Karibu tujadili Ubovu wa Yanga kitaalamu.

Abby Newton

JF-Expert Member
Nov 12, 2017
1,227
2,197
Msimu huu pekee Yanga wamebadilisha makocha zaidi ya 3 lakini timu bado haina matokeo mazuri.Kitendo cha kubadili badili makocha ni dalili tosha kuwa timu ina matatizo ndani ya uwanja.Nimekuwa nikiifuatilia Yanga inapocheza kwa makini sana. Yanga wanatatizo kila idara,na sina hakika km wanajua na wameaamua kukaa kimya tu.

1.Eneo la Makipa.
Hadi sasa haieleweki kipa namba moja wa Yanga ni yupi.Hali hii inasababisha makipa kukosa kujiamini.Kila anaepangwa kuanza anafanya makosa sababu ya kukosa kujiamini. Ni lazima kocha aamue yupi awe kipa namba moja.

2.Eneo la mabeki wa pembeni.
Hapa ndo kunatatizo kubwa la msingi. Mabeki wote wa pembeni hawawezi kupanda kushambuliwa,hawana ubunifu(Skills), passing accuracy yao ni "very poor".Hii inasababisha wapoteze mpira kirahisi sana.

Vilevile hawana uwezo mzuri wa kupiga cross au faulo za pembeni. Kwa mpira wa kisasa mabeki wa pembeni wanakuwa washambuliaji pale timu inaposhambulia. Mabeki wa pembeni wa Yanga wanachofanya ni kimoja tu kuokoa na kupiga mpira mbele ambayo ni staili ya kizamani au kwenye ndondo. Mfano,jana nimemfuatilia Adeyuni dk zote 90 sikumuona amepiga Cross au hata kufanya "Overlap" moja ya maana. Upande kulia dogo anajaribu lakini bado anamengi ya kujifunza kutoka kaka ake Shomari Kapombe.

3.Mabeki wa kati.
Mabeki wa kati wa Yanga hawana utulivu hasa pale wanaposhambuliwa mfululizo.Ni km wanachanganyikiwa. Vilevile hawana uwezo mzuri wa kuanzisha mashumbulizi kutoka eneo la nyuma. Kitu pekee wanachokifanya ni kubutua mpira mbele. Angalia Wawa na Onyango wanavyocheza kwa utulivu hicho ndicho kinachokosekana kwa mabeki wa Yanga. Lamine Moro ni beki machachari lakini si beki wa kiwango hiiiiiicho! Anacheza faulo nyingi na mbaya bila sababu. Sehemu ya kutumia akili yeye anatumia nguvu tu. Jana dhidi KMC km si huruma ya refa kadi nyekundu ingemhusu.

4. Eneo la viungo wa kati
Pamoja na sifa wanazopewa Mukoko na Feitoto,bado kila mmoja anamapungufu yake yanayogharimu timu.Mukoko anakaba sana lakini anapoteza mpira kirahisi sana. Hii inasababisha mipira isifike mbele kwa haraka na kwa wakati.

Kwa upande wa Feisal km kiungo wa mbele anashida ya kasi( speed) hasa pale timu inapoenda kushambulia. Lakini pia anacheza chini sana kitu kinachotengeneza gepu kati ya eneo la kati na eneo la mbele. Yanga wanahitaji kuongeza viungo wabunifu na wanyumbulifu wenye uwezo mzuri wa kumiliki mpira na kupiga pasi maridhawa( Killer pass) eneo la mwisho. Oh

5. Eneo la Ushambuliaji
Hapa ndo kuna janga zito. Takwimu zinaongea zaidi. Wachezaji pekee wa kigeni wenye afadhali ni Ntibazonkiza,Tuisila,na Yaocuba. Wengine waliobaki inabidi wapishe. Najua Carlinhos anajua mpira lakini kwa ligi ya Tanzania inayohitaji nguvu si saizi yake.

Mapufungu eneo la ushambuliaji ni mengi mno ambayo njia pekee ni kusajili wachezaji wenye uwezo kuliko hawa waliopo.

Karibu tujadili Ubovu wa Yanga na nini wafanye kitaalamu kabsa bila mihemko. Nawasilisha.
 
Aina ya ubora wa Wa Yassin Mustapher na Adeyum
Yassin ni mzuri sana kwenye kuzuia ana panda juu na ana rudi fasta kujaza nafasi pindi timu inapo pokonywa mpira....

Tofauti na Adeyum Kurudi ni mzito mmno kitu ambacho hata kwajana ilikuwa ni hatari mmno.

Kiungo kikiwa hovyo Basi Fei Hawezi kufanya kile unacho taka..
Ukiangalia kwa mchezo wa Jana Mukoko ana fanya timu iwe na Balance ila bahati mbaya Yanga haina Box to box midfielder ambaye ni mzuri kwenye ubunifu... unaona jana Ana toka Mukoko Fei ana rudi chini kuwa zuia ila bahati mbaya Shughur ikawa ngumu mpaka alivyo ingia Zawadi mauya kati paka rudi kidogo..

Pale Mbele kwa Jana naona Yocouba na Saido walikuwa vizuri mmnoo ila walikuwa hawana usaidizi lakini tuseme ukweli Molinga ndiye mshambuliaji ambaye alifunga kila aina ya magoli na kwenye nafasi tofauti tofauti... kwa sasa hatuna mshambuliaji kama huyo pale
 
Msimu huu pekee Yanga wamebadilisha makocha zaidi ya 3 lakini timu bado haina matokeo mazuri.Kitendo cha kubadili badili makocha ni dalili tosha kuwa timu ina matatizo ndani ya uwanja.Nimekuwa nikiifuatilia Yanga inapocheza kwa makini sana. Yanga wanatatizo kila idara,na sina hakika km wanajua na wameaamua kukaa kimya tu.

1.Eneo la Makipa.
Hadi sasa haieleweki kipa namba moja wa Yanga ni yupi.Hali hii inasababisha makipa kukosa kujiamini.Kila anaepangwa kuanza anafanya makosa sababu ya kukosa kujiamini. Ni lazima kocha aamue yupi awe kipa namba moja.

2.Eneo la mabeki wa pembeni.
Hapa ndo kunatatizo kubwa la msingi. Mabeki wote wa pembeni hawawezi kupanda kushambuliwa,hawana ubunifu(Skills), passing accuracy yao ni "very poor".Hii inasababisha wapoteze mpira kirahisi sana.

Vilevile hawana uwezo mzuri wa kupiga cross au faulo za pembeni. Kwa mpira wa kisasa mabeki wa pembeni wanakuwa washambuliaji pale timu inaposhambulia. Mabeki wa pembeni wa Yanga wanachofanya ni kimoja tu kuokoa na kupiga mpira mbele ambayo ni staili ya kizamani au kwenye ndondo. Mfano,jana nimemfuatilia Adeyuni dk zote 90 sikumuona amepiga Cross au hata kufanya "Overlap" moja ya maana. Upande kulia dogo anajaribu lakini bado anamengi ya kujifunza kutoka kaka ake Shomari Kapombe.

3.Mabeki wa kati.
Mabeki wa kati wa Yanga hawana utulivu hasa pale wanaposhambuliwa mfululizo.Ni km wanachanganyikiwa. Vilevile hawana uwezo mzuri wa kuanzisha mashumbulizi kutoka eneo la nyuma. Kitu pekee wanachokifanya ni kubutua mpira mbele. Angalia Wawa na Onyango wanavyocheza kwa utulivu hicho ndicho kinachokosekana kwa mabeki wa Yanga. Lamine Moro ni beki machachari lakini si beki wa kiwango hiiiiiicho! Anacheza faulo nyingi na mbaya bila sababu. Sehemu ya kutumia akili yeye anatumia nguvu tu. Jana dhidi KMC km si huruma ya refa kadi nyekundu ingemhusu.

4. Eneo la viungo wa kati
Pamoja na sifa wanazopewa Mukoko na Feitoto,bado kila mmoja anamapungufu yake yanayogharimu timu.Mukoko anakaba sana lakini anapoteza mpira kirahisi sana. Hii inasababisha mipira isifike mbele kwa haraka na kwa wakati.

Kwa upande wa Feisal km kiungo wa mbele anashida ya kasi( speed) hasa pale timu inapoenda kushambulia. Lakini pia anacheza chini sana kitu kinachotengeneza gepu kati ya eneo la kati na eneo la mbele. Yanga wanahitaji kuongeza viungo wabunifu na wanyumbulifu wenye uwezo mzuri wa kumiliki mpira na kupiga pasi maridhawa( Killer pass) eneo la mwisho. Oh

5. Eneo la Ushambuliaji
Hapa ndo kuna janga zito. Takwimu zinaongea zaidi. Wachezaji pekee wa kigeni wenye afadhali ni Ntibazonkiza,Tuisila,na Yaocuba. Wengine waliobaki inabidi wapishe. Najua Carlinhos anajua mpira lakini kwa ligi ya Tanzania inayohitaji nguvu si saizi yake.

Mapufungu eneo la ushambuliaji ni mengi mno ambayo njia pekee ni kusajili wachezaji wenye uwezo kuliko hawa waliopo.

Karibu tujadili Ubovu wa Yanga na nini wafanye kitaalamu kabsa bila mihemko. Nawasilisha.
Ili Yanga ipate mafanikio ni mambo mawili tu.
1) kuondoka uongozi wa Msola
2) timu kupewa mwekezaji mwenye ela na aliyekuwa serious

Mpira ni pesa, mipango na mikakati
 
Nmeangalia marudio, kiukwel Yanga Refa aliwabeba, Lamine Moro ilitakiwa apewe red card mapema, alafu KMC walikuwa wamem target Feisal, wanajua madhaifu yake ya kukaa na mpira, walikuwa wanahakikisha akishika mpira anafanyiwa pressing ya nguvu na wanampokonya kilain, sema refa alikuwa anamlinda sana yan, isingekuwa hivyo lingekuwa balaa!
 
Aina ya ubora wa Wa Yassin Mustapher na Adeyum
Yassin ni mzuri sana kwenye kuzuia ana panda juu na ana rudi fasta kujaza nafasi pindi timu inapo pokonywa mpira....

Tofauti na Adeyum Kurudi ni mzito mmno kitu ambacho hata kwajana ilikuwa ni hatari mmno.

Kiungo kikiwa hovyo Basi Fei Hawezi kufanya kile unacho taka..
Ukiangalia kwa mchezo wa Jana Mukoko ana fanya timu iwe na Balance ila bahati mbaya Yanga haina Box to box midfielder ambaye ni mzuri kwenye ubunifu... unaona jana Ana toka Mukoko Fei ana rudi chini kuwa zuia ila bahati mbaya Shughur ikawa ngumu mpaka alivyo ingia Zawadi mauya kati paka rudi kidogo..

Pale Mbele kwa Jana naona Yocouba na Saido walikuwa vizuri mmnoo ila walikuwa hawana usaidizi lakini tuseme ukweli Molinga ndiye mshambuliaji ambaye alifunga kila aina ya magoli na kwenye nafasi tofauti tofauti... kwa sasa hatuna mshambuliaji kama huyo pale
Kabla ya kumsifia mchezaji yeyote ndani ya Yanga jaribu kumlinganisha na mchezaji wa Simba anayecheza sawa. Km lengo la Yanga ni kuchukua ubingwa basi utaungana nami kuwa Yanga ina wachache sana wenya ubora kuweza kushindania ubingwa na Simba.
 
Yanga inateswa na kivuli cha simba......
Akizidiwa kidogo na simba anatimua team nzima anaanza upya, kamwe hutofika ukiwa una mtindo huo.
Wachezaji lazima wakae pamoja wazoeane.
Hata hii Simba ambayo watu wanasema imetengenezwa kwa mrefu,bado wachezaji wanaoibeba ni wachezaji walioongezwa hivi karibuni. Tukubali tukatae Tatizo la Yanga lipo kwenye ubora.

Mfano ni Morrison alijiunga Yanga na ndani ya mda mfupi ubora wake ukaonekana. Vipi kuhusu akina, Waziri,Zawadi,na Nchimbi mtu mwaka mzima hajafunga goli na anacheza kila siku bado tuseme eti wazoeane? Tusifiche tatizo la msingi kwa kisingizio cha kuzoeana
 
timu lenu bovuuuuu
niliposoma kwamba wawa na onyango ni mabeki bora nikaishia hapo baada ya kukumbuka onyango kupigiza upara chini na kutaka kumdaka miguu T.K master, nkakumbuka wawa alivyo channuliwa miguu kule Sudani nimecheka sana nkafunga na uzi
 
Hata hii Simba ambayo watu wanasema imetengenezwa kwa mrefu,bado wachezaji wanaoibeba ni wachezaji walioongezwa hivi karibuni. Tukubali tukatae Tatizo la Yanga lipo kwenye ubora.

Mfano ni Morrison alijiunga Yanga na ndani ya mda mfupi ubora wake ukaonekana. Vipi kuhusu akina, Waziri,Zawadi,na Nchimbi mtu mwaka mzima hajafunga goli na anacheza kila siku bado tuseme eti wazoeane? Tusifiche tatizo la msingi kwa kisingizio cha kuzoeana
Mkuu ukweli ni kwamba hao wachezaji wanasema wapewe mda ni eidha wameflop au viwango vyao na mentality siyo vya timu kubwa. Huwezi kaa kwenye timu mwaka hubadiliki wala huoneshi dalili alafu umesainiwa miaka 2, viongozi wanakulipa mshahara + bonuses alafu wachambuzi uchwara wanasema wapewe mda, how? Timu imekuleta uipambanie kwenye season target, sasa wewe unapewa time unableach manywele kutwa tu, uwanjan hata kutuliza mpira shida! Wazungu wapo smart sana, hawavumilii kukaa na liabilities, mfano Samatta Aston Villa.
 
Sio kwamba Yanga hawana Timu nzuri...wana timu nzuri ila hawana Kikosi kikubwa chenye kupambana Msimu Mzima...
Kinacho tokea Leo ni matokeo ya kuwa na kikosi kidogo hakuna mbadala .....

Huwezi sema yanga hawana Timu nzuri lakini ukiangalia kwenye Mechi 25 Kapoteza mechi 1...

Kabla ya kumsifia mchezaji yeyote ndani ya Yanga jaribu kumlinganisha na mchezaji wa Simba anayecheza sawa. Km lengo la Yanga ni kuchukua ubingwa basi utaungana nami kuwa Yanga ina wachache sana wenya ubora kuweza kushindania ubingwa na Simba.
 
niliposoma kwamba wawa na onyango ni mabeki bora nikaishia hapo baada ya kukumbuka onyango kupigiza upara chini na kutaka kumdaka miguu T.K master, nkakumbuka wawa alivyo channuliwa miguu kule Sudani nimecheka sana nkafunga na uzi
Mechi ya Juzi kule Misri wawa kampiga mtu mateke kusudi..
 
Back
Top Bottom