Kaniacha kisa jana nimelala lock up.

kyanyangwe

JF-Expert Member
Joined
Oct 31, 2018
Posts
1,501
Reaction score
4,282
Wakuu

Chemistry ya wanawake inanishangaza sana.

Well saivi me ni jobless tu niko kitaa naunga unga maisha baada ya kuzinguana na aliyekua mwajiri wangu.
Sasa jana mtaani kwetu sikujua kama kulikua na operation ya police kukamata wazururaji na watu wanaokunywa pombe muda wa kazi.

Me kwenye saa 7 hivi mchana nikawa bar flani napiga safari lager zangu.mara nikaona raia wanatoka nduki sijakaa sawa police hao wakaniweka chini ya ulinzi tukafungwa mashati tukapakizwa kwenye cruza yao mpaka kituo cha police golani tukapewa mashtaka ya uzembe na uzururaji tukapigwa lock up.nikampigia the so called baby wangu aje anitoe au aniletee msosi akapotezea akasema nitajijua mwenyewe huko.

Basi asubuhi ya leo nikawacheck washkaji zangu flani wakaja pale wakanitoa lockup.

Mwanamke kasikia nimetoka ndani kanitumia ujumbe kuwa mimi na yeye basi hanitaki tena eti namtia aibu.
Ni sahihi wakuu?
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…