Joanah
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 20,880
- 72,534
Lol.Basha wake achukue nafasi.
Mmekumiss pia twin. ππ π
I miss you twin
Sasa hivi tumehamia kwenye daladala, mwendokasi na treni kisa mafuta yamepanda sana bei π€£π€£Tulikubaliana wanaJF wote tuna magari
Hatuwaelewi na hizi story zenu za daladala
Daaa jamanUngemwambia uliambiwa gari zipo zinawasubilia abilia kama nyie, mpe konda au dereva akusaidie kumpakata.
Yan serikali inayotumia kichwa used cha SGR ianze kudeal na daladala,mpe kaisar yalo yakeIfike mahali Waziri mwenye dhamana ya usafirishaji atangaze kuwepo na seat maalumu kwenye kila daladala ambayo siti hizo watakaa wanawake wajawazito, au walemavu, wazee na wenye watoto. mtu mwingine ataruhusiwa kukalia siti hizo ikiwa tu hakuna katika hao. Vinginevyo tunawatesa hawa akina mama wenye watoto kwa sababu wao hawajageuza na gari, ni watanzania wangapi wenye uwezo wa kulipia nauli mara 2 kwa safari moja?
Watanzania tuache roho mbaya jamani, ni kweli umegeuza na gari na umelipia mara mbili lakini isiwe ndio sababu ya kuacha kusaidia wenye matatizo. Hawa watoto tutawafanya wakue na tabia za chuki na roho mbaya kwa sababu ya sisi tuliowafanyia roho mbaya wakati wakiwa wadogo. Mimi afya sio nzuri lakini nikiwa kwenye daladala akaingia mwenye mtoto, au mjamzito au mzee nampisha hata kama nimegeuza. Huwa nafurahi napomsaidia mtu barabarani
Story yako inafanana na nilichotaka kusimulia. Ilikuwa hivyo hivyo, dada kaacha gari kibao zinapakia akasimama kando yangu na mtoto, halafu gari ilipoondoka akaniambia ''Kakaa naomba unisaidie huyu mtoto''. Tofauti na wewe mimi nilimpa makavu na nikamwambia sitaki. Nikamwosha yale magari tuliyoacha nikamwambia kwa nini asipande?Kuwapa tu watu dhambi ndogo ndogo, siku moja yalinikuta nimepanda coaster alafu nyumba kuna kama coaster nne ivi zimepaki zinasubiriana kupakia. Ile niliyopanda ikajaa ikawa inataka kuondoka stand akaja mdada na mwanae mdogo mgongoni akapanda ile coaster akasimama pembeni yangu ilhali anaona kabisa zile zingine zilizokuwa chini pale jirani niliyekaa naye akamwambia mbona utateseka sana na mtoto zile pia zinaenda hajajibu. Mie kimya nikainamia siti kabisa earphone maskioni kidogo ananiamsha dada nisaidie kupakata mtoto nikamwambia mlete mtoto akaanza kilio hataki watu nilimpisha akakaa na mwanae ila alinikera mnoo.
Ni kweli vinakera wengi. Na pia mtu mwenye flu kali, au mtu mchafu kupitiliza ananuka majasho. Bila kusahau hawa vijana malimbukeni wanaobeba vibegi vya mgongoni kama gamba la kobe, huku wanageuka na kugonga navyo abiria wengine.vitu vinavyokosesha utulivu ukiwa ndani ya dala dala.
kukaa seat moja na wachuuzi wa vitunguu,nyama au samaki wabichi.
kuketi ktk seat wakati kuna mama kasimama akiwa kabeba mtoto amekugeukia anakutizama.
konda kubaki na chenji yako.
kukaa na muongeaji wa simu muda mrefu na ananuka mdomo.
dah jaman tuombeane kununua magari aisee,mji mgumu sana huu.
Hahahaha mkuu utaniua kwa kuchekaToka nimpishe mzee tandika akaniibia elf 60 yangu ya ada niliweka mfuko wa nyuma wa suruali,na nimetoka kuomba kwa ndugu maana wazazi walishatangulia mbele ya haki mwaka 2009 hiyo nakaribia kupiga pepa ya form 6, niliapa sitkuja kumpisha kiumbe yoyote kwenye daladala labda mke wangu akiwa na mtoto wangu
Mie niko poa,habari za uzima?Mmekumiss pia twin. π
Ila Umenifanya nicheke mana mie mwenyewe nipo kwenye daladala hapa nimeshikilia bomba. Teh teh π
I hope uko mzima?
Kuwa na adabu hata kama hautaki kumpisha mtu lakini kitendo cha kumuita abiria mwenzako ng'ombe kinaonesha upumbavu wako na kukosa adabu, kuwa memba JF si ujanja.π π mimi sikuhiz sipishi ng'ombe yoyote seat, yaaan labda uwe na mguu mmoja... Mjamzito Mzee Mlemavu wa kawaida tu au Mama mwenye mtoto I don't care utasimama mbele yangu mwanzo wa kituo hadi mwsho wa safar na sipepesi macho pembeni
Kuwa na adabu hata kama hautaki kumpisha mtu lakini kitendo cha kumuita abiria mwenzako ng'ombe kinaonesha upumbavu wako na kukosa adabu, kuwa memba JF si ujanja.
, kupakata mtoto wa mtu kwenye daladala ni mtihani.Nilimpakata mtoto siku moja naenda Chamazi, akasinzia akanikojolea mkojo unanuka kishenzi!
Unapanda daladala na ng'ombe? Wapi huko ng'ombe mnapanda nao daladala?mimi sikuhiz sipishi ng'ombe yoyote seat, yaaan labda uwe na mguu mmoja... Mjamzito Mzee Mlemavu wa kawaida tu au Mama mwenye mtoto I don't care utasimama mbele yangu mwanzo wa kituo hadi mwsho wa safar na sipepesi macho pembeni
Wahuni pia wanazeekaAiseeee, nimecheka ila pole sana