Kirumberumbe
JF-Expert Member
- Mar 28, 2017
- 982
- 1,187
Ninavyo fahamu na ndivyo ilivyo, kila Parokia ina mipaka yake au tuseme Eneo lake kiutawala/kiutendaji. Paroko na wasaidizi wake wanatakiwa watoe huduma za kiroho ndani ya Eneo lao na si vinginevyo. Utoaji wa huduma una gharama zake ambazo Waumini wa Eneo hilo ndio wanatakiwa kuzichangia. Kusali ni mahali popote kwa raha zako; lakini ujue kwamba inapokuja ni suala la Huduma za Kiroho utakazohitaji zitatolewa na Parokia yako husika. Vinginevyo Huduma za kiroho unaweza kuzipata kutoka Parokia nyingine kwa kibali cha Maandishi kutoka Parokiani kwako. Hili lipo hivyo ili kuepusha migongano, migogoro, vurugu na hata uvunjifu wa Taratibu za Kikanisa hususan kwa wale Waumini au hata Maparoko wakorofi wasiozingatia Taratibu zilizowekwa na Kanisa Mahalia.Baba paroko wa parokia ya roho mtakatifu Kitunda kwa nini anakuwa na kigugumizi cha kutangaza Jumuiya zilizohamishwa kutoka parokia Yake kwenda Parokia ya Kipunguni - Akwino.
Kwanini bado hatangazi ili hali taarifa anazo haoni kama waamini anawagawa.
Kanisa katoliki linamsimamo lazima aheshimu maamuzi ya Askofu kugawa mipaka haiwezekani watu watembee km 4 kwenda kusali ili hali kuna Parokia ipo karibu km haifiki.
Baba Askofu amuangalie sana Huyu paroko amekaa hapo muda mrefu ametengeneza himaya yake. Kitu ambacho sio kizuri kwa kanisa.
Haiwezekani tumehamishwa kwenda parokia nyingine lakini viongozi wanadai michango ya parokia nyingine ambayo tumeshahama hili ni tatizo na linaleta mgawanyo ndani ya Jumuiya.
Nawasilisha.