Kassim Majaliwa ateuliwa na Rais Magufuli kuwa Waziri Mkuu awamu ya tano (Wasifu wake)

Magazetini

JF-Expert Member
Aug 16, 2014
588
1,698

attachment.php


Habari wakuu,

Subira yavuta heri, hatimae Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, Dr. John Pombe amepeleka pendekezo la jina la waziri mkuu kwa awamu ya Tano anayoiongoza. Rais amempendekeza Majaliwa Kassim Majaliwa kuwa waziri mkuu ambae anahitajika kuthibitishwa na bunge kwa kura za siri kabla ya kutangazwa rasmi.

Majaliwa anapendekezwa kuwa waziri mkuu baada ya kumaliza kutumikia Unaibu waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Ofisi ya Waziri Mkuu wakati wa serikali ya awamu nne chini ya Rais Jakaya Kikwete.

Majaliwa ambae kazaliwa Desemba 22, 1960 pia aliwahi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Rufiji mkoani Pwani hadi mwaka 2009. Pia aliwahi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Urambo mkoani Tabora.

Kadhalika, Majaliwa amekuwa Mbunge wa Ruangwa tangu 2010, alisomea Ualimu Chuo cha Ualimu Mtwara na Mafunzo ya JKT alifanyia kambi ya Makutopora mkoani Dodoma. Pia alisoma katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na pia aliwahi kuwa Katibu wa Chama cha Walimu Singida. Majaliwa alisoma elimu yake ya msingi katika shule ya msingi Mnacho mwaka 1970 mpaka 1976 na baadae akajiunga na shule ya sekondari Kigosensera mwaka 1977.

Baada ya wabunge kupiga kura, alithibitishwa na bunge baada kupata kura nyingi zaidi za ndio hivyo kuwa waziri mkuu wa awamu ya tano.

Wabunge 394
Wabunge waliosajiliwa 369
Wabunge wanaotakiwa kufika akidi 184
Wabunge waliopo na kupiga kura 351
Kura zilizoharibika 2 (0.06%)
Kura za Hapana 91 (25.9%)
Kura za Ndio 258 (73.5%)




Personal Details
Salutation: Hon.
Surname: Majaliwa
First Name: Kassim
Middle Name: Majaliwa
Date of Birth: 22 Dec. 1960
Marital Status: Married
Sex: Male
Mobile Number: (+255) 785 205 910
Email: majaliwa.kasimu(at)yahoo.com
Address: P.O.Box 51, Ruangwa

Education Background:

Primary Education: 1970 -1976 Mnacho Primary School
CSEE: 1977-1980 Kigonsera Secondary School
- 1991 - 1993 Mtwara Teachers College
Bachelors Degree 1994 - 1998 University of Dar es Salaam
PGDP 1999 - 1999 Stockholm University

Other Trainings:
-

Experience
2010 - 2015 Member of Parliament
2006 - 2010 District Commissioner
2001 - 2006 Reginal Secretary (PS - CWJ)
2001 - 2001 District Commissioner (PS - CWJ)
1988 - 2000 PS - Moec (Instructor)
1984 - 1986 TD - Lindi Council (Teacher)

Hobbies: Soccer
 

Attachments

  • Kassim.jpg
    Kassim.jpg
    20.4 KB · Views: 21,053
Last edited by a moderator:
Ni maamuzi sahihi

Lizabon, kwa mara ya kwanza niungane na wewe. Ningehuzunika sana kama yule aliyekana andiko lake la PhD angepewa hicho cheo. Mungu ni mwema Mh JPM kapendelea watu wasio na makundi na wanafiki. Hakuna jambo zuri kama kusimamia andiko lako lililokupa Cheti.
 
Safi sana Magufuli. Sasa bado mtihani mmoja, tupa kule makamba na rizi kwenye baraza lako la mawaziri ili tuzidi kukwamini kuwa hutoi vyeo kishkaji
 
Wimpish move, chaguo la uoga.

Naibu Waziri Tawala za Mikoa is not enough qualification for Prime Minister's office. President decided to follow Benjamin Mkapa's textbook, chagua muendesha baiskeli mmoja asiyejulikana wala kujua lolote awe Waziri Mkuu asije akakufunika au akawa too influencial with party and government.

Jakaya Kikwete alijaribu a powerful Prime Minister akaja funikwa from day one. Magufuli ameogopa. Such a wimpish move. Bunge linaenda kumu evaluate. On what record? Majaliwa who?
 
nikiwa mwanachama hai wa upinzani... nakupongeza Mh. Magufuli tunahitaji mishtuko kama hii ili tuweze kuondokana na siasa za kinafiki... huyu jamaa sijamsikia hata mara moja akitukana ovyoo wala akiiponda upinzani...maanake ni Mtanzania na sio MCCM ... umenipa moyo baba... naona umebadilisha gia hewani kwa kumpiga chali mwenyekiti mkuu wa ccm... haya mambo yafanye hata kwa baraza lako la mawaziri baba... ule wimbo wa ccm ni ileile ubadilishwe mapema..
 
Wimpish move, chaguo la uoga.

Naibu Waziri Tawala za Mikoa is not enough qualification for Prime Minister's office. President decided to follow Benjamin Mkapa's textbook, chagua muendesha baiskeli mmoja asiyejulikana wala kujua lolote awe Waziri Mkuu asije akakufunika au akawa too influencial with party and government.

Jakaya Kikwete alijaribu a powerful Prime Minister akaja funikwa from day one. Magufuli ameogopa. Such a wimpish move. Bunge linaenda kumu evaluate. On what record? Majaliwa who?
Hivi ulitaka amchague Diamond?
 
Tanzania imekwisha, tutashudia maajabu, yaani wajanja wameshinda, wote hakuna anayeweza compete kimataifa. Mungu tusaidie
 
mzee naona anatoka kivingine... hebu ngoja nijifebruary hapa naweza kuula..

Mzee naomba utufikirie sie watoto ambao kwenye koo zetu na vijiji vyetu hatujawahi kupata hata kukanyaga bungeni..wengine hata wabunge wetu ni wakukodisha toka dar salaam... ikifikia uchaguzi wanakuja tu wanachukua ubunge wanarudi dar es salaam... hii imesababisha hata wanafunzi hawaoni umuhimu wakuwa dada au kaka mkuu kwani tunaamini viongozi wanatoka dar tu ... tuko bize kukimbilia dar ... Nahc hata mimi mzee naweza ukinipa kati ya vile viti vyako 9 vilivyobaki... mimi ni ukawa ila nakuahidi sitakuangua... Haki ya nani vile mie nitakuwa mbunge wa wanachama wote...
 
Back
Top Bottom