Kasumba kuhusiana na mji wa Moshi

Kasumba kuhusiana na mji wa Moshi

Forrest Gump

JF-Expert Member
Joined
Jul 2, 2021
Posts
757
Reaction score
2,141
Nimekuwa naona mijadala mbali mbali juu ya miji tofauti hapa Tanzania. Mijadala juu ya maisha ya kijamii, mzunguko wa fedha, fursa za biashara, utulivu wa mji, mwingiliano na ukarimu (hospitality)

Ukigusia mji wa Moshi, tumekuwa tunapata hisia mchanganyiko (positive na negative). L

Ningependa tupate maoni ya wana jamii waliohamia kwenda mji wa Moshi na hali ya maisha waliokutana nayo hapo katika nyanja tofauti za jamii, uchumi na biashara.

Karibu.
 
Moshi pagumu sana kupata hela, kila mtu mjanja mjanja, biashara za kujuana, matajiri wachache wamehodhi biashara zote za maana huwezi ibuka na wazo lako jipya la biashara ukatoboa maana unadhibitiwa chap.

Biashara za moshi labda ufanye kuchuuza bidhaa upate senti mbili tatu
 
Moshi pagumu sana kupata hela, kila mtu mjanja mjanja, biashara za kujuana, matajiri wachache wamehodhi biashara zote za maana huwezi ibuka na wazo lako jipya la biashara ukatoboa maana unadhibitiwa chap. Biashara za moshi labda ufanye kuchuuza bidhaa upate senti mbili tatu
Ukianza kusoma ulichoandika na mwisho ni kwamba Moshi panafaa kufanya biashara!!...Kama unaweza kuanza biashara Ndogo Ndogo ni sehemu salama sana
 
Moshi janja janja Sana si wanaume si wanawake wote ni wa janja kwa mgeni si rahisi kutoboa Mana wenzio unakuta tayari fursa ZOTE wameshaziteka labda uwe na mtaji Mkubwa ndo waweza fanikiwa.
Mtaji na kufanya biashara kweli utatoboa!!..Moshi kuna makabila Aina tofauti wanafanya biashara vizuri sana!!
 
Mtaji na kufanya biashara kweli utatoboa!!..Moshi kuna makabila Aina tofauti wanafanya biashara vizuri sana!!
Moshi vijijini Kuna wa Bibi wa kichaga miaka 70 wanafuga ngombe wa maziwa 2 au 3 kibiashara wanapanda milima na kushuka kusaka nyasi za kulishia ngombe ni hatari.

Kule kiboriloni sokoni Kuna wanawake wanafanya biashara ya mitumba ni hatari , Wachaga popote mlipo nawapa Salute,.
 
Francis..tupatie mawili matatu kuhusiana na moshi bila ya kuweka upendeleo
Katika Miji rahisi kutoboa ni Moshi!!..Moshi kuna mkusanyiko wa wachagga (Tuongelee hii)..Wachagga ni watu wanaopenda biashara sana na kupenda vitu vipya!

Wachagga wengi wanaoishi Moshi bado ni washamba na biashara nyingi zinafanywa na watu wageni (ukiingia ndani).

Hakuna Mchagga mbaguzi kama wewe hukumbagua,Hakuna watu wanapenda wageni kama wachagga ndio maana unaona Moshi mjini wafanyabiashara wengi ni wageni!!.

Ukienda Kibororoni ya Leo au Majengo hukuti Wachagga kama awali ni kwasababu ya kukubali wageni kuleta maendeleo

Kati sehemu ambazo hakuna ukilitimba wa biashara Moshi is the best!!...Moshi hakuna mtu anaejali unatokea wapi as long watu wanapata mahitaji salama kutoka kwako!!...Moshi kuna watu binafsi wanakopesha vijana wengi tena mikopo isiyokua na Dhamana!!.

Moshi kokote pale Unaweza kufanya biashara unazingatia usafi tu!!..Ajabu ni kwamba Wachagga wanauza Ndizi zao huko milimani kuja kununua Ndizi za kukaanga,maandazi,chapati etc Mjini kwasababu vitu hivyo vikipikwa na makabila mengine ni vitamu zaidi
 
Moshi fursa zimebana sana!! Hakuna ardhi ya kutosha,hakuna uvuvi,hakuna ufugaji mkubwa,hakuna madini,hakuna viwanda kama ilivyokua zamani!!! Kwakeli tusidanganyane ni pagumu hasa!
 
Nimekuwa naona mijadala mbali mbali juu ya miji tofauti hapa Tanzania. Mijadala juu ya maisha ya kijamii, mzunguko wa fedha, fursa za biashara, utulivu wa mji, mwingiliano na ukarimu (hospitality)

Ukigusia mji wa Moshi, tumekuwa tunapata hisia mchanganyiko (positive na negative). L

Ningependa tupate maoni ya wana jamii waliohamia kwenda mji wa Moshi na hali ya maisha waliokutana nayo hapo katika nyanja tofauti za jamii, uchumi na biashara.

Karibu.
Moshi Pazur Nmezaliwa moshi ,Maji mazur Tanzania nzima,Biashara Nzur Inalipa,Kind people na vingine Yan best of the best.
 
Katika Miji rahisi kutoboa ni Moshi!!..Moshi kuna mkusanyiko wa wachagga (Tuongelee hii)..Wachagga ni watu wanaopenda biashara sana na kupenda vitu vipya!

Wachagga wengi wanaoishi Moshi bado ni washamba na biashara nyingi zinafanywa na watu wageni (ukiingia ndani).

Hakuna Mchagga mbaguzi kama wewe hukumbagua,Hakuna watu wanapenda wageni kama wachagga ndio maana unaona Moshi mjini wafanyabiashara wengi ni wageni!!.

Ukienda Kibororoni ya Leo au Majengo hukuti Wachagga kama awali ni kwasababu ya kukubali wageni kuleta maendeleo

Kati sehemu ambazo hakuna ukilitimba wa biashara Moshi is the best!!...Moshi hakuna mtu anaejali unatokea wapi as long watu wanapata mahitaji salama kutoka kwako!!...Moshi kuna watu binafsi wanakopesha vijana wengi tena mikopo isiyokua na Dhamana!!.

Moshi kokote pale Unaweza kufanya biashara unazingatia usafi tu!!..Ajabu ni kwamba Wachagga wanauza Ndizi zao huko milimani kuja kununua Ndizi za kukaanga,maandazi,chapati etc Mjini kwasababu vitu hivyo vikipikwa na makabila mengine ni vitamu zaidi
Mkuu umeandika ukweli mtupu
 
Moshi fursa zimebana sana!! Hakuna ardhi ya kutosha,hakuna uvuvi,hakuna ufugaji mkubwa,hakuna madini,hakuna viwanda kama ilivyokua zamani!!! Kwakeli tusidanganyane ni pagumu hasa!
Ufugaji upi unasemea ??
Ukitaka juq ufugaji nenda mnadani au buchani nunua nyama (which is cheap sana Moshi?))
Fursa zipo zinabadilika overtime now kuna utalii, huduma, usafirishaji, viwanda bado vipi ila ardhi ni shida na ardhi ya wachaga ni ndogo na hawauzi
 
Juzi nimepita Moshi Double Road hapana Vibe kama miaka ya nyuma
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom