unajiuliza, hivi ni mtu gani ambaye ni “smart” au anayedai kuwa msomi lakini anashindwa tu kuelewa concept rahisi kwamba mawazo ambayo yako ndani ya kichwa cha mtu lakini hayajatolewa na kuwa “Shared” kwa jamii na wala hayafanyiwi kazi na mtu yoyote akiwemo aliyenayo; mawazo hayo hayana maana yoyote?

Kuna hoja kuwa, hata watu wakitoa mawazo waliyo nayo hayafanyiwi kazi. Sasa swali la kujiuliza, kama kweli wewe ni “Smart” kwa nini wewe usitoe hayo mawazo yako halafu ukaanza kuyafanyia kazi katika level yako kulingana na kile kilichopo ndani ya uwezo wako ili angalau kuonesha mfano?

Halafu pia tunafikiri tuko “Smart” lakini tunashindwa kuelewa jambo moja muhimu na rahisi sana kueleweka kuwa,ili kufanikiwa; haihitajiki mawazo yako yote ya kubalike. Inahitajika wazo lako moja tu likubalike hata kama umetoa mawazo 10,000.

Ikumbukwe kuwa hata kama unaomba kazi kwa mfano, huhitaji kupata kila kazi unayoomba, unahitaji kupata kazi moja tu kati ya mamia ya kazi unazoomba. Utakuwa mtu wa ajabu kama utaomba kazi 400 halafu unataka upate zote muda huo huo unadai wewe ni “Smart” halafu usipopata unaacha.

Unatoa ushauri mara tatu, halafu ushauri wako wenyewe umechanganya na matusi humo humo, ushauri unaoutoa wewe mwenyewe ungeweza kuanza kuufanyia kazi katika level yako lakini hujafanya kitu, halafu unaancha unadai sasa husikilizwi utafanyaje? Hivi kama tunakata tama kirahisi hivyo, ikitokea siku ukipewa majukumu yeye controversies kibao unafanya nini?

Tunasahau kuwa hata wanasayanisi waliofanya uvumbuzi wa aina mbali mbali, walifanya majaribio yaliyofeli mara maelfu lakini walihitaji jaribio moja tu lilikubali na kuibadili dunia na wamefanikiwa mara nyingi?. Kwa hiyo kama wewe kwa mfano una wazo ambalo unadhani ni zuri, halafu kwa kuwa ulishalifanyia kazi mara moja ukashindwa kasha ukaacha, au ulishatoa ushauri mara moja ukakataliwa ukakata tamaa nab ado unajiaminisha kuwa wewe ni mtu “smart” Ujue unajidanganya. Sifa ya kwanza ya mtu yoyote smart ni kusimamia anachoamini katika shida na raha.

Ni kweli tuna changamoto nyingi ila ili tutoke tulipo na kupiga hatua, ni lazima tutambue hasa mzizi wa tatizo ni nini na kushughulika na mzizi, kuja na majibu marahisi rahisi hakuwezi kuwa na faida ya maana.

Ikumbukwe, wewe ukidhani uko “Smart” au ni “msomi” lakini hutekelezi wala kusimamia mawazo yako; wale ambao unawaona sio smart watasimamia na kutekeleza mawazo yao, na kwa msingi huo, wao ndio smart hata kama wewe unawaona kinyume chake.

Kama una mawazo ambayo unaamini ni mazuri lakini huna ujasiri wa kuyatoa hadharani, wenye mawazo ambayo wewe unadhani ni mabaya watayatoa na yatafanyiwa kazi, na kwa kuwa hamna mbadala; hayo yatakuwa ndio mawazo bora zaidi katika eneo na muktadha huo.

Jambo hili la kusimamia kile mtu anachoamini kwa uwezo wake wote ni jambo muhimu. Kwa hiyo ni vyema tukajifunza jambo hili jema kutoka kwa Mheshimiwa.Hata hivyo, ni muhimu Zaidi kuendelea kujifunza ili kujiridhisha kama yale tunayoamini ni sahihi maana wakati mwingine pia unaweza kuamini jambo na baadae ukagundua ulichoamini hakikuwa sahihi.
No points,full of confusión (Rubbish
 
Hata hivyo, ni muhimu zaidi kuendelea kujifunza ili kujiridhisha kama yale tunayoamini ni sahihi maana wakati mwingine pia unaweza kuamini jambo na baadae ukagundua ulichoamini hakikuwa sahihi, kutokana na kuwa na taarifa zisizo sahihi, kutokuwa na taarifa za kutosha juu ya unachoamini, au Imani iliyosababishwa na mazingira uliyokulia

Lakini pia njia bora Zaidi ya kujifunza ni ku share unachoamini ni sahihi ili kama sio sahihi watu wengine watakuambia lakini pia kutekeleza ili ukikosea utajifunza namna ya kujisahihisha lakini kuamua kutoamua, au kulalamikia wengine tu ni tatizo kubwa.
Senseless song
 
Nazungumzia nafasi kwa watunga Sera huwa hakuna ushirikishwaji wa watumiaji sera
Kwani ni kila kitu ni cha kisera? by the way sasa nikusaidie kitu kidogo.

Moja ya mambo yanayosaidia katika utungaji sera au ubadilishaji wa sera katika nchi mbali mbali ni maoni ya umma. "Public Choices". Kwa hiyo inapotokea wazo likawa linatolewa mara nyingi na watu wengi na likawa kwenye mfumo mzuri ambao unaweza kutekelezeka na kuleta faida linaweza kuchukuliwa. Sasa jiulize! kama hao wanaodai wana mawazo mazuri hawana hata courage ya kuyatoa? hapo vipi?
 
Back
Top Bottom