Kashfa Nyingine nne nzito Zinakuja

Kashfa Nyingine nne nzito Zinakuja

Miltary duty free shop nako ni ka-uchochoro ka kuingiza bidhaa bila ushuru.Pawe na udhibiti wa wazi.Na kuangalia aina ya bidhaa. Haiingii akilini kwa kuingiza juice ya embe isiyo na ushuru wakati zinazalishwa na Bahressa .
au kuingiza sukari huku wakulima wetu hawana pa kuuzia bidhaa zao
 
ndio shida yetu watz kudhani jambpo hili ni la zzk

Sio kwamba ni la Zito ila ndio kiongozi wao,wakishamtoa wengine wataogopa na watakaa kimya kama wabunge wengine walivyo nyamazishwa hawakuongea hata kuhusu escrow ni sisi wananchi kuchukua hatua
 
pAC go go go wala usirudi nyuma wala kuangalia kima yoyote
 
ZITTO+PX.jpg


Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Kabwe Zitto amesema baada ya kukamilisha shughuli ya ufisadi wa Akaunti ya Tegeta Escrow ambayo Sh306 bilioni zilichotwa, kamati yake sasa inaelekeza nguvu katika kashfa nyingine nne.

Zitto alisema kamati yake itatumia mwezi huu na Januari kupitia ripoti nne ambazo zina masilahi kwa Taifa, ikiwamo ya utoaji wa vibali vya kuagiza na kuingiza sukari nchini.

Alisema ufisadi katika utoaji wa vibali hivyo ni mkubwa kuliko sakata la escrow... “Hili linagusa moja kwa moja maisha ya wananchi, wamiliki wa viwanda na uzalishaji. Tayari tumewaita Bodi ya Sukari tujadiliane kwa kina kuhusu suala hili,” alisema.

Mbali na suala la sukari, alizitaja ripoti nyingine kuwa ni ya uchunguzi wa ubinafsishaji wa Benki ya NBC, ripoti maalumu ya Bandari na mikataba ya gesi.

“Baada ya kazi ya PAC, tunapumzika, kwani kama unavyojua kazi ilikuwa ngumu, wiki mbili nilikuwa silali. Kwa kuwa tuna ratiba ya wiki mbili. Kwa Desemba na Januari tutaanza kuzifanyia kazi,” alisema Zitto ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema).

Wiki iliyopita, Bunge lilijadili ripoti ya PAC kuhusu ufisadi katika Akaunti ya Tegeta Escrow na kuhitimishwa kwa kuweka maazimio manane yakiwamo ya kuitaka Serikali iwawajibishe baadhi ya mawaziri na watendaji wengine wakuu huku likitaka pia uchunguzi uendelee kwa wote waliotuhumiwa kupokea fedha hizo kwa njia moja au nyingine.

Kauli ya Zitto inakuja wiki moja baada ya wamiliki wa viwanda vya sukari vya Kagera, Mtibwa na Kilombero kutishia kuvifunga kutokana na kuviendesha kwa hasara.

Wamiliki hao walisema watafunga viwanda hivyo kutokana na Serikali kushindwa kuzuia uagizwaji wa sukari nchini kinyume cha taratibu.

Mkurugenzi wa Viwanda vya Kagera na Mtibwa, Seif Seif alisema uagizaji wa sukari kutoka nje unafanyika kwa ushirikiano wa wafanyabiashara wakubwa na vigogo serikalini kinyume cha makubaliano na hivyo kurudisha nyuma maendeleo ya viwanda.

“Tulikubaliana kwamba Serikali iwe inaagiza tani 100,000 kutoka nje lakini sukari inayoingizwa sokoni ni zaidi ya tani hizo. Sukari tunayozalisha katika viwanda vyetu ipo na haina pa kwenda,” alisema Seif na kuongeza:

“Leo ukipita katika maduka utakutana na sukari ya kila aina, wafanyabiashara wanaoagiza wanawatumia vigogo serikalini kuingiza sukari wapendavyo, tena bila kulipa kodi,” alisema Seif.

Kutokana na hali hiyo, Seif alisema wamelazimika kupunguza wafanyakazi 2,000 na kubakiwa na 5,000 katika Kiwanda cha Kagera, Kilombero imepunguza 3,000 na wamebaki 6,000 huku Mtibwa ikiondoa wafanyakazi 3,000.

“Hali ni mbaya, si kama Watanzania wanavyofikiri. Tukifunga kabisa Watanzania wengi watakosa ajira kama ambavyo mnaona wengine wamekosa, hatuwezi kuendelea kufanya biashara ya hasara ambayo Serikali inaihalalisha,” alisema.

Mwenyekiti wa Bodi ya Kiwanda cha Sukari Kilombero, Balozi Ami Mpungwe alisema: “Hali ni mbaya, tunaona kuliko kuendelea na hali hii ni bora tusimame kuzalisha sukari.

“Serikali kama kweli ina dhamira ya kuvifufua na kuviendeleza viwanda vyetu vya ndani ni lazima kuvilinda na kupiga marufuku uagizwaji holela wa sukari kutoka nje.”


Chanzo: Mwananchi Decemba 2, 2014

Hivi hii kamati ni audit team au?? Kwa nini kazi zao ni postmortem tu??
Living in such a reactive society is really boring.

Man up Zitto and the rest I think you are always missing in action until it is too late... Else tujue kwamba huwa mnaibua haya mambo pale tu mnapokuwa mmekosa mgao?!?
 
Last edited by a moderator:
inasemekana kuna tajiri aliichuza NBC kwa kuchukua mkopo wa mabilioni nbc kisha eti aliwashinda kesi mahakamani na kisha nbc kufilisika na kuuzwa kwa bei ya kutupa kwa africa ya kusini

sasa nawaomba wabunge wanaoitetea nchi hii wamtafute huyo mtu arudishe hizo hela na huyo jaji aliempa ushindi wa mabavu ashitakiwe nawaamini akina zito wafanye kazi hiyo.taarifa zake za huyo alieifirisi nbc zipo takukuru
 
fuatilia vizuri haya masakata
Hivi hii kamati ni audit team au?? Kwa nini kazi zao ni postmortem tu??
Living in such a reactive society is really boring.

Man up Zitto and the rest I think you are always missing in action until it is too late... Else tujue kwamba huwa mnaibua haya mambo pale tu mnapokuwa mmekosa mgao?!?
 
Sasa na hii kamati isilewe sifa ikaingilia biashara, kwasababu ya maslahi ya viwanda nchini bila uchunguzi, biashara ya ushindani inapunguza bei ya bidhaa kwa wananchi, inaleta ushindani wa ubora wa bidhaa na inaingiza kodi, mambo ya kiuchumi tuwaachie wachumi sio wanasiasa.
 
CCM wanahitaji fedha za uchaguzi mwakani na watafanya chochote hata kula nyama za watu ili mradi malengo yao yatimie. Hawatajali hata kama viwanda vyote nchini si vya sukari tu vikifungwa mradi wapate fedha za uchaguzi kwa kuruhusu uingizaji holela wa bidhhaa zisizolipiwa ushuru toka nje. Kinana na Nape wako kimyaa kwa sababu wanajua kinachotokea.
 
Huyo ni bosi wao. Robo tatu ya wabunge wote wa Tanzania wanaripoti kwake.
 
tukimaliza hao tuje kwake na ile kashfa ya 600ml.alizopokelea jerman kwa kaz ya kusambaratisha chama.
 
mchuma janga hula na wa kwao! hivo basi PAC shughulikieni wote mathalani waliohusika moja kwa moja, uzembe, namna moja au nyingine.
 
Aaaah, yamekwisha hayo. Hakuna cha kuwajibika mtu wala nini, maisha yanaendelea Tanzania. Mnalalamikia visenti anavyopewa mtu kwa consultation, sasa angepewa pesa ya kununua SIMIYU?
 
Mmh...hii ya kweli? Haiwezekani akawa mtu mmoja kama ni kweli.
 
Back
Top Bottom