Kanuni mpya za fedha: Dr Mpango

Kanuni mpya za fedha: Dr Mpango

Kusema ukweli hata $10,000 n ndogo kwa wafanyabiashara hata wa level ya kati.
Hiyo pesa ni dogo sana hamna mfanya biashara anae enda nje na mtaji wa $10,000 tu atumie air tiketi $1200 hotel $1000 alipie na usafiri wa mzigo pamoja na kodi.....hapo wanafanya hali kua ngumu Kenya wataendelea kutupiga bao bora nitumie badari ya Kenya na benki za Kenya kuliko za hapa mfanya biashara yoyote hapendi usumbufu tunafukunza wafanya biashara wakati na wakubwa
 
Wachumi sababu ya kufanya hivi mbali kuzuia utakatishaji wa pesa,kina faida kwa uchumi?
 
KANUNI mpya za kudhibiti utakatishaji fedha, zinatarajiwa kubana zaidi wanaofanya miamala kwa njia za kielektroniki ikiwamo benki na simu za mkononi.

Kwa mujibu wa kanuni hizo zilizosainiwa na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango, Mei 7, mwaka huu na kuchapishwa kwa umma Mei 24, zinataka taarifa za mtu anayefanya muamala wa fedha zenye thamani ya Dola za Marekani 10,000 (zaidi ya Sh mil. 20) au zaidi, kutoa taarifa Kitengo cha Kudhibiti Fedha Haramu (FIU).

Kanuni hizo pia zinabana wanaochezesha michezo ya kubahatisha kwa njia mbalimbali ambao nao wanatakiwa kutoa taarifa zao FIU.

Kwa mujibu wa kanuni hizo, kiasi hicho kinachotakiwa kutolewa taarifa ni kile kilichofika thamani hiyo ya fedha kwa muamala uliofanyika kwa wakati mmoja.

Katika kanuni hizo, uhamishaji fedha umetafsiriwa kuwa unajumuisha “shughuli yoyote ya fedha inayohusisha amana, utoaji, kubadilisha, malipo au kupokea fedha kwa shilingi za Tanzania au sarafu yoyote ya kigeni.”

Kanuni ya tano inasema, “mtu anayepaswa kutoa taarifa, atapaswa kutoa taarifa zifuatazo katika Kitengo cha Kudhibiti Fedha Haramu (FIU) (a) ubadilishaji wa fedha zinazohusisha shilingi za Tanzania au sarafu yoyote ya kigeni ambayo thamani yake ni sawa na dola 10,000 za Marekani au zaidi kwa mara moja.

“(b) Kuhamisha fedha kwa mtandao, unaohusisha shilingi za Tanzania au sarafu yoyote ya kigeni sawa na Dola 1,000 za Marekani au zaidi kwa mkupuo.

“(4) Katika kutambua thamani ya fedha za kigeni sawa na Dola za Marekani 10,000 kwa madhumuni ya taarifa ya fedha au dola 1,000 kwa lengo la kutoa taarifa za uhamisho wa fedha za kwa njia ya kielektroniki, muhusika anatakiwa kutumia viwango vilivyowekwa na Benki Kuu ya Tanzania vinavyotumika kwa wakati huo.”

Akizungumzia kanuni hizo, Msemaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Ben Mwaipaja, alisema; “kanuni zinasema mtu yeyote anayefanya muhamala wa fedha kwa njia ya mtandao ama anayesafirisha fedha kwa njia ya mtandao, atoe taarifa kwamba ‘nataka kusafirisha kiasi fulani kwa sababu fulani’.

“Kama unatuma fedha Japan kwa ajili ya kununua gari ama umepokea fedha kutoka nje, au unataka kumtumia mtu fedha zinazofika kiasi kilichotajwa kwenye kanuni, lazima utoe taarifa, hii ni kwa benki ama simu kwa sababu zote hizo ni njia za kielektroniki.

“Utaona dhumuni hapa ni kupambana na fedha haramu ama ndiyo maana ukienda kwenye mambo ya ‘cash’ kuna sheria inabana ipo kwenye viwanja vya ndege na mipaka, kwamba mtu anaweza kusafirisha kiasi gani cha fedha na azitolee taarifa.

“Kwa hiyo inahusu watu wote kama ni nje ama ndani ndiyo maana inasema ndani au nje ya nchi,” alisema.

Alisema kanuni hizo zinabana hata wale wanaochezesha michezo ya kubahatisha ambao kama wanataka kutoa fedha kama zawadi ambazo zinafika kiwango kilichotajwa na kanuni wanatakiwa kutoa taarifa hizo.

“Kwa hiyo hizi kanuni zinakubana kama unataka kutumia njia za kielektroniki kutuma fedha ama kuchukua fedha huko,” alisema.

Kanuni ya 11 inasema miamala miwili au zaidi ikifanywa ndani ya saa 24 na kufikia dola 10,000 za Marekani au zaidi, itachukuliwa kuwa ni muamala mmoja na hivyo itatakiwa kutolewa taarifa.

Kwa mujibu wa kanuni hizo, ripoti za uhamisho wa fedha kielektroniki au ripoti zote za fedha zitapelekwa FIU kabla ya kumalizika kwa siku tano za kazi baada ya siku ya uhamishaji.

“Zitapelekwa kwa njia ya kielektroniki au vinginevyo inavyohitajika na FIU, kila operesheni ya shughuli za michezo ya kubahatisha atahitajika kutoa ripoti ya fedha kwa fedha zilizopatikana kutoka kwa mteja,” inasema sehemu ya kanuni hizo.

Kanuni hizo pia zimeweka adhabu mbalimbali kwa watakaoshindwa kufuata matakwa yake ikiwa ni pamoja na faini na kifungo.

Zinasema FIU au mdhibiti akiridhika kwamba mtoa ripoti ameshindwa kutoa ripoti ya fedha au uhamisho wa fedha zilizohamishwa kielektroniki au kimataifa, kitengo hicho kinaweza kutoa onyo au tahadhari ya kurudia mwenendo uliosababisha kutotii.

Mtu atakayefanya kosa hilo pia anaweza kusimamishwa kufanya shughuli yake ama biashara, kutozwa faini isiyozidi Sh milioni tano na isiyopungua Sh milioni moja kwa siku ambayo kasoro ilijitokeza.

Adhabu nyingine ni kusimamisha leseni ya biashara au kusimamishwa au kuondolewa kutoka ofisi ya mfanyakazi ambaye alisababisha kasoro hiyo.

Kwenye kiwango kuna mahali umeweka 1000$ na kwingine 10,000$, kiwango ni nini?
 
TRUE. We have been there before. Now they are taking us back into the communist world. Communists are dictators. Wanaweza kumfunga mtu kwa majina haya lakini matendo yao yanaonyesha. Wameharibu uchumi. Itafika wakati watakosa hata pesa za kulipa mishahara ya wafanyakazi. Watalazimika kutaifisha nyumba na amana za watu benki ili kuendesha serikali kama alivyofanya Nyerere mwaka 1967. Why are they not learning from history? Kuna nchi gani ya kikomunisti iliyowahi kupata maendeleo ya watu ama vitu?
These people are communists, hawa jamaa ni wakomunisti, na wakomunisti hupenda sana mambo ya control, kwao hii huwahakikishia kuthibiti madaraka lakini at the exponse ya maisha ya kimasikini ya watu huku wao watawala wakiishi katika neema.

Chini ya dr Mpango na serikali hii kiukweli tunapiga U-turn kwa kasi kubwa kurudi katika maisha ya kinyongenyonge ya kuvaa midabwada ambayo tulishaacha.

Hii serikali ya Kikomunisti iambiwe kuwa sera zake za uchumi ni Muflisi itatupa umasikini wa kutisha kwa sera zake za kupenda kuthibitithibiti.

Uchumi siyo siasa, Siasa unaweza kuthibitithibiti na kutokana na watu kuwa busy kutafuta ugali wa watoto wao wakakuacha tu, Lakini ukijifanya kuthibiti thibiti natural flow ya uchumi unavuruga juhudi za watu kupata ugali!. Ikifikia watu wanakosa ugali wao kwa sababu ya sera mbovu hakuna magari ya washawasha yatawarudisha nyuma, hawa jamaa hawajifunzi huko Sudan na nchi nyingine?
 
Jamaa wanaharibu uchumi kisha wanakuja kutupia lawama kwa wazungu kwa kuwaita eti mabeberu, yaani slogan zile zile za enzi za ujamaa wanazirudisha tena
 
Hadi vidola 1000 navyo mnavimaindi, hivi hii.mentality ya kimasikimasikini nani aliwapandikizia hawa watu?

Huwezi kubanabana flow ya pesa hata hizi ndogo ndogo kisha ukadhani unasaidia flow ya mitaji na business kwa watu wa kipato kidogo na cha kati
Unazijua kanuni za India na us wewe?
 
Hadi vidola 1000 navyo mnavimaindi, hivi hii.mentality ya kimasikimasikini nani aliwapandikizia hawa watu?

Huwezi kubanabana flow ya pesa hata hizi ndogo ndogo kisha ukadhani unasaidia flow ya mitaji na business kwa watu wa kipato kidogo na cha kati
Mbona hiyo n kawaida Sana nchi za wenzetu ?kwa watumiaji wazuri was benki wenye transaction kubwa hiyo kitu wanifaham ila Kama unatransaction ndogondogo utaona n kitu kipya

All in all money laundering Ina impact kubwa Sana kwenye uchumi was nchi.Hata hivyo tumechelewa Sana kuja na hi sheria
 
Hivi siku hizi madokta wanapatikanaje kwani?

Hahaha, Umenifanya nicheke kwa sauti
Kuna mtu alisema, "Mpango wa tume ya mipango na Mpango wa Wizara ya fedha na mipango ni watu wawili tofauti"
Lakini ki-ukweli, hizi ni zama tu, nazo zitapita
 
Mbona hiyo n kawaida Sana nchi za wenzetu ?kwa watumiaji wazuri was benki wenye transaction kubwa hiyo kitu wanifaham ila Kama unatransaction ndogondogo utaona n kitu kipya

All in all money laundering Ina impact kubwa Sana kwenye uchumi was nchi.Hata hivyo tumechelewa Sana kuja na hi sheria


Blablabla ndio hizi

Money Laundering ni kuharibu ushahidi wa pesa iliopatikana katika njia zisizo halali sasa mnataka kutuambia watanzania wengi wetu tuna pesa haramu au?

Kama sio wivu wa waliokosa na chuki kwa wenye nacho na usumbufu?
 
Ukiwa mjinga utasapoti kila kitu - hata ujinga. Kanuni za India na US zinasemaje kuhusu miamala ya $1000? US na India unaizona kwenye ramani tu, siyo?
Unazijua kanuni za India na us wewe?
 
Ukiwa mjinga utasapoti kila kitu - hata ujinga. Kanuni za India na US zinasemaje kuhusu miamala ya $1000? US na India unaizona kwenye ramani tu, siyo?
India huwezi kutuma nje ya india dola 1,000 bila ya benki kuu kujulishwa
Tatizo lenu mnauza bucha,vingunguti to manzese muamala umekamilika
 
Hao ndio wasomi wetu bhana hiyo Wizara wamkabidhi Bashe wa Nzega au Halima Mdee watukomboe kwenyd hii deep shit.
 
Unaota wewe. Nani kakwambia India ukituma rupee kiasi kadhaa kwa shangazi yako ambaye yuko hapo hapo India inabidi utoe taarifa kama hii sheria yenu mpya ya kikomunisti inavyotaka? Hata kama una mapenzi na huu ushetani, mambo mengine ni vema kuyanyamazia tu. Nani kakwambia kwamba BOT huwa haijulishwi na mabenki ya biashara kuhusu pesa wanazotuma na kupokea kutoka nje?
India huwezi kutuma nje ya india dola 1,000 bila ya benki kuu kujulishwa
Tatizo lenu mnauza bucha,vingunguti to manzese muamala umekamilika
 
Kwa US$ 1000 kuitolea maelezo ni kusumbuana tuu...

Kwa US$ 10,000 kuzitolea maelezeo tena swala litafanyiwa kazi ndani ya siku tano, ni kuchelewesheana mishahara tuu...

Bank ifanye kazi zote za kupeleka hayo maelezo panapohusika mimi mambo yangu yaendee...

Hapo sasa itakua kama una issue zako juu ya US$10,000 unaanza kuzitoa kidogo kidogo kila siku mpaka tarehe ya jambo lako una US$10,000 mkononi...


Cc: mahondaw
 
Kwa US$ 1000 kuitolea maelezo ni kusumbuana tuu...

Kwa US$ 10,000 kuzitolea maelezeo tena swala litafanyiwa kazi ndani ya siku tano, ni kuchelewesheana mishahara tuu...

Bank ifanye kazi zote za kupeleka hayo maelezo panapohusika mimi mambo yangu yaendee...

Hapo sasa itakua kama una issue zako juu ya US$10,000 unaanza kuzitoa kidogo kidogo kila siku mpaka tarehe ya jambo lako una US$10,000 mkononi...


Cc: mahondaw

Ukiitoa kidogo kidogo wanakata kodi, kwa hiyo utagundua kuwa sababu mojawapo ya kubanabana huenda ni ili walime kodi kwenye miala mingi utakayofanya!
Ndiyo maana hata kwenye ATM wameweka limit ya kutoa laki nne nne ili ukitoa milioni wakate gharama za kodi za miaamala minne!
 
Ukiitoa kidogo kidogo wanakata kodi, kwa hiyo utagundua kuwa sababu mojawapo ya kubanabana huenda ni ili walime kodi kwenye miala mingi utakayofanya!
Ndiyo maana hata kwenye ATM wameweka limit ya kutoa laki nne nne ili ukitoa milioni wakate gharama za kodi za miaamala minne!

Kwa Bank niliyopo mimi chini ya US$ 1,000 unatoa bila kukatwa chochote, juu ya hapo ndiyo wanakata asilimia moja ya kuanzia US$ 1,000 and above...


Cc: mahondaw
 
Safi sana Serikali kwa kuliona ilo, natumaini pia ni njia sahihi ya Watu wanao takatisha Pesa kukomeshwa.

Kuna wengine wananunua Magari ya Fahari wanayajaza Showroom yote hiyo kutakatisha Fedha.

Hii njia ni Bonge la Mwarobaini kwa Serikali yenye juhudi za kuweka Usawa. Pongezi Waziri Dr Mpango heshima kwako.
 
Sijaelewa maana ya hii kitu kwa kweli.
Tayari tunayo sheria na kanuni za antimoney laundering.

Kanuni hizi zinaelekeza kila bank inatakiwa kutoa taarifa ambazo kwa mihala ya aina yoyote ambayo sio ya kawaida inayofanywa na wateja wao "suspicious transactions". Mabank yamepewa nguvu za kutokufanya mihamala hiyo ikibidi. Serikali binafsi imeishatumia mamilion ya pesa kuwa train maafisa wa bank namna ya kutambua mihamala yenye mashaka, Mabank pia yamewekeza pesa nyingi sana kwenye kutrain wafanyakazi wao, yamewekeza kwa kuajiri na kuwalipa mishara mizuri sana wafanyakazi ambao ni mahusi kwa kuangalia mihala hiyo na yamewekeza pesa nyingi sana kwenye teknologia ya utambuzi wa mihala yenye mashaka.

Sasa inamaana hayo yote ni bure? au kanuni hizi zinafanya kazi kwa pamoja?
serikali inauwezo wa kuipitia mihamala yote hii au ndio inataka kuingilia private financial affairs zetu, financial surveillance ya namna hii inatia mashaka na ninaamini imetengenezwa katika misingi ya ujinga wa uongozi.

mtu yeyote anayefikiria anaweza kucontrol kila kitu ni mjinga tu.
 
Back
Top Bottom