Kaniacha bila sababu, moyo unaniuma

Kaniacha bila sababu, moyo unaniuma

mkuu fuata ushauri uliopewa na mimi naongezea kuwa bora pengo kuliko jino bovu...achana nae na kamwe usije kulamba matapishi yako kwa maana najua tu kuna mtu kamshikia akili na ninaamini atarudi mrudiane...acha kabisa kama uwezo unakuruhusu tafuta binti aliyetulia uoe.
 
pole sana kijana Tafuta pesa kwanza kwa bidii,
mapenzi utapata, muache aende akikutana na vijana wa mujini atakukumbuka😀😀
 
""Nikaenda kwa mama yake akasema nimvumilie kwa kuwa bado hajakuwa kiakili nikavumilia nikampa onyo akajirekebisha wiki mbili tu baada ya hapo karudia tena tabia ile ile ya kuto nisikiliza anataka asikilizwe yeye tu nikimshauri jambo anajifanya mjuaji sana, kiburi nje nje.""


Huyo mzazi wake anamtetea mwanae anasema mwanae hajakua kiakili but mi nasema mwanae amekuwa kivitendoo, ndo mana anasema hivyoo, but usijaribu kwa mzazi wake Fanya uchunguzi hata kwa Rafiki zake, usijekuta ashapewa maneno tiale
 
Huyo bado hajajua thamani yako kwake, muache ndo atajifunza
 
Ndugu zangu wanajamvi habari za asubuhi.

Nimekuja hapa kuandika uzi huu nikiomba ushauri nikihitaji faraja kutoka kwenu.

Mimi ni kijana miaka 25, mwenzangu huyu 21, nimemaliza chuo miaka miwili iliyopita, mwenzangu kaishia form 4. Tumekuwa kwenye mahusiano karibu mwaka na nusu. Niseme kweli nilimpenda sana na yeye alinipenda. Nilijitolea sana kwa hali na mali kwa moyo wote kumsaidia katika maisha yake nilimpenda kwa moyo wote. Hali ilibadilika miezi kadhaa tangu tuingie kwenye mahusiano.

Mwenzangu akabadilika ghafla kaanza kunifanyia vituko majibu machafu nikimkosea tena kosa dogo laki binadamu, mwenzangu anachukulia nimefanya makusudi anakuwa mkali ugomvi hauishi wiki nzima. SMS akawa hajibu hata calls zangu hapokei.

Nikachunguza mabadiliko haya nikagundua mitandao ya kijamii ndio imemponza. Nikasema ngoja nipunguze mapenzi. Akajirudi akawa mpole akawa anasema ananipenda. Nikarudisha tena mapenz tena kwake baada ya muda akarudia ile tabia majibu machafu kiburi cha wazi wazi.

Nikaenda kwa mama yake akasema nimvumilie kwa kuwa bado hajakuwa kiakili nikavumilia nikampa onyo akajirekebisha wiki mbili tu baada ya hapo karudia tena tabia ile ile ya kuto nisikiliza anataka asikilizwe yeye tu nikimshauri jambo anajifanya mjuaji sana, kiburi nje nje.

Mimi sikuwahi msaliti na despite ya vituko anavyo nifanyia nilizidi kumwonyesha upendo, mimi nilimlipa kwa mema sijawahi kulipiza kisasi kwake, mpaka ndugu zake walikuwa wakisifia upendo wangu kwake. Lakini mwenzangu alikuwa haoni hilo.

Kila tulipo kosana alitaka tuachane hata kama kosa ni dogo anataka tuachane. Nikikubali anakaa week 1 moja anaomba msamaha na kuahidi kubadilika lakini baada ya hapo tena anarudi madudu.

Jana usiku nilimpigia simu kumsalimia kumjulia hali akakata simu, nikamtumia SMS hajajibu. Nilipompigia mara ya pili akapokea nikamuuliza kwanini anafanya hivyo akasema hajisikii kuwa na mimi nikamuuliza kwanini, ni kosa gani nimekutenda akasema hakuna ila hajisikii tu na ananitakia maisha mema na mahusiano yaishe.

Sasa wadau sijamtenda baya lolote lakini yeye kaamua hivinifanyaje?

Naomben ushauri?
Nitausema ukweli utakuuma kijana mwenzangu/Mdogo wangu ni hivii elewa Huyo binti anajihusisha kimapenzi na mwanaume mwingine ,binti anampenda jamaa ila jamaa hampendi binti hizo turn around unazoziona ni pale anapozinguliwa na jamaa ,inabidi aje kupoza kwako believe me atarudi kuja kuomba msamaha tena kwako.
Nini cha kufanya sasa kama gentleman jikite kwenye vitu vya msingi katika maisha yako haswa masuala ya kiuchumi let her go, usikumbatie kaa la moto hata ukilazimisha hatokufaa maishani kwako , atakusumbua ukilazimisha kumuoa huwezi kuendelea kuishikilia kamba inayovutwa na gari/ng'ombe kisa tu kung'ang'ania kuiweka kwenye uelekeo unataka wakati kamba inakuumiza mikono yako.
 
kifupi wewe una mbembeleza mtafutie time kwanza na wewe akipiga usipoke mda mwingine mpe adhabu kama mwezi hivi then utaona wewe una muogopa kumpoteza una onyesha mi wangu alikuwa hivyo ni simple saizi kimya kajielewa
hiyo kitu ngumu sana kupractice kwa mtu anayempenda kama huyo mshikaji mtafanya awe anaangalia WhatsApp kila dk kuona kama demu yuko online au offline na akimuona roho inauma sana. Kupenda kubaya sana huyo jamaa sasa hivi ni kama anaumwa ila ndio hivyo hamna namna. Tatizo la demu wake ni kwamba ana jamaa mwingine na pia umri wake ni mdogo hivyo hajielewi
 
Mkuu wanawake wengi huwa wanajisahau sana wanapopendwa tena wakiwa na uhakika wa kutoachwa. Huwa wanadharau na kiburi sana si anajua huwezi kumuacha. Tena kibaya umeshaonesha udhaifu, hata akikuudhi unamsamehe.
Hapo lazima akusumbue tu. Mkuu kwa usalama wa afya yako usije kuthubutu kumuoa huyu mwanamke. Utajuta
 
HV kama hali hiyo inakutokea kwa MTU umeshamlipia mahari; unatakiwa ufanyeje
 
hiyo kitu ngumu sana kupractice kwa mtu anayempenda kama huyo mshikaji mtafanya awe anaangalia WhatsApp kila dk kuona kama demu yuko online au offline na akimuona roho inauma sana. Kupenda kubaya sana huyo jamaa sasa hivi ni kama anaumwa ila ndio hivyo hamna namna. Tatizo la demu wake ni kwamba ana jamaa mwingine na pia umri wake ni mdogo hivyo hajielewi
Hawa wanawake wa miaka 21 wengi wana matatizo sana. Wanachangamoto sana. Ukitaka kuoa angalia mwanamke mweny umri angalau 24 hiv
Hatari sana halafu huyu mwanamke baada ya miaka kadhaa atasema wanaume walaghai na hawana mapenzi ya dhati.
Wanawake wapo wa aina 2
1. Wife material
2. Sex material
inategemea unakutana na nani
 
Unachotakiwa kufanya ni kushukuru kwamba hamkufikia hatua ya kufunga pingu za maisha ukajua tabia zake.
 
Bora alivyokuambia ukweli kuliko aendelee kukupotezea muda.
Hata hivo vituko anafanya ili umuache lakini kwakuwa unampenda unavumilia na muda mwingine yawezekana anakuonea huruma ndo mana anakuomba msamaha.
Anakwambia hajisikii kuwa na wewe lakini kunasababu zinazomfanya awe hivo ila tu hataki au hawezi kukwambia kwakua utajisikia vibaya sana.
Muache afanye anavyotaka na wewe kuwa bizzy na shughyli zako wala usimtafute.
Akili zikimrudia atakutafuta wakati huo keshachelewa na wewe umemove on.
 
[QUOTi11, post: 17991085, member: 201241"]Unachotakiwa kufanya ni kushukuru kwamba hamkufikia hatua ya kufunga pingu za maisha ukajua tabia zake.[/QUOTE]
Mkuu sasa mtu huyo anavunjaje uchumba; na mahari ashalipa
 
kuacha au kuachwa ni jambo la kawaida sana katika huo umri wenu, take it easy bado unasafar ndefu ya kujionea mengi zaid ya hayo mdogo wangu
 
kukosa sababu na yenyewe ni sababu pia. Chapa lapa mdogo wangu.
 
Back
Top Bottom