KATIBA: Askofu Ruzoka amlima barua Waziri

KATIBA: Askofu Ruzoka amlima barua Waziri

Invisible

Robot
Joined
Feb 26, 2006
Posts
16,285
Reaction score
8,464
JPLETTER.jpg
 
Editable text:

HOFU NA MASHAKA YA WANANCHI KUHUSU
MUSWADA WA MAPENDEKEZO YA KUTUNGWA KWA SHERIA
YA MABADILIKO YA KATIBA YA NCHI YA MWAKA 2011

Kwa
Waziri wa Katiba na Sheria

Mheshimiwa Waziri,
Muswada wa Mabadiliko ya Katiba ya Nchi wa mwaka 2011 Namba 1 wa tarehe 11 Machi, 2011 umetangazwa katika siku chache zilizopita.

Baada ya kuusoma muswada huu tulishangazwa kuona kwamba mchakato wote unaanzia na kuishia kwa Rais na kwamba Chombo Kikuu cha kuratibu mchakato wote ni Tume itakayoteuliwa na Rais ambaye ni Mwenyekiti wa Chama tawala.

Tunatambua kwamba kilio cha kutaka Katiba mpya kilitokana na utashi mwema na pia hasira njema ya jamii ya Watanzania wakitaka mabadiliko yaliyo na hekima na utu.

Tunahofia kwamba maudhui na mwelekeo wa muswada wa marekebisho ya Katiba unaopelekwa Bungeni havitakidhi mahitaji mazito ya watu na huenda ukachochea hasira ambayo imekwisha jidhihirisha katika jamii yetu.

Tunakuomba ulisimamie zoezi la marekebisho ya katiba kwa hekima sana ukiongoza tafakari jadidi na elimu angavu itakayowezesha zoezi lote kuwa la mazungumzo ya kitaifa kweli kweli huku amani, maelewano na makubaliano vikilindwa sana katika wakati mgumu huu.

Tafadhali lipatie taifa muda wa kufaa na chombo huru kinachoaminika kuongoza wananchi kufikia makubaliano yatakayojenga msingi imara wa taifa letu kwa wakati ujao.


Askofu Mkuu Paulo Ruzoka
MWENYEKITI

TUME YA HAKI NA AMANI (TEC)

5/4/2011
 
Umeishapelekwa bungeni hawezi kurudi nyuma

Serikali haina DINI
Mkuu sijui kama umesoma vema; sijaona kipengele ambacho kasema USIENDE Bungeni ama alikosema Serikali iwe na dini.
 
Appreciable initiative, but i smell something fishy on this innocent thread.

Watchful waiting.
 
Mambo yameanza sasa.

Ni dhahiri huu mchakato unaburuzwa kwa nia ya kulinda maslahi ya baadhi ya watu na haswa watawala pasipo kujua ya kwamba Katiba ni ya Watanzania wote.

Waliongea wadau na washiriki mbalimbali katika kongamano la kujadili mchakato wa Katiba mpya pale Chuo Kikuu sehemu ya Mlimani na kikubwa ni kwa wengi kutokuridhishwa na jinsi zoezi lenyewe linavyoendeshwa. Tunahitaji tume huru ambayo itakuwa tayari kuchukua maoni ya walio wengi na kuyafanyia kazi.

Je, suala hili linavyoendeshwa kwa sasa tuendelee kuwa na imani nalo? Sidhani, kama serikali wanania ya dhati kabisa ya mabadiliko haya. Barua ya Askofu Ruzoka ni mwanzo mzuri wa kuonyesha kutoridhishwa na uendeshaji wa mchakato huu unaofanywa na serikali kwa sasa.
 
Asante mkuu invisible.

Tunashukuru kwa viongozi wetu wa dini kwa kuliona hili. Huu ni ukweli usiojificha huo muswaada una mapungufu, kwanini viongozi wetu wana tamaa ya madaraka.

Comrades, your time is over waachie na wengine jamani kama wewe ni mpenda amani unayoitangaza kila siku step down basi
 
Mmmmmh jamani mambo ya shakuwa mambo,

Kama serikali itaendelea kukaidi maoni ya wananchi naona watakuwa wameruhusu wenyewe Nguvu ya umma ichukue hatamu katika kujenga katiba.....
 
kanisa likishasema basi hakuna wa kupinga!muswada umeshagonga mwamba!
 
Kwani wapi amesema usipelekwe bungeni? Halafu wapi ameongelea dini jaman? Si ifike mahali tuache ushabiki wa kidini kwny mambo ya msingi?
Umeishapelekwa bungeni hawezi kurudi nyuma

Serikali haina DINI
 
kama ni mwelewa na anacmamia haki, atafuata alyoelekezw kwnye barua kwa manufaa ya waTZ wote! Mungu ibarik Tz, Mungu 2barik waTz!
 
Umeishapelekwa bungeni hawezi kurudi nyuma

Serikali haina DINI


Tatizo lako unatumia mak**** kufikiri badala ya ubongo. Kuna sehemu umeona wamesema usiende bungeni? Au kwamba serikali ina dini?
 
Kama sehemu ya jamii, Kama wadau wa amani na utulivu, Kama wadau wa maendeleo, na kama Watanzania, nakubaliana kuwa viongozi wa dini kwa kuwakilisha wanaowaongoza watoe maoni yao yao mama kukubali au kupinga mchakato huu.

Naamini serikali inatakiwa ijue kuwa yenyewe bila ushiriano wa wananchi na makundi mbali mbali ya wananchi haitaweza kutengeneza katiba inayotosheleza matakwa ya watanzania wengi.
 
piga ua ufisadi utafikia kikomo very soon.



1) wakibadili katiba na kuwapa wananchi katiba wayoitaka, kuna uwezekano mkubwa CCM ikatoka madarakani, ika vunjika na mafisadi
kushugulikiwa.


2) wakileta mzaha na kutengeneza katiba wanayoijua wao kwa mchakato wao , basi watakua wanatengeneza mazingira ya North Africa
(na huko uarabuni) na mwisho wake BADO mafisadi itabidi waondolewe
 
Hivi kwanini Kupeng'e unakimbilia sana U-DINI?

Katiba mpya lazima ijumuhishe makundi yote ya JAMII - Should transcend all boundaries! BAKWATA,KKKT, & TEC all inclusive.. Tukianza kutizamana kwa jicho la udini tutakuwa tunawapa wanasiasa nafasi ya kuendelea kututawala with impunity!

Jaribu kuwa na POSITIVE ATTITUDE angalau kwa mambo yanagusa maisha ya Watanzania wote!

Ni hayo tu
 
Kwanini hajaandika barua yeye kama yeye? na kaamua kupitia TEC

Kupeng'e aka malaria sugu, aka jeykey wa ukweli, aka mtoto wa jeykey, aka francis muro, aka basra rashid, aka jinomswakiwanini, aka.....; wewe ulitaka aandike yeye kama yeye kwa sababu gani wakati taasisi ipo?

Na wewe mwandikie huyo waziri mkuu kupinga barua ya TEC.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom