Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi ni lazima sii hiyari, tudai vyote

CCM hawawezi kujifunza lolote linapokuja swala la kuachia madaraka ya nchi.Mifano ni mingi katika huu ulimwenge lakini wanajitia upofu.
Ni kweli mkuu unachosema, salary slip, kuwa linapokuja suala la kuendelea kubaki madarakani kwa njia zozote zile, ziwe za halali au haramu, CCM watafanya jambo lolote lile ili mradi liwe linawahakikishia kuendelea kubaki madarakani.

Lakini nieleze kitu kimoja, naweza kuifananisha CCM kwa sasa kama mgonjwa aliyeko ICU ambaye kuendelea kuishi kwake, kunategemea kuendelea kuwekwa 'ON' kwa mitambo ya oxygen inayomsaidia kupumua, na siku madaktari watakapoamua kuchukua maamuzi 'magumu' ya kuswitch 'OFF' mitambo hiyo, ndiyo itakuwa mwisho wa maisha ya huyo mgonjwa.

Vivyo hivyo kwa CCM, hivi sasa wapo ICU na wanapumulia mashine, na 'mashine' hiyo inayowafanya waendelee kupumua si nyingine, bali ni katiba ya zamani ya mwaka 1977, na kama ingetokea katiba hiyo ingefanikiwa kuwa replaced na katiba hii iliyoandaliwa kutokana na maoni ya wananchi, yaliyoratibiwa na Tume ya Warioba, hiyo ingekuwa sawa na mgonjwa aliyeko ICU na madaktari wakaamua kuzima mitambo inayomfanya aendelee kupumua, siku ambayo katiba ya zamani itaseize kutumika nchini, basi tutambue kuwa huo ndiyo utakuwa mwisho wa chama chetu 'kipenzi' cha CCM kuendelea kutawala nchini!

Ni ukweli ambao ni mgumu sana kuupokea, BUT THAT IS PURELY REALITY!
 
Nani kasema Katiba imeshindikana wakati iatapatikana tarehe 4 Oktoba na Bunge la Katiba linamaliza muda wake inabaki kazi ya kupiga kura ya maoni 201sitaaaaaaaaa. Kama kuna anayetegemea kuna bunge na wabunge wa bunge la Katiba baada ya tarehe hiyo imekula kwake. Viongozi waoga wa Ukawa wanajua lakini hawataki sema ukweli. Mmepotea
 
Hakuna Tume huru ya uchaguzi Mkuu, Tume ya uchaguzi ya MACCM itaendelea kuwa kitengo cha MACCM kama vitengo vyake vingine vya UVCCM na UWT. Kwa maneno haya ina maana 2015 hakutakuwa na uchaguzi huru na wa haki.
 
Viongozi wa UKAWA wanapaswa kutazama mbali zaidi vinginevyo wataishia kuwa walalamikaji tu na jamii itawachoka.
tatizo la Ukawa wanasema sana bila vitendo! Kinachotakiwa ni kuingia barabarani na mitaani kudai katiba mpya, wacha tupigwe tu, hakuna atakayeishi milele hapa duniani! Kwa mfumo wa ccm kwa taifa hili nadiriki kusema huwezi pata katiba mpya au tume huru kwa majadiliano tu ya mezani. Inahitaji jamii iliyohamasika na iliyotayari kudai katiba mpya bila woga.
 
Ni kweli kabisa unachosema nkongu ndasu, lakini vile vile tukumbuke kuwa hata huku kuanza kwa mchakato wa uundwaji wa katiba mpya, haukuanza kwa 'mapenzi' ya CCM, bali ilitokana na shinikizo kubwa sana, kutoka kwa makundi mbalimbali ya kisiasa na kijamii.

Kwa maana hiyo basi , let's hope for the best, the same spirit which enabled our country to 'launch' starting 'fetching' the path of having new constitution, can also enable us having 'real' National Electoral Commission!
tanzania kupata katiba mpya kwa hali ilivyo sasa haiwezekani, labda katiba mpya kwa kitabu tu kuwa kipya, lakini content ni ileile...
 
Nani kasema Katiba imeshindikana wakati iatapatikana tarehe 4 Oktoba na Bunge la Katiba linamaliza muda wake inabaki kazi ya kupiga kura ya maoni 201sitaaaaaaaaa. Kama kuna anayetegemea kuna bunge na wabunge wa bunge la Katiba baada ya tarehe hiyo imekula kwake. Viongozi waoga wa Ukawa wanajua lakini hawataki sema ukweli. Mmepotea
haa haa,katiba itakayopatikana oktober 4 ni katiba ya ccm na watawala kiujumla! Bila umma kuchukua hatua katiba mpya ni ndoto!
 
Hakuna Tume huru ya uchaguzi Mkuu, Tume ya uchaguzi ya MACCM itaendelea kuwa kitengo cha MACCM kama vitengo vyake vingine vya UVCCM na UWT. Kwa maneno haya ina maana 2015 hakutakuwa na uchaguzi huru na wa haki.
naunga mkono mkuu, ukawa wana option 2, au kuungana na wanyang'au hapo dodoma kama walivyofanya wapinzani feki kama kina cheyo, dovutwa, mrema na wengine. Au kuendelea kuuhamasisha umma hasa sisi vijana kupinga huu uhuni unaoendelea dodoma wa ukwapuaji wa mali za watanzania.
 
Ukiangalia kwa mbaaali zaidi naona ukaribisho wa Al shababi, Boko Haram, Al Qaeda n.k .
Haya makundi hayaji hivihivi lazima kuna sababu.
Kwa hali hii ya CCM wanavyotaka sidhani kama mtu utakuwa mzalendo na nchi yako.
 
inabidi Jaji Joseph Sinde Warioba ndio awe mwenyekiti wa tume huru ya uchaguzi, hapo ndio nitaamin hyo tume ni huru!

Kwanza hatakubali maana haamini katika kutengeneza katiba kwa njia tunayotaka kuifanya ya kuacha kiporo na kuja kukimalizia.
 
Ukiangalia kwa mbaaali zaidi naona ukaribisho wa Al shababi, Boko Haram, Al Qaeda n.k .
Haya makundi hayaji hivihivi lazima kuna sababu.
Kwa hali hii ya CCM wanavyotaka sidhani kama mtu utakuwa mzalendo na nchi yako.
ni kweli mkuu, kuwa mzalendo kwenye nchi inayoongozwa na unafiki wa viongozi wa aina hii ni ndoto.
 
Waislamu, wakulima na wafugaji, walimu, wasanii, wa uraia pacha n.k hakikisheni matakwa yenu mnayaunganisha kwenye kifurushi cha wanasiasa kudai tume huru kabla ya 2015 msikubali matakwa yenu yaahirishwe hadi 2016 ili kusubiri wanasiasa kuwaza tena mchakato wa katiba mpya wakati wao matakwa yao ya "msingi" washayapata.
 
Hivi wana -UKAWA mmejiuliza ni nini maana ya Raisi Kikwete kukabidhiwa rasimu ya katiba inayopendekezwa kwa mbwembwe na sherehe kubwa kama ile?Niwaambie tu kuwa hapo jibu ni kwamba ile rasimu ndio imepita.Unadhani wako tayari kusheherekea kitu ambacho hawana uhakika nacho?

Je,unadhani uhakika huo wanaotoa wapi zaidi ya kutegema tume ya uchaguzi?Kwa mazingira haya,tusitarajie tume huru ya uchaguzi bali kuibuka kwa mvutano na mgogoro mwingine kuhusu tume hiyo.

Kwasababu hizo basi,UKAWA msipoungana na kuwa na sauti moja hakika na hili litatushinda.Kosa kubwa mlilofanya wana-UKAWA ni kuwa mlikuwa kitu kimoja ndani ya Bunge la Katiba ila kwa bahati mbaya,nje ya Bunge hamkuwa kitu kimoja.Hili ndio kosa kubwa mlilolifanya na mkiendelea hivyo hatutakaa tupate ushindi.

Kama ilivyokuwa kwa Katiba mpya,CCM hawakuwahi,hawana na kamwe hawatakuwa na dhamira ya kuwa na Tume huru ya uchaguzi.

Hatua hii basi inahitaji ujasiri na umoja, tofauti na hapo itakula kwetu.

Mbali na mikutano ya hadhara,mipango na mikakati madhubuti ianza sasa.

Campagin za kura ya hapana bila Tume huru ya uchaguzi ni sawa mkutano wa campaign uliojaza wafuasi ambao hawajajiandikisha kupiga kura.

=Nashangazwa sana na huu ukimya wa viongozi wa UKAWA katika kudai tume huru ya uchaguzi ili hali muda unazidi kuyoyoma.

Kwa muda sasa,kumekuwa na ukimya kuhusu madai haya na sioni jitihada zozote za kuridhisha kupigania kupatikana kwa tume hii ili hali muda uliobaki ni takribani miezi 10 tu kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu hapo mwakani.

UKAWA,mkisubiri katiba mpya ipatikane(na inaweza isipatikane pia) itakuwa imekula kwenu kwani muda utakuwa hautoshi na hapo watawala(CCM) watapata sababu ya kuja na hoja kama hizi zifuatazo.

Mosi,watasema kwa kuwa muda uliobaki ni mfupi,basi uchaguzi huu usimamiwe na hii tume iliopo ili tuweze kwenda na ratiba ya uchaguzi kama ilivyopangwa.

Pili,wasivyo na aibu wa haya,CCM wanaweza kutoa pendekezo kuwa,kama ni lazima tume huru ipatikane,basi tumuongezee muda wa miezi 6(huo ni mfano tu) mheshimiwa raisi Kikwete kukaa madarakani ili tupate muda wa kutosha wa kuunda tume hiyo.

Najua raisi Kikwete aliwahi sema hakusudii kubaki madarakani pindi muda wake ukiisha ila mtambue tu mwanasiasa si mtu wa kumuamini sana.

Na niwaambie tu,wanajua kabisa hilo pendekezo la pili hamtalikubali kamwe na mtabaki na chaguo moja tu la kufanyaki kwa uchaguzi huo chini ya tume hii iliopo na hapo mkikubali tu, ndio tutakuwa tumepigwa bao la kisigino.

Pia,kwa mtazamo wangu,kesho kwenye hotuba yake,raisi Kikwete,pamoja na mambo mengine,anaweza pia kugusia swala hili la tume huru ya uchaguzi na kuwapa matumanini ila mwisho wa siku inaweza kuwa kinyume chake na nyinyi mtakuwa mmezidi kujisahau kwa kupewa matumaini hewa.

Viongozi wa UkAWA,pakuanzia papo na si pengine bali ni kukumbushia makubaliona yenu na raisi Kikwte kuwa tume huru ya uchaguzi iundwe wakati mchakato wa kupata katiba mpya ukiendelea.


Hint:Kama JK aliweza kuwageuka kuhusu muda wa kupiga kura ya maoni,atashindwa nini kuwageuka katika kutekeleza makubaliona ya kupata tume huru ya uchaguzi wakati tukisubiri katiba mpya ipatikane?

NB:Kwa matokeo ya uchaguzi huu wa serikali za mitaa,bila shinikizo na kugangamala,tume huru ya uchaguzi ni ndoto ya mchana.

Akili ya kuambiwa,changanya na zako-JK



Wadau wa Fikra pevu;

Bila shaka wengi tunaelewa juhudi kubwa ambazo zimeshafanywa ktk mabadiliko ya Siasa za Tanzania na kuimarika kwa Demokrasia iliyofikia hatua ya Vyama pinzani kuungwa mkono na kujiimarisha hadi ngazi ya chini kabisa vijijini na ktk vitongoji, na hivyo kuweka matumaini makubwa sana kwa Tanzania mpya kuzaliwa ifikapo Oktoba 2015.

Ufanisi huu wa Vyama vya Upinzani nchini, na hasa muungano wa Vyama vinne vilivyounda UKAWA [Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi na NLD], umewapa watawala wa CCM tumbo moto kila siku kukicha na hivyo kwa juhudi mbalimbali, watawala hawa wanatumia nguvu za ziada kwa kila kinachowezekana kurejesha nyuma matumaini ya Demokrasia na Watanzania kujikomboa na kujinasua ktk minyororo ya mateso iliyowakaba koo kwa zaidi ya Miaka 30 sasa chini ya Utawala huu wa CCM.

UKAWA imekuwa 'nyota ya asubuhi' ktk mioyo ya mamilioni ya Watanzania ambayo inang'aa na kuashiria 'ukombozi wa taifa' na kuundwa kwa utawala unaowajibika, unaojali watu, na unaotimiza ndoto za watanzania wengi.

Katika kuelekea Uchaguzi Mkuu hapo Oktoba, ambapo muda ndio unakaribia kwa kasi kubwa [uchaguzi upo mlangoni], pamoja na UKAWA kubeba matumaini ya ukombozi wa Taifa hili, yapo masuala 4 muhimu ambayo bila UKAWA kuyafanyia maamuzi ya Haraka na kupatiwa ufumbuzi wa haraka, kuna dalili za matumaini ya Ukombozi kutokukamilika mbele ya utawala huu unaolenga 'kufanya lolote' ili kusalia madarakani hata kama wananchi wote watapiga kura ya HAPANA!

Tutakumbuka kuwa, katika Makubaliano ya Rais JK na Viongozi wa UKAWA + TCD [2014], wakati wa 'mgogoro' wa kuvurugwa kwa Rasimu ya 2 ya Katiba Mpya', Mh Rais JK aliwaaminisha Wakuu wa Vyama, Watanzania, Wanaharakati na Taasisi za Kimataifa kuwa atahakikisha kuwa maamuzi ya Kikao chao yanatekelezwa mapema. Nini kimefanyika? Ndoto!

Haya Mambo 4 muhimu ndiyo masuali ambayo UKAWA wanatakiwa wajiulize mara 10 kabla ya kuelekea Uchaguzi wa Oktoba 2015:-


  • Wapi Sheria kuunda Tume Huru ya Uchaguzi? Bila Tume Huru ya Uchaguzi [NEC], Ushindi utaifikiaje UKAWA? - 'Tume ya CCM' wataipa UKAWA ushindi? Kivipi hata ikishinda?
  • Wapi Sheria kuruhusu Mgombea Huru? Sheria hii inayowafungia 'mikono mgongoni' wananchi wasiwe na maamuzi huru ya Kisiasa na Kikatiba inatupeleka wapi? Hii inaisaidia CCM au UKAWA?
  • Wapi Sheria kuamua Mshindi wa Urais kwa Asilimia 50 + 1 (50+ 1%)?? Hii inaisaidia CCM au UKAWA?
  • Wapi Sheria kuruhusu Mshindi wa Urais kupingwa Mahakamani?

Kwa mambo hayo manne, hadi sasa ilibidi UKAWA na wanaharakati wa Dekokrasia, Katiba na Haki za Binadamu, wawe walishawasilisha Maombi mahakamani kuhakikisha hatua stahiki za kisheria zinachukuliwa mapema iwezekanavyo. Ni Maswala ya Kikatiba, HAKI, na Demokrasia ambayo Mahakama itahitajika kuyafanyia Kazi bila ubishi au kigugumizi! Badala ya UKAWA 'kusubiria CCM uwaonee huruma', 'iwape ushindi' hapo Oktoba! TUME ni yao, ni ya Utawala wa CCM, itawezaje kuitukuza UKAWA? Oktoba ipo mlangoni, na Watawala na CCM wanaombea kila kukicha ili 'UKAWA iendelee kuyasahau haya mambo' ili iwe 'ahueni' kwao!. .....Mjumbe hauwawi!

Tuyatafakari mambo haya, ...UKAWA ni sauti ya Umma, tushauri, tuelekeze, tuchukue hatua haraka!!

Nawasilisha!
 
Nikiwa mwingi wa furaha kutona na matokeo niliyopata toka kila pembe ya nchii hii, Sina budi kushare nanyi wazo lililonijia haraka sana kichwani baada ya kupata matokeo hayo.

Nianze kwa kuwahabarisha kile tulichofanya jana Wanatunduma hapa Katika Mitaa 71 iliypo hapa Tunduma Chadema imechukua 48 ccm 23!!!!! ktk kura zote Wenyeviti,Vitongoji mpaka Viti maalum.

Nirudi kwenye mada,Wakuu Makamanda kwa Magamba, pamoja na kushangilia hili kwa kupata uamsho mpya kwa Wananchi kujitokeza kwa wingi na hatimaye kwa wingi uleule kujitokeza kupiga na hatimaye kulinda kura napata shaka sana na Uchaguzi wa Mwakani, Kwani utaratibu wa uchaguzi huu ni tofauti na uchaguzi mkuu ktk suala zima la kuhesabu na mpaka kutangaza Mshindi.

Wakati uchaguzi huu wa Mitaa kura zinapigwa na kuhesabiwa hapohapo, uchaguzi wa Madiwani,Ubunge na Rais ni tofauti kidogo kwani huu Mashindi aweza kutangazwa baada ya hata siku tatu!!! kitu ambacho kinatengeneza mazingira yaw kuchakachuliwa kirahisi hasa kutokana na uwepo wa Tume isiyokuwa huru na ambayo ndiyo yenye maamuzi ya Mwisho kwa mshindi kwani akishatangazwa tu kwa utaratibu wa sasa huwezi kuhoji popote (Kwa Urais).

Wakuu kila mmoja wetu kwa nafasi yake ameonja utamu ama uchungu wa uchaguzi huu hivyo kwa namna moja ama nyingine mapungufu yaliyotokea kwenye uchaguzi huu asingependa yajitokeze kwenye uchaguzi mkuu wakati kwa yale mazuri kila mmoja wetu angependa yaboreshwe ili kwenda na kasi ya wakati husika. Na moja ya Mapungufu hayo ni Uwepo wa TUME HURU YA UCHAGUZI.

Shime Watanzania tusiwaachie Viongozi wetu kushinikiza uwepo wa Tume hii, kwani tukishindwa tu kusimamisha Tume hiyo tuandike tumeumia ktk Uchaguzi ujao. Hawa watu bila shaka matokeo haya kwa namna moja yamewashitua na hayajawafurahisha hata kidogo na kwa hakika hawataki yawakute tena kwenye Uchaguzi mkuu.

Hivyo watakuja na mbinu mbalimbali za kutengeneza mazingira ya wizi ktk uchaguzi huo. Hii iliyofanyika jana nchi nzima ni kengere ya Alarm masikioni mwa hawa ccm hivyi watakwenda kujipanga kwa njia haramu na halali ili wasiweze kushindwa ktk uchguziw huo. Binasfi radha nzuri ya uchaguzi huu wa Serikali za mitaa nisingependa itoweke kwa namna ambayo ilitokea kwenye Uchaguzi wa Mwaka 2010 na hili hatuwezi kulikwepa kama tutawndelea kuwa na Tume hii inayoteuliwa na Kuwajibika kwa Rais.

Wakuu nirudie tena TUIPIGANIE KWA NGUVU ZOTE TUME HURU YA UCHAGUZI.

BACK TANGANYIKA
 
Tume huru ya uchaguzi badala ya hiki kitengo cha chama cha Maintarahamwe ambacho hufumbia macho taratibu mbali mbali zinazokiukwa na hiki chama cha wahuni na wezi na katika chaguzi zote Tume huhusika katika kuchakachua matokeo ya uchaguzi ni muhimu sana ikapatikana kabla ya uchaguzi mkuu wa 2015, lakini hii Serikali dhalimu itafanya kila hila ikiwemo uongo, unafiki n.k. ili kitengo chao hiki ndio kisimamie tena uchaguzi mkuu wa 2015.
 
kiukweli tume haipo huru japo wenyewe wanasema ipo huru haiwezi ikawa chini ya ofisi ya waziri mkuu bado tukasema ipo huru wakati uhuru hakuna
iwe taasisi inayojitegemea tutapowang'oa magamba 2015
 
Hahhahaaa mbona hawa wakwetu tu, unajua kuna idadi ya kuiba kura lakini kuna kura ambazo haziibiki tena.....kwa mfano sikumbuki ni wapi lakini nilisoma kama sio hapa JF basi ni kwenye group fulani kuwa msimamizi eti kasema kura mia mbili zimeharibika, hilo ni eneo dogo. kwa mtu mwenye akili kamwe haiingiii akili watu mia mbili wakosee, watiki vibaya au namna yoyote ile iwayo hadi wafikie mia mbili. Ninachosema hapa ni kwamba hata kama wataiba, kamwe ushindi kwetu utakuepo.
Simaanishi kwamba Tume Huru si muhimu. la hasha,nasema kwa hali ilivyo kwa sasa hata wakiiba bado sehemu kubwa tutawashinda tu.

labda kitu cha kuongeza hapo ni kuhakikisha kuwa Watu wetu wanaendelea kupata elimu ya utambuzi dhidi ya hawa wezi na wahuni wa uchumi wetu. Ni kuhakikisha kuwa wananchi wenyewe wanakua Walinzi wa kwanza kuhakikisha kile walichokifanya ni sahihi, ni hilo tu, yote mawili, tume huru ya uchaguzi na elimu ya utambuzi zaidi aaagh Magamba hayachomoi tena.

Naskia siku hizi sio Chama dume tena bali ni Tezi dume. Hongera zao watani zetu
 
Tume huru ya uchaguzi badala ya hiki kitengo cha chama cha Maintarahamwe ambacho hufumbia macho taratibu mbali mbali zinazokiukwa na hiki chama cha wahuni na wezi na katika chaguzi zote Tume huhusika katika kuchakachua matokeo ya uchaguzi ni muhimu sana ikapatikana kabla ya uchaguzi mkuu wa 2015, lakini hii Serikali dhalimu itafanya kila hila ikiwemo uongo, unafiki n.k. ili kitengo chao hiki ndio kisimamie tena uchaguzi mkuu wa 2015.

Mkuu ndiomaana nasema tuwe tayari kuifia hii tume, maana kinyume na hapo tumekwisha as usually

BACK TANGANYIKA
 
Mkuu Elli, ushindi bila kuongoza serikali ni kazi bure hapa mipango yetu yote kuanzia Ilani mpaka Sera za uchaguzi na chama ni kuongoza serikali ili tuweze kuvitekeleza. Sasa hatuwezi kufurahia kuongeza viti vya serikali za mitaa,Madiwani na Wabunge,ilhali hatupati serikali. Na iweleweke si kwasababu tunashindwa ila tunanywa kushindwa na hii inayojiita Tume ya Uchaguzi.

So hapa utaona wazi namna Tume huru ilivyo na tija katika suala zima la Uchaguzi. Na katika kushadidia hoja yangu hebu angalia mataifa yaliyopata Viongozi (Marais) nje ya chama kilichokuwa kinatawala utaona kama si Mapinduzi ya Umma basi Vyama vya Upinzani kwaw Support ya Wananchi vilipigania mpaka Kupatikana kwa TUME HURU YA UCHAGUZI hii ni kuanzia Kenya mpaka Zambia

BACK TANGANYIKA
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom