Kanumba kufanya kazi na Ramsey Nouh

nngu007

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
15,862
5,797
kanumb2.jpg


Steven Kanumba

Kwa mujibu wa maombi yake kwa mashabiki wake, sasa Muigizaji Steven Kanumba analazimika kufanya kazi na msanii, Ramsey Nouh kutoka Nigeria.Kanumba kupitia mtandao wake aliwaomba mashabiki wamchagulie staa mmoja wa filamu barani Afrika ili afanye naye kazi na wamemchagulia Ramsey Nouh.

Katika ombi hilo aliorodhesha majina ya wasanii watatu wakubwa kutoka Nigeria na Ghana ambao ni Desmond Elliot, Ramsey Nouh na Van Vicker.Mashabiki wake wengi wamependekeza Ramsey Nouh huku wakimtaka atumie lugha ya kiingereza katika filamu hiyo ili iweze kubamba sehemu kubwa ya bara la Afrika na duniani.

Ombi lake kwenye mtandao lilikuwa kama hivi;

"Kwa mwaka huu nimepanga kufanya kazi na msanii mmojawapo kati ya hawa hapa Desmond Elliot, Ramsey Nouh au Van Vicker,Sasa nakupa nafasi kwa wewe shabiki wangu kunichagulia ni yupi ambaye ungependa kuona nafanya nae movie kwa mwaka huu nami nitatimiza ahadi,

filamu itahusu mambo ya 'secret society' yaani jamii fulani ambayo haiamini Mungu kabisa bali shetani na wamefanikiwa kuiteka dunia kwa 'power',pesa,umaarufu na 'technology' ambao pia wana ishara zao na ibada zao.

Pia amewaomba mashabiki wakae kupendekeza jina la filamu hiyo ambayo anatarajia kuifanya baadae mwaka huu. Bado anakaribisha maoni unaweza kumuandikia kupitia info@kanumba.com This e-mail address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it .
 
Hii imekaaje? Kanumba you should think twice. Otherwise, you should be very strong. Are not these illuminate? Some say that they killed Michael Jackson, 2-Pac and many other celebrities
 
Nadhani Nigeria wamekuwa na filamu zinazokaribiana na hii proposal ya kanumba kama Billionaires Club na Coming of the Anti-Christ. Napata shida sana juu ya filamu zetu na za Nigeria kwa kuwa hata Ramsey hana jipya kama alivyo Desmond Elliot, huyo mwingine simfahamu. Labda nizidiwe na "kelele za uzalendo" lakini vinginevyo sioni jipya. Kanumba alikwisha igiza na Wanigeria, sinema haikuwa interactive, sehemu ambayo wangehitaji majibizano kuingiliana walikuwa wanaacha gaps na walikuwa slow kwa sababu ya kukariri skript ya Kiingereza. Mzee Hammie Rajab amekuwa akilaumu waigizaji wakubwa kutotaka kujifunza Kiingereza.

Siwapendi waNigeria kwa kuwa wana-over-act, wanafoka sana, wanaigiza upole kupindukia au uchekibobu wa kupindukia. Najitahidi sana kutazama sinema za Nigeria lakini naona bado makosa ya kiufundi ni makubwa sana. Btw nilipata kupenda sinema za mNigeria Richard Moffe "The Price" na "Suicide Mission."

Sinema ya kwanza ya SciFi ya Nigeria "Kajola" (Starring Desmond Elliot) ilisababisha watu wadai kiingilio chao kirudishwe! In short ni "wanazi" tu ndiyo hutetea kuwa tunaziponda sinema zetu. Niko tayari kujitetea kwa hoja (technically) na mifano.
 
Hii imekaaje? Kanumba you should think twice. Otherwise, you should be very strong. Are not these illuminate? Some say that they killed Michael Jackson, 2-Pac and many other celebrities

Hizi ni hisia tu, Illuminates na Masons hawana muda wa kudeal na sinema hizi. Mambo mengi kuwahusu hawa watu ni Conspiracy theories tu. Kwa wafuatiliiaji afya ya Michael Jackson na matatizo yake ya ki-sosholojia na kisaikolojia yanafahamika. Mi nisingeshangaa kupata habari kuwa Michael J alikuwa anatumia madawa ya usingizi au kupunguza maumivu kwa sababu maisha yake yanafahamika. Kuna wakati alikuwa anataka kujiua kwa umeme, kuna wakati alihamia Arabuni, amekufa akiwa na msimamo wa Uislam (si jambo baya), kashfa, uchumi, nduguze (Letoya/Latoya), baba etc.

Ugomvi wa Tupac na akina Big nao unafahamika.
 
Hizi ni hisia tu, Illuminates na Masons hawana muda wa kudeal na sinema hizi. Mambo mengi kuwahusu hawa watu ni Conspiracy theories tu. Kwa wafuatiliiaji afya ya Michael Jackson na matatizo yake ya ki-sosholojia na kisaikolojia yanafahamika. Mi nisingeshangaa kupata habari kuwa Michael J alikuwa anatumia madawa ya usingizi au kupunguza maumivu kwa sababu maisha yake yanafahamika. Kuna wakati alikuwa anataka kujiua kwa umeme, kuna wakati alihamia Arabuni, amekufa akiwa na msimamo wa Uislam (si jambo baya), kashfa, uchumi, nduguze (Letoya/Latoya), baba etc.

Ugomvi wa Tupac na akina Big nao unafahamika.
Mkuu! Inakuwaje unaamini kuwepo kwa hawa jamaa na wakati huohuo unasema ni hisia tu. Pia unasema hawana muda wa kudeal na sinema hizi. Je, unajua shetani anavyofanya kazi? Je shetani hawezi ingia katika kazi ya mtu MKUBWA kama Kanumba ambaye kwa kiwango kikubwa ana-influence maisha ya watu wengi hasa vijana? Kwa taarifa yako: lengo la hawa jamaa ni kutawala kila kitu kinachomhusu mwanadamu duniani kote. Na mara nyingi wanatumia, media, music industry, na filamu...vitu hivi vinawalenga sana vijana ambao kimsingi ni impressionable. Endelea kuamini unachokiamini !!!!!
 
Back
Top Bottom