Kati ya baba na mama wewe unampenda nani?

Kati ya baba na mama wewe unampenda nani?

Haijalishi walipendana ama walipigana
Kwangu mzazi ni mzazi pamoja na mapugufu yote
Kuanza kuchagua mmoja kati yao ni 'utoto', hayo mambo nilifanya nikiwa darasa la 5
baada ya kukua na kuona maisha, wote ni wazazi basi

Familia uliyotoka na makuzi uliyokulia yanachangia kwa wewe kutoweza changua nani unempenda ila ni tofauti sana na maelezo ya mtoa mada na watu wengine, mfano mimi when I was young, nilikuwa naona jinsi my mother anavyokuwa mistreated na dad, tena bila huruma mara kibao tu alikuwa anafukuzwa na kulala nje na mimi nikiwa naye all the times hadi dady akawa anadai mimi na mama yangu letu moja though hata sikujuaga ugomvi wao ulikuwa unasababishwa na nini.

Mimi kiukweli nampenda sana mama yangu tena sana ila simchukii dad ila uzito wa penzi uko kwa mama na mdingi analijua hilo ila hana jinsi na uzuri huwa anakiri kuwa alimkosea mama na huwa anaomba msamaha kwa aliyomtendea. KongoshO mshukuru Mungu kama wazazi wako waliishi kwa upendo na amani
 
mama yangu ni kila kitu

my mom is my everything,nna perception hii labda kwa sababu baba yangu alifariki mapema na nikakaa na mama tu ambae ame hustle saana hadi sasa nna maisha yangu mwenyewe I will always be grateful to her.
 
Oedip complex inasema wanaume wanawapenda mama zaidi, wanawake wanawapenda baba zaidi. Voila!

Mimi mama yangu ni Mungu wangu wa pili.......Nina almost miezi kama 7.....sijawahi dial number za dingi......yani ki ufupi simfeel kivile.....au kabisa.....
 
nmeishi na baba na mama! Nampenda baba zaidi, na yy anajua inafika wakati hata akiugua huwa anasema wasiniambie, maana naweza kwenda nyumban hta ucku wa manane! Baba yangu oyeeeeee
 
::
Nachojua mimi mtoto wa kiume anampenda sana Mama,
Na yule wa kike anampenda sana Baba.
Na ikitokea mtoto wa kiume amepata binti wa kuoa mwenye tabia kama za mama yake atamuoa haraka Na kinyume chake kwa binti.
NB
Mtazamo wa kisaikolojia sio wa kimalezi.
=

Nakuunga mkono; nampenda sana mama; nina watoto wawili jinsia tofauti, mtoto wa kike ananipenda sana. Nikiwa pale nyumbani anapenda sana kukaa na mimi na kuniuliza vijiswali vingi sana; ila sasa wa kiume muda mwingi anapenda kuwa na mama yake, kumsindikiza sehemu mbali mbali n.k
NANI KAMA MAMA? SIJAWAHI SIKIA M2 AKISEMA NANI KAMA BABA.....
 
Haijalishi walipendana ama walipigana
Kwangu mzazi ni mzazi pamoja na mapugufu yote
Kuanza kuchagua mmoja kati yao ni 'utoto', hayo mambo nilifanya nikiwa darasa la 5
baada ya kukua na kuona maisha, wote ni wazazi basi

Narudia swali la mtoa mada ..
Kati ya baba na mama wewe unampenda nani?

Labda atubadilishie isomeke hivi ...
Kati ya baba na mama wewe unampenda nani zaidi?

Swali lake sio kama unavyomaanisha wewe, umechangia utafikiri kauliza hivi
Kati ya baba na mama; nani mzazi?
 
Kwa BABA anayeijua nafasi yake Kumpenda lazima uwe vizuri kichwani-Ndo maana nahisi mleta mada ni below 30. "A really father never spare the rod"
 
Kweli swali hili ni gumu sana kwangu huenda ni kwa sababu sijakaa sana na wazazi wangu zaidi ya kuwa nao muda wa likizo, hata hivyo muda huo walikuwa wakienda kazini na kurudi jioni labda tumepumzika wote wiki-end na yenyewe mara nyingi tulikuwa tunapata wageni. Ila nawapenda wote maana naona kila mtu amecheza nafasi yake, japo tofauti inakuja pale ninapopata tatizo Mama analichukulia kwa uzito sana ila Baba analichukulia simple sana japo ana-support. Baba alikuwa anapenda kutoka na mimi japo mama naye huwa ananipokea vizuri, Mama alikuwa ananichapa wakati mwingine huku Baba hajawahi nichapa zaidi ya kunielekeza. Nashindwa kujua nampenda nani kwa sana, nikimfikiria baba naona nampenda zaidi, mama naye naona nampenda zaidi, dah! nashindwa japo mwanangu wa kiume naona anampenda mama yake zaidi harafu ananizuga nisigunduwe.
 
Mimi nawapenda sana wazazi wangu wote wawili.Lakini mama yangu alikuwa zaidi ya mama.Sikuwahi kuishi na baba but niliwahi kushuhudia mama akilia juu yangu kisa baba amekataa kunisomesha fomu one.Kwa chozi la mama na maneno aliyomtamkia baba alijikuta mwenyewe anakubali kunilipia ada.Zaidi ya hayo mama yangu amelikuwa akinipigania kwa kila jambo na hakupenda kuona napata shida ndani ya dunia hii.I love you mom. even though we are not together physically but spiritually we are together.
 
Mimi mama yangu ni Mungu wangu wa pili.......Nina almost miezi kama 7.....sijawahi dial number za dingi......yani ki ufupi simfeel kivile.....au kabisa.....
Kweli wanaume tumeumbwa mateso...!.
 
Mapenzi kwa mtoto/mzazi yanaweza kugawanyika. Hata wazazi(baadhi ) wanakuwa na mapenzi zaidi kwa baadhi ya watoto wao. Ila kwa busara sana, hawatakiwi kuonyesha au kubagua watoto.
Kwa hiyo si ajabu kwa mtoto kumpenda zaidi mzazi mmoja kuliko mwingine, na mara nuingi sababu zinakuwepo, tena za kutosha tu. Mimi sioni ajabu sana. Nawapenda wazazi wangu wote ila definitely mmoja kati yao anaweza kuwa na nafasi zaidi kwenye moyo wangu.
 
i luv my father moree kwa kweli,,,, mama nae nampenda, ila baba zaidi,,, pamoja na ukali wake, lkn he was always there for me, nakumbuka zamani, mama na baba waliishi mikoa tofauti kwa sababu za kikazi, na baba akanichukua na kuishi na mimi, kipindi icho just a young boy,, around 3 - 9 yearz,,,, mpaka walipobahatika kupata kazi sehemu moja tena,,,, God bless u daddy,,, nakupenda sana baba.
 
Back
Top Bottom