Kataa Ugali, Ugali ni Mateso

Sio kweli.

Wali mweupe ni mbaya kuliko ugali wa sembe.

Ugali wa dona ni bora kuliko ugali wa sembe.

Ugali wa dona ni bora kuliko wali mweupe, ni bora hata kuliko viazi vitamu.
 
Shida sio ugali, shida ugali unakula na nini..
Kweli ugali unakosa madini mengi tu.
Lakini ugali hauliwi pekee yake, ugali unaenda na mboga gani!!

Juzi kati nimeenda kwa mama ntilie ugali ule ni mtamu, mboga standard mpaka nikamuuliza kwa buku jero hupati hasara kweli!?

Ugali laini,
Dagaa wametiwa nazi
Maharage nazi
Mboga za majani
Na nyama

Mboga zoote quality, si mpenzi saana wa ugali, ila ile nilikula ugali mchana kwa siku 5 mfululizo
 

Attachments

  • IMG_20250616_160519.jpg
    402.7 KB · Views: 12
  • IMG_20250616_160954.jpg
    351.5 KB · Views: 7
Ugali na kitimoto lost.Hii kampeni imeshafeli.
 
ugali ndio hushibisha vema kuliko mapochopocho mengine
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…