Katibu Mkuu wa CCM uko wapi? Kuna tatizo chamani!

Katibu Mkuu wa CCM uko wapi? Kuna tatizo chamani!

Wahamiaji kutoka CHADEMA na CUF (Mollel na Mtulia) walipitishwa bila kura za maoni ndani ya CCM kugombea Siha na Kinondoni. Tukavumilia. Tukasonga mbele. Tena, kuna mpango wenye viwango wa kuwapitisha Wahamiaji wengine Mwita Waitara na Kalanga kugombea Ukonga na Monduli bila kura za maoni. Utekelezaji wa mpango umeshaanza.

Waungamkono wa mpango huo wanajificha kwenye Kanuni za Kiuchaguzi za CCM. Eti, Kamati Kuu yaweza kuondoa utaratibu wa kura za maoni. Sasa, lini na wapi Kamati Kuu ya CCM iliketi, iliamua na kuelekeza kuwa Ukonga na Monduli kusiwe na kura za maoni? Halafu, Katibu Mkuu wa CCM na viongozi wengine mpo kimya tu. Kwanini?

Kura za maoni ni mchakato muhimu. Ni mchakato wa kichama na kisiasa. Lazima mgombea apimwe kukubalika kwake kuanzia kwa wanachama wa CCM wa Jimbo lake/Wilaya yake. Halafu, Kamati Kuu huidhinisha. Kura za maoni huonesha picha halisi ya mgombea mtarajiwa wa CCM katika Jimbo husika.

Ukimya huu wa viongozi wetu, huku kukiwa na malalamiko ya makada wetu wa CCM wa Monduli na Ukonga unatokana na kuwa na uhakika wa 'kushinda' chaguzi hizi za marudio? Katibu Mkuu wa CCM, Ndugu yangu Dr. Bashiru Ally uko wapi? Kuna tatizo chamani!

Majibu ya Jeshi la Polisi kwa Waziri Lugola yamemuimarisha na kumjenga sana!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
CCM ni mali ya mtu mmoja tu .
 
Ndo maana mikosi imewaandama Maishani mwenu halafu mnatafuta mchawi kumbe ninyi wenyewe, sasa wewe kubwa zima kudanganya na kujifanya CCM wakati ni Mtumwa wa Mbowe kwa nini usilaanike? Mungu hapendi uongo tubu jisafishe kuwa mkweli maishani ili upate baraka, watu kama ninyi ndo mnaoifanya chadema ilaaniwe kwa kuwa Muongo na mnafiki!
Na huyu kada wenu naye mnataka kumuonyesha bunduki kama Nape ?
 
Wahamiaji kutoka CHADEMA na CUF (Mollel na Mtulia) walipitishwa bila kura za maoni ndani ya CCM kugombea Siha na Kinondoni. Tukavumilia. Tukasonga mbele. Tena, kuna mpango wenye viwango wa kuwapitisha Wahamiaji wengine Mwita Waitara na Kalanga kugombea Ukonga na Monduli bila kura za maoni. Utekelezaji wa mpango umeshaanza.

Waungamkono wa mpango huo wanajificha kwenye Kanuni za Kiuchaguzi za CCM. Eti, Kamati Kuu yaweza kuondoa utaratibu wa kura za maoni. Sasa, lini na wapi Kamati Kuu ya CCM iliketi, iliamua na kuelekeza kuwa Ukonga na Monduli kusiwe na kura za maoni? Halafu, Katibu Mkuu wa CCM na viongozi wengine mpo kimya tu. Kwanini?

Kura za maoni ni mchakato muhimu. Ni mchakato wa kichama na kisiasa. Lazima mgombea apimwe kukubalika kwake kuanzia kwa wanachama wa CCM wa Jimbo lake/Wilaya yake. Halafu, Kamati Kuu huidhinisha. Kura za maoni huonesha picha halisi ya mgombea mtarajiwa wa CCM katika Jimbo husika.

Ukimya huu wa viongozi wetu, huku kukiwa na malalamiko ya makada wetu wa CCM wa Monduli na Ukonga unatokana na kuwa na uhakika wa 'kushinda' chaguzi hizi za marudio? Katibu Mkuu wa CCM, Ndugu yangu Dr. Bashiru Ally uko wapi? Kuna tatizo chamani!

Majibu ya Jeshi la Polisi kwa Waziri Lugola yamemuimarisha na kumjenga sana!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
Alafu watamleta Nape na Bashe kumnadi waitara
 
Write your reply...nnje ya mada:nauliza waitara ndio yule meya?hadi kwenye uzinduzi wa daraja la kigamboni akasifiwa na mkuu huku akitaniwa (kiukweliukwel) kuwa huyu sio mpinzan ni wa kwetu?
 
Kuna wakati katibu mkuu alitoa maoni tofauti kuhusu kina Nape
 
Write your reply...nnje ya mada:nauliza waitara ndio yule meya?hadi kwenye uzinduzi wa daraja la kigamboni akasifiwa na mkuu huku akitaniwa (kiukweliukwel) kuwa huyu sio mpinzan ni wa kwetu?
Huyo unayemsema wewe anaitwa Isaya Mwita ni diwani wa kigamboni na pia ni Meya wa Jiji la Dar,

Mwita Waitara ni mbunge aliyejitowa ubunge wa jimbo la ukonga na anautaka ubunge wake.

Lipumba ndio muhasisi wa hizi siasa za kishamba, aliacha uenyekiti kwa hiyari yake baadaye anataka arejeshewe uenyekiti uleule.
 
Hujui tu, siku hizi kuna chombo kipya CCM kinaitwa "Mkuu wa Kamati kuu ya Halmashauri kuu". Huyo ndiye amekaa mwenyewe na keshaamua!
 
Alikuwa Arusha juzi jana nanenane akaonekana Simiyu ,Leo karudi Arusha possibly yupo njiani kurejea Dar
 
Uongo uko wap? Soma akina Coupland kuhusu Afrika wanasema au wanafananisha waafrika na wanyama wa porini

Ukishwa fananishwa na mnyama na akili zako ni ni sawa na wanyama akina nyumbu
Iq chini ya 80, ndio maana Hatua aibu
 
Ndoto yangu ya kugombea ubunge 2020 inaanza kufifia! Kwa hali hii, kuna uwezekano mkubwa 2020 wagombea wakateuliwa toka juu bila kufuata michakato ya kura za maoni jimboni!!
Ndo kitakachokuwa we subiria mkorogano ccm itauliwa na wana ccm wenyewe kuna kubwa sana kati ya kijani asili na kijani mateuzi.Hapo kuna kumwaga mboga kumkomoa mwenyekiti. Hivo wataamua ether waache kupiga kura au watawasapoti upinzani ili kumwaga mboga we subiria ya monduli ndo yatakuwa mengi.Kingstone hawezi shindana na umma.
 
Ukijaribu kuhoji majimbo yetu yakimkakati utashulikiwa vizuri tuu.
 
kwani kwenye gia ya angani kulifanyika kura za maoni au walikaa watu wachache wakapitisha jina la mgombea urais
 
nimeso
Waafrika waliopo chini ya jangwa la Sahara hawana akili,akili zao ni kama nyumbu,hawana uwezo wa kufikiria,hawana wanalolifanya hapa duniani,hawana mchango wowote hapa duniani,wanasindikiza dunia,

Waafrika waliopo chini ya jangwa la Sahara hawana akili,elimu mbovu,umasikini umekithiri lakini wanatumia mamilion ya Pesa kurudia uchaguzi wa mtu Yule yule kwa interest zake

Hizo bilioni zinazotumika kufanya uchaguzi na kununua wapinzani ni bora wangezigawa kwa kila kijiji ili wananchi waamini ahadi ya Rais

Lakini kwa vile tupo chini ya jangwa la hasara ngoja tusubiri miujiza kwenye maendeleo na viwanda
nimesoma comment yako yaani nimehuzunika na kufadhaika sana.....ngoja tu nikapige balimi ndogo moja maana sisi akili zetu ndivyo zilipofikia mwisho....
 
CCM ina wanachama wengi, imeunda serikali na ina mashabiki wa kutosha.
Kuhangaika na wapinzani wajiunge kwa ahadi za kugombea tena siyo sawa hata kidogo.
Huku ni kubomoa mshikamano na umoja wa wanachama,ni dharau kwa kwa walio wengi kwa kuondoa usawa na haki ya kuchagua au kuchaguliwa.
Madhara yake yaweza kuwa makubwa kuliko faida kwa wale wanachama wenye mtazamo wa kuona mbali.
 
Back
Top Bottom