mchangamadini
Member
- Jun 1, 2017
- 59
- 28
Katibu wa CCM mkoa wa Singida, Jimson Mhagama na katibu wa CCM wilaya ya Singida Vijijini, Grace wanalalamikiwa na wananchi na wanachama wa chama hicho kufisadi fedha za chama zilizotolewa na CCM makao makuu kufanikisha shughuli mbalimbali za ujenzi wa chama mkoani na wilayani humo pamoja na kufanikisha uchaguzi mdogo wa ubunge jimbo la Singida Kaskazini.
Katibu wa wilaya Grace shindika na katibu wake msaidizi binti Selemani waliamua kufoji saini za viongozi wa Kata,matawi na mashina ili kuhalalisha wizi wao huo.
Sisi wanachama wa CCM mkoa wa singida tumelisemea hili kwenye vikao halali lakini makatibu hawa wanatufokea na kusema kuwa wao hawadaiwi na hakuna wa kuwafanyia lolote kwani wamekishika chama taifa hivyo hawayumbishwi na mtu.
Katibu wa wilaya sasa hivi ameikimbia ofisi yake badala yake amehamia ofisi za wilaya zingine zilizopo jengo la CCM mkoa.
Tunaomba chama taifa tusikie kilio chetu, Grace na Mhagama wanatunyanyasa na wanakiua chama mkoani Singida.
Katibu wa wilaya Grace shindika na katibu wake msaidizi binti Selemani waliamua kufoji saini za viongozi wa Kata,matawi na mashina ili kuhalalisha wizi wao huo.
Sisi wanachama wa CCM mkoa wa singida tumelisemea hili kwenye vikao halali lakini makatibu hawa wanatufokea na kusema kuwa wao hawadaiwi na hakuna wa kuwafanyia lolote kwani wamekishika chama taifa hivyo hawayumbishwi na mtu.
Katibu wa wilaya sasa hivi ameikimbia ofisi yake badala yake amehamia ofisi za wilaya zingine zilizopo jengo la CCM mkoa.
Tunaomba chama taifa tusikie kilio chetu, Grace na Mhagama wanatunyanyasa na wanakiua chama mkoani Singida.