ukisoma habari hii kwa makini unaweza kujiuliza mara moja tu kuwa nia ya mwandishi ni kuonyesha kwamba kanisa katoriki halikumtaka Hilary kwa sababu ni mwislamu kuwa mbunge wa sumbawanga lakini pia kanisa halikumtaka mgombea wa CCM lilimtaka wa Chadema.
ukizama ndani zaidi, unabaini ukweli kwamba mtafaruku ulianza wakati wa kampeni ambapo taarifa ya mwandishi inadai Hilary ambaye ni mwislamu aliukufuru utatu mtakatifu wakati wa kampeni alipojifananisha na Yesu kristo kwa kueleza dhana ya mafiga matatu yaani kuchagua Rais, mbunge na diwani wa CCM.
Mpaka hapo unabaini kwamba, tatizo hapo sio CCM wala Uislamu wa mbunge bali kauli zake wakati wa kampeni kuhusu utatu mtakatifu. Mimi nafikiri kwamba baada ya kauli hiyo ya kufuru kanisa katoriki parokia ya sumbawanga liliweka msimamo wa kutomuunga mkono mtu aliyekashifu utatu mtakatifu au ukristo kwa ujumla sio kwa uCCM wake au Uislamu wake bali kwa kauli zake. Msimamo huu wa kanisa ukageuka kuwa imani ya parokia hiyo na wale waliosaliti imani hiyo wakaadhibiwa kwa kumuunga mkono aliyekufuru utatu mtakatifu jambo ambalo katika dini zote linaweza kutokea kuwapa adhabu wanaokufuru dini.
Nashauri kwamba, badala ya mwandishi kulikuza suala hili na kulipa sura au picha ya kanisa kupinga mwislamu kuwa mbunge au mgombea wa CCM angetusaidia kumuulliza mgombea, na waathirika wa kadhia hii kama ni kweli walikashifu/ walikufuruku utatu mtakatifu na pengine hawakutaka kukili kosa hilo mapema kwa kuomba radhi ili yaishe.
kama huu ungekuwa ndio msimamo wa kanisa katoriki nchi nzima dhidi ya Uislamu au CCM migogoro kama hii ingesikika mahali pengine nchini na sio sumbawanga pekee kwani kuna wakatoriki wengi tu walikipigia kura chama cha CCM lakini bado ni wakatoriki na hakuna aliyewahoji kwa hilo... nini kimejiri huko sumbawanga? Tuambiwe ukweli.
Je waliotengwa walikwenda kufanya nini kwenye ibada ya mazishi kama sio uchokozi uliwahi kuona lini kafri akaruhusiwa kuingia msikitini? hawa wametengwa na kuondolewa ukatoriki wao na mvutano ndio kwanza unaanza hakuna suluhu ni nini kiliwatuma huko? walipoambiwa waondoke kupisha ibada ya mazishi wangekuwa waungwana kutoka nje kwa amani ili padri afanya kazi yake.