Invisible
Robot
- Feb 11, 2006
- 9,075
- 7,878
6 Aprili 2011
Mhe. Celine Kombani
Waziri wa Katiba na Sheria
Mheshimiwa Waziri,
Yah: TAHADHARI KUTOKA CCT JUU YA MUSWADA WA MAPENDEKEZO YA KUTUNGWA KWA SHERIA YA MABADILIKO YA KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA YA MWAKA 2011
Jumuiya ya Kikrito Tanzania (CCT) inaipongeza hatua ya kijasiri ya Serikali katika kusikiliza maoni ya wananchi hadi kufikia hatua hii ya kutoa muswada kuhusiana na hitaji lao la Katiba mpya. Hii ni hatua kubwa ambayo tumefurahishwa nayo sana.
Tarehe 11 Machi 2011, Serikali ilitangaza kuwepo kwa muswada uliokusudiwa kujadiliwa Bungeni mwezi Aprili mwaka huu, juu ya mabadiliko ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; Muswada Namba 1 wa mwaka 2011.
Mategemeo ya Jumuiya ya Kikristo Tanzania na wananchi kwa ujuma ni kwamba muswada huu utaruhusu uwazi na nafasi ya kushiriki kwa wanajamii wote ili kuweza kuweka bayana ni aina gani na mfumo upi wa Katiba wanayoitaka.
Lakini Muswada huo unaonyesha kutokuzingatia matarajio halisi ya wananchi, kwani lengo wanalolitaka wananchi ni kutungwa kwa Katiba mpya inayoendana na zama hizi na zijazo na sio mabadiliko tu ya Katiba ya nchi. Maudhui ya muswada yanafifisha na kudhoofisha ari na matarajio yao, maana mabadiliko yamekuwa yakifanyika kila mara lakini licha ya mabadiliko hayo mengi bado lengo la kupata Katiba mpya halijakidhiwa.
Hivyo basi CCT inatoa tahadhari kama ifuatavyo:-
Katiba ni mkataba ambao wananchi wanajiwekea kuonyesha jinsi wanavyotaka nchi itawaliwe na kuweka misingi ya kufuatwa na ukomo wa mamlaka kati ya watawala na watawaliwa. Hivyo wananchi ndio wenye usemi wa mwisho juu ya Katiba ya Nchi. Watawala wote akiwemo Rais ni waajiriwa wa wananchi ikiwa ni pamoja na Bunge; kwani wao huomba na kuingizwa kwenye utumishi kwa ridhaa ya wananchi kwa kutumia taratibu za kidemokrasia. Kwa hiyo hawana budi kuwarudia wananchi ili wapate maoni yao juu ya mstakabali endelevu wa nchi yao. Hivyo, ni sharti wananchi wenyewe wawezeshwe kutoa maoni yao moja kwa moja au kwa njia ya wawakilishi wa makundi yote ya kijamii.
Ipo hatari ya kukasimu mamlaka haya kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama Tawala kuteua Tume ya kusimamia mchakato huu ikiwemo Sekretarieti yake.
Utaratibu huu unamfanya Rais awe wa mwanzo na mwisho (Alpha na Omega) na kuondoa ushiriki wazi wa wananchi katika kusimamia na kuamua mstakabali wa nchi yao. Ni vyema mamlaka haya yakakasimiwa kwa wawakilishi wa wananchi kupitia Bunge na vyama vya siasa.
Mambo haya yanahitaji kupata muda wa kujifunza kutoka ndani na nje ya nchi (katika mtazamo hasi na chanya) ili kuwa na uelewa dhahiri utakaolenga katika kupata Katiba inayokidhi mahitaji ya wananchi. Tusijikute kwamba tunaharakia kufanya mabadiliko ya Katiba ili kukidhi hitaji la Uchaguzi ujao wa 2015 tu.
Ni vyema Tume ihusishe ushiriki wa wadau wote wa makundi yote ya kijamii, kisha iwasilishe taarifa yake kwa wawakilishi wa wananchi watakaokuwa wameiteua; kwa kupata ridhaa na maamuzi.
Tunakuomba utumie weledi na hekima yako kuhakikisha kwamba rai yetu inapewa nafasi na umuhimu katika jambo hili ili kuleta umoja, usawa, amani na utangamano pamoja na maendeleo ya nchi yetu yatakayotokana na Katiba iliyoandaliwa na wananchi wenyewe.
Askofu Mkuu Dkt. Valentino Mokiwa
MAKAMU WA KWANZA WA MWENYEKITI - CCT
Nakala: - Waziri Mkuu - Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
- Mwanasheria Mkuu wa Serikali
Mhe. Celine Kombani
Waziri wa Katiba na Sheria
Mheshimiwa Waziri,
Yah: TAHADHARI KUTOKA CCT JUU YA MUSWADA WA MAPENDEKEZO YA KUTUNGWA KWA SHERIA YA MABADILIKO YA KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA YA MWAKA 2011
Jumuiya ya Kikrito Tanzania (CCT) inaipongeza hatua ya kijasiri ya Serikali katika kusikiliza maoni ya wananchi hadi kufikia hatua hii ya kutoa muswada kuhusiana na hitaji lao la Katiba mpya. Hii ni hatua kubwa ambayo tumefurahishwa nayo sana.
Tarehe 11 Machi 2011, Serikali ilitangaza kuwepo kwa muswada uliokusudiwa kujadiliwa Bungeni mwezi Aprili mwaka huu, juu ya mabadiliko ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; Muswada Namba 1 wa mwaka 2011.
Mategemeo ya Jumuiya ya Kikristo Tanzania na wananchi kwa ujuma ni kwamba muswada huu utaruhusu uwazi na nafasi ya kushiriki kwa wanajamii wote ili kuweza kuweka bayana ni aina gani na mfumo upi wa Katiba wanayoitaka.
Lakini Muswada huo unaonyesha kutokuzingatia matarajio halisi ya wananchi, kwani lengo wanalolitaka wananchi ni kutungwa kwa Katiba mpya inayoendana na zama hizi na zijazo na sio mabadiliko tu ya Katiba ya nchi. Maudhui ya muswada yanafifisha na kudhoofisha ari na matarajio yao, maana mabadiliko yamekuwa yakifanyika kila mara lakini licha ya mabadiliko hayo mengi bado lengo la kupata Katiba mpya halijakidhiwa.
Hivyo basi CCT inatoa tahadhari kama ifuatavyo:-
Katiba ni mkataba ambao wananchi wanajiwekea kuonyesha jinsi wanavyotaka nchi itawaliwe na kuweka misingi ya kufuatwa na ukomo wa mamlaka kati ya watawala na watawaliwa. Hivyo wananchi ndio wenye usemi wa mwisho juu ya Katiba ya Nchi. Watawala wote akiwemo Rais ni waajiriwa wa wananchi ikiwa ni pamoja na Bunge; kwani wao huomba na kuingizwa kwenye utumishi kwa ridhaa ya wananchi kwa kutumia taratibu za kidemokrasia. Kwa hiyo hawana budi kuwarudia wananchi ili wapate maoni yao juu ya mstakabali endelevu wa nchi yao. Hivyo, ni sharti wananchi wenyewe wawezeshwe kutoa maoni yao moja kwa moja au kwa njia ya wawakilishi wa makundi yote ya kijamii.
Ipo hatari ya kukasimu mamlaka haya kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama Tawala kuteua Tume ya kusimamia mchakato huu ikiwemo Sekretarieti yake.
Utaratibu huu unamfanya Rais awe wa mwanzo na mwisho (Alpha na Omega) na kuondoa ushiriki wazi wa wananchi katika kusimamia na kuamua mstakabali wa nchi yao. Ni vyema mamlaka haya yakakasimiwa kwa wawakilishi wa wananchi kupitia Bunge na vyama vya siasa.
Mambo haya yanahitaji kupata muda wa kujifunza kutoka ndani na nje ya nchi (katika mtazamo hasi na chanya) ili kuwa na uelewa dhahiri utakaolenga katika kupata Katiba inayokidhi mahitaji ya wananchi. Tusijikute kwamba tunaharakia kufanya mabadiliko ya Katiba ili kukidhi hitaji la Uchaguzi ujao wa 2015 tu.
Ni vyema Tume ihusishe ushiriki wa wadau wote wa makundi yote ya kijamii, kisha iwasilishe taarifa yake kwa wawakilishi wa wananchi watakaokuwa wameiteua; kwa kupata ridhaa na maamuzi.
Tunakuomba utumie weledi na hekima yako kuhakikisha kwamba rai yetu inapewa nafasi na umuhimu katika jambo hili ili kuleta umoja, usawa, amani na utangamano pamoja na maendeleo ya nchi yetu yatakayotokana na Katiba iliyoandaliwa na wananchi wenyewe.
Askofu Mkuu Dkt. Valentino Mokiwa
MAKAMU WA KWANZA WA MWENYEKITI - CCT
Nakala: - Waziri Mkuu - Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
- Mwanasheria Mkuu wa Serikali