Emma.
JF-Expert Member
- Jun 25, 2012
- 19,935
- 5,558
Wana JF,
Katibu Mkuu wa Chama wa Wananchi (CUF) Maalim Seif ameshatua Zanzibar tayari kwa ajili ya Kikao cha Baraza Kuu la CUF kinachofanyika leo huko Zanzibar kumjadili aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama hicho Profesa Lipumba.
Kikao hicho kimeitishwa kwa dharura kumjadili [HASHTAG]#Lipumba[/HASHTAG] baada ya [HASHTAG]#Lipumba[/HASHTAG] akishirikiana na wafuasi pamoja na Jeshi la Polisi kuvamia Ofisi za Makao Mkuu ya CUF Buguruni jijini Dar es salaam kwa kile wanachodai wamepokea barua ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini Jaji Francis Mutungi ikimtambua Lipumba kama Mwenyekiti halali wa CUF baada ya kujiuzulu uenyekiti wa CUF mwenyewe Agosti 6 mwaka jana akipinga uamuzi wa UMOJA wa [HASHTAG]#UKAWA[/HASHTAG] kumsimamisha Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa kugombea urais.
Prof.Lipumba kung'oka leo?
#My take: Baada ya kutolewa taarifa kutoka kwa Msajili wa Vyama vya Siasa Jaji Francis Mutungi kumtambua Prof. Lipumba kama Mwenyekiti halali wa CUF kumetokea sintofahamu kubwa sana kuhusu jambo hilo.
Nilisoma kazi na majukumu ya Msajili vya Vyama lakini sijaona kifungu ambacho kinampa mamlaka Msajili wa Vyama kupingana na Maamuzi ya Vikao Vya Kamati Kuu au Baraza Kuu ya Vyama vya Siasa nchini kama alivyofanya kwa CUF, kwa kutoa barua ya kumtambua Lipumba kama Mwenyekiti halali wa CUF wakati alishajiuzulu mwenyewe.
Baada ya hapo Baraza Kuu lilipokutana kwenye Mkutano wake wa ndani kujaza nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya CUF ndipo Lipumba alivamia Mkutano huo na kuandaa vijana kufanya vurugu na kuvunja Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu uliokuwa unafanyika ambapo ilimpelekea kuchukuliwa hatua za kufukuzwa uanachama.
Nawatakia kila la heri CUF kwenye Mkuu wa Baraza Kuu unafanyika leo naamini watatoa maamuzi sahihi kwa maslahi mapana ya nchi. Migogoro ndani ya chama huleta mgawanyiko mkubwa sana kwa wafuasi wao. Naamini [HASHTAG]#Lipumba[/HASHTAG] ataheshimu maamuzi ambayo yatatolewa baada ya Mkutano huo.
Katibu Mkuu wa Chama wa Wananchi (CUF) Maalim Seif ameshatua Zanzibar tayari kwa ajili ya Kikao cha Baraza Kuu la CUF kinachofanyika leo huko Zanzibar kumjadili aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama hicho Profesa Lipumba.
Kikao hicho kimeitishwa kwa dharura kumjadili [HASHTAG]#Lipumba[/HASHTAG] baada ya [HASHTAG]#Lipumba[/HASHTAG] akishirikiana na wafuasi pamoja na Jeshi la Polisi kuvamia Ofisi za Makao Mkuu ya CUF Buguruni jijini Dar es salaam kwa kile wanachodai wamepokea barua ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini Jaji Francis Mutungi ikimtambua Lipumba kama Mwenyekiti halali wa CUF baada ya kujiuzulu uenyekiti wa CUF mwenyewe Agosti 6 mwaka jana akipinga uamuzi wa UMOJA wa [HASHTAG]#UKAWA[/HASHTAG] kumsimamisha Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa kugombea urais.
Prof.Lipumba kung'oka leo?
#My take: Baada ya kutolewa taarifa kutoka kwa Msajili wa Vyama vya Siasa Jaji Francis Mutungi kumtambua Prof. Lipumba kama Mwenyekiti halali wa CUF kumetokea sintofahamu kubwa sana kuhusu jambo hilo.
Nilisoma kazi na majukumu ya Msajili vya Vyama lakini sijaona kifungu ambacho kinampa mamlaka Msajili wa Vyama kupingana na Maamuzi ya Vikao Vya Kamati Kuu au Baraza Kuu ya Vyama vya Siasa nchini kama alivyofanya kwa CUF, kwa kutoa barua ya kumtambua Lipumba kama Mwenyekiti halali wa CUF wakati alishajiuzulu mwenyewe.
Baada ya hapo Baraza Kuu lilipokutana kwenye Mkutano wake wa ndani kujaza nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya CUF ndipo Lipumba alivamia Mkutano huo na kuandaa vijana kufanya vurugu na kuvunja Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu uliokuwa unafanyika ambapo ilimpelekea kuchukuliwa hatua za kufukuzwa uanachama.
Nawatakia kila la heri CUF kwenye Mkuu wa Baraza Kuu unafanyika leo naamini watatoa maamuzi sahihi kwa maslahi mapana ya nchi. Migogoro ndani ya chama huleta mgawanyiko mkubwa sana kwa wafuasi wao. Naamini [HASHTAG]#Lipumba[/HASHTAG] ataheshimu maamuzi ambayo yatatolewa baada ya Mkutano huo.