Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,662
- 218,149
Huyu kiongozi alikamatwa tangu jana pale alipofika kituo cha Polisi ili kuripoti makosa ya mtandaoni baada ya Tweet ya Dadi Igogo , badala yake akakamatwa yeye ambaye ni mlalamikaji na kuswekwa selo na kunyimwa dhamana .
Masonga amewahi kufungwa jela kwa kesi ya uongo iliyotungwa kwa uratibu wa Aliyekuwa RC wa Mbeya , Amos Makalla na RPC Mpinga ambayo pia ilimhusisha Joseph Mbilinyi , hawa wote walifungwa jela , lakini walitolewa jela katika mazingira ya kutatanisha na baadaye walishinda rufaa yao .
Niliweka uzi hapa kuhusu jambo hili lakini ulifutwa na Moderator mnoko bila sababu.