Karl Marx, Adam Smith and Others…!

TPP

JF-Expert Member
Joined
Mar 18, 2023
Posts
650
Reaction score
783
Thread hii ni maalumu katika kuelezea na kutambua mchango wa wanafalsafa mbalimbali wa kiuchumi au kisiasa katika dunia hii ya usasa.

Ruksa member yoyote mwenye uelewa na ufahamu kuhusu mwanafalsafa wa kiuchumi au kisiasa anaye mfahamu kumuelezea humu.

Binafsi yangu nitaanza na hawa wawili maarufu, Karl Marx na Adam Smith

Karl Marx
Huyu ni mwanafalsafa maarufu katika masuala ya uchumi na siasa mchango wake mkubwa binafsi nautambua zaidi katika mageuzi ya kisiasa katika mataifa mbalimbali duniani

Sehemu kubwa alipo fanikiwa zaidi Marx mpaka sasa ni kwenye mageuzi ya kisiasa

Vitabu vyake maarufu duniani ni Das Kapital na The communist manifesto.

Maarufu zaidi ni "The communist manifesto" kilicho andikwa kwa ushirikiano na mwanafalsafa mwenza wa kijerumani Frederick Engels hiki ndicho kitabu kilicho leta mageuzi makubwa sana katika mataifa mbalimbali
Adam Smith
Bwana Smith yeye alikuwa mwanafalsafa na mtaalamu wa masuala ya uchumi, asili yake ni uskotishi.

Bwana Smith mchango wake unatambulika zaidi duniani kupitia mawazo yake kuhusu dhana nzima ya uchumi bora ndani ya kitabu chake maarufu zaidi cha " The Wealth of Nations"

miongoni mwa vitabu vyake maarufu ni pamoja na The Wealth of Nations na The theory of moral sentiments.

Mchango wa Smith katika dunia ya sasa ndani ya mataifa mbalimbali umejikita katika masuala ya uchumi au mageuzi ya kiuchumi katika mataifa mbalimbali duniani.

Smith ni mshindi wa mageuzi ya kiuchumi wakati Marx yeye ni mshindi katika mageuzi ya kisiasa/tawala katika dunia ya usasa.

N.b Taja au muelezee mwanafalsafa yoyote mtaalamu wa masuala ya uchumi au siasa unaye mfahamu sio lazima Marx na Smith.

Ruksa pia kuweka picha, documents, Quotes, machapisho, vitabu n.k kumuhusu huyo mwanafalsafa.
 
I prefer Adam Smith over those two Karl and Hengel
 
Reactions: TPP
Free market economy and Gross domestic product were his concepts -Adam Smith.
Ukipata muda tuletee habari ya Microfinance by Muhammad Yunus.
 
Free market economy and Gross domestic product were his concepts -Adam Smith.
Ukipata muda tuletee habari ya Microfinance by Muhammad Yunus.
Ok
 
Sipendi socialism definetly siwez mpenda karl marx
 
Reactions: TPP
Sipendi socialism definetly siwez mpenda karl marx
At one time Karl Marx supported capitalism when Joint Stock Market or Limited Liability Companies started. He thought that that would be the death of capitalism and imperial rise of socialism but we both know he was wrong.
 
Reactions: TPP
Communism Ni mfumo wa hovyo Sana Sana,Karl nikimkubali itabd nijiombe msamaha
 
Kwa nini ipo hivyo ?
The biggest mistake kwny mifumo ya kijamaa ni kukandamiza haki za binadamu,pia communism inahubiri equality ambayo haipo,ktk mfumo wa kijamaa kiongoz aweza fikiria na kuamua lolote kwa niaba ya raia wengine wote,swali ni je,vp akikosea au kupotoka????communists are the devil's workshop
 
My role model in Economics is Joseph Schumpeter with his theory of Entrepreneurship ( Combining land,labour and capital in production).
But one thing I have noticed is that we in Third world countries most aren't entrepreneurs but petty traders who consider themselves entrepreneurs.
 
Apart from Mr.smith mwengine unaye mfahamu ?
🤔🤔🤔🤔🤔🤔

Just a minute........

Labdq nipekue library yangu,vitabu vyote vinavyohusu ubepari hasa by Ayn Rand na wengineo
 
Reactions: TPP
Hakuna kitu cha kipumbavu kuwahi kufikiriwa kama ujamaa
 
🤔🤔🤔🤔🤔🤔

Just a minute........

Labdq nipekue library yangu,vitabu vyote vinavyohusu ubepari hasa by Ayn Rand na wengineo

N.b Taja au muelezee mwanafalsafa yoyote mtaalamu wa masuala ya uchumi au siasa unaye mfahamu sio lazima Marx na Smith.

Ruksa pia kuweka picha, documents, Quotes, machapisho, vitabu n.k kumuhusu huyo mwanafalsafa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…