Hawakurupuki, wao wanaogopa pesa ya mabeberu isiingie nchini kinyamela. Nchi zinazopata misuko suko huwa kuna donor somewhere anaingiza nguvu ya pesa, wao hapo wamebana. Vyama vya siasa wamepewa mashart magumu kuliko yenu, wao kiasi chochote wanachopewa wanahitaji kuriport serikalini, na balozi zote zimepewa masharti ya jinsi na namna ya kusaidia vyama vya siasa na NGOs, lengo lao ni kuhakikisha hakuna anayepata pesa nje serikali isifahamu, huo ndio udhibiti walioweka. Ubalozi au shirika lolote la nje likitaka kukisaidia chama cha siasa kwanza serikali inapewa taarifa za kiasi na malengo ya msaada, na ndio maana uliona ulifanyika uhakiki wa NGOs zote na kuweka masharti ya kutoa taarifa za mipango kazi yao mara kwa mara serikalini.
Walengwa siyo nyie wananchi wakawaida, nyie mmekumbwa na mtego wa panya. Kulinda madaraka siyo kazi rahisi, lazima yatengenezwe mazingira magumu kwa kila mtu ili ionekane ni kawaida, na siku wakibinywa waseme hii siyo kwao tu bali ni nchi nzima.
Hivyo msimlaumu Dr. Mpango, yeye ni mtekelezaji wa mipango iliyo kwisha ratibiwa serikalini. hata akifahamu hasara ya sera Fulani leo, hawezi kubadirisha kama imeamriwa hivyo. Nyie mnadhani Bashe anaakili sana kuliko Dr.mpango, ni kwasababu mpango hutekeleza mipoango iliyopo hatengenezi sera yeye.