Karibu Dodoma, hii ndo Dodoma kwa Ufupi

Karibu Dodoma, hii ndo Dodoma kwa Ufupi

figganigga

Platinum Member
Joined
Oct 17, 2010
Posts
27,638
Reaction score
62,534
Si unakuja Dodoma enhe? Hii ndio Dom kwa ufupi....

1. Hakuna Bahari Dodoma....sahau kuogelea labda Dom hotel...saint Gaspar

2. Hakuna madada poa wengi...waliopo ni very cheap...by the way sio wazuri!

3.Hakuna club Nyingiii Dodoma...zipo Tatu nzuri. Club maisha..club 7...labda na club 84. Nyingine ni club uchwara!

4.Hakuna utumbo na miguu ya kuku kama dar..wale wapenzi Wa mbio za kuku..huku vinatupwa...hapa ni kuku Wa kienyeji Tu..

5.Hakuna wauza soseji kwenye mabar kama dar..Fursa hiyo changamkia.

6. Dodoma kila mdada Wa mjini ukimuuliza ana kazi gani anakwambia anasoma udom. ukimuuliza course gani, tarajia kushangazwa...wengine watakwambia HGL!

7.Dodoma vyakula baada ya SAA tano usiku hupati...chips mwisho SAA NNE!

8.Dodoma ukienda bar wahudumu hawana haraka na Mara zote hawana chenchi. Mteja ukija na mwanamke uchangamfu Wa wahudumu kwako unapungua!

9.Dodoma ukipaki gari usiwe na wasi hata ukiliacha kesho unalikuta halijadokolewa chochote na unaweza pata msaada bila kutoa hela, watu waungwana ukiwaambia asante ...imeisha hiyo!

10. Dodoma wanaume wengi waaminifu na wakarimu kuliko wadada...lakini ukarimu wao unakishindo kikubwa...watch out!

11. Dodoma hakuna super market za ukweli kama za mlimani city, wala hakuna mall hata moja...kuna mini market uchwara...Fursa hii wenye Pesa zenu!

12.Dodoma mjini unaweza kutembea kwa miguu SAA moja umeimaliza...mji mdogo.

13.Dodoma mjini hakuna kusweti ila unaungua na jua na unakuwa mweusi...mwezi Wa sita mpaka Wa saba kuna baridi, ukiamka asubuhi umepauka kama ulikuwa unachezea mchanga!

14.Dodoma vumbi mwaka mzima kasoro January mpaka April...nunua miwani...dodoma usishangae ukivaa open shoes vumbi likafika kisogoni...

15. Dodoma gari lako halitaishiwa Mafuta ..hakuna pa kwenda parefu labda uamue kwenda kongwa, Mpwapwa, kondoa, au chamwino...hakuna foleni.

16.Dodoma hakuna waosha vioo vya magari bila mapatano...Fursa hii kama unaweza! Pia Dodoma hakuna wauza chenchi kama wale Wa mwenge na ubungo mataa.

17. Dodoma bado hakuna wafanya biashara wengi Wa kutumia mitandao kama wasap, instagram etc. Ukifungua business yako na ukatengeneza accounts zako za kuuza vitu online ndani ya dodoma...utapata sana chapa...customers wengi...wanavyuo wengi...
Chuo cha mipango, udom, saint John's univ, cbe, chuo cha madini, na vingine kibao! Fursa hii.

Kama upo Dom na waijua vizuri dom unaweza ongeza sifa za Dom unazozijua....
 
Sawa mkuu lakini naona unaijua Dom juu juu sana.
Ni kweli Dom ni ndogo na unaweza izungukia yote kwa lakini si ndani ya lisaa limoja. Kwa mtu mwenye spidi itamchukua nusu saa kutoka Area C via Iringa-Singida-Moro/Dar-Arusha roundabout kwenda Kikuyu, Kikuyu-Stand 25-30minutes, Stand to Ipagala na hapo hajapiga round kwenda za kupita CDA, 77 Sokoni, Jamhuri, General Hospital, etc.
 
Kweli uliposema dodoma wakarimu sana na chakula nacho saa 4 hakipo ila vumbi ni soo.
 
mhmhmhm kwa ombaomba dodoma ndio kiwandani kwao,mara ya kwanza nilishangaa sana ukiwa hotelini unakula ukienda kunawa mikono ukirudi unakuta ombaomba wamekula msosi wako
Teh teh......hao jamaa ni hatari sana..!
 
Dodoma umeme haukatiki, na maji ni muda wote, hakuna biashara ya maji, yakikatika kwako basi jiandae kulia maana hakuna nyumba utakayouziwa maji, kina mtu na bomba lake labda uswahilini tu.
Dodoma hakuna joto kama Dar
Dodoma huruhusiwi kujenga nyumba bila kibari, nyumba yako itabomolewa fasta!
Dodoma ndani ya robo saa umefika kazini ukitokea eneo lolote la mji kwa daladala au private.
Dodoma majengo yenye lift yako UDOM na mengine hayazidi matano
 
Dodoma kuna kitimoto ya kufa mtu kuna sehemu inaitwa Jacana na pale karibu na bunge,alafu kuna ukumbi mbele ya maisha club jina limenitoka wanapiga nyimbo za kiswahili copy safi saana ila tatizo ikifika saa 5 tu usiku goma linazimwa
 
Dodoma hakuna mrundikano wa gesti kama Sinza au kwa wahaya Mwananyamala.
Ukiwa na hamu zako kama hujahamia na wife wako, jua utapiga nyeto usiku kucha mpaka umchubue Abdala kichwa wazi
 
Back
Top Bottom