M-mbabe
JF-Expert Member
- Oct 29, 2009
- 13,203
- 23,020
tumekusikia Emmanuel Mbasha.Ndugu zangu katika kristo nawaslimu Sana!
Ni Takribani wiki mbili tangu kutokea kuvuja kwa Video ya ngono iliyomuhusisha askofu mkuu wa makanisa ya ufufuo na Uzima ndugu Josephati Gwajima,sote tunakumbuka nnchii ilijaa taharuki kubwa baada ya video hii ikimuhusisha moja kwa moja mtumishi wa kiroho.
Kwa Tanzania Matukio kama haya yamekuwa ni kawaida lakini mara nyingi yamekuwa yakihusisha wasani mfano Wema Sepetu,Diamond,Nandy, Amber Ruty pamoja na mume wake, wote hawa walichukuliwa hatua kali na wengine mpaka leo bado wapo na kesi mahakamani,lakini kwa viongozi wakiroho imekuwa ni mara ya kwanza kuvuja kwa Video ya namna hii tena ikimuhusisha Askofu mkuu wa makanisa ya ufufuo na uzima,lakini pia vile vile sio mara ya kwanza Kwa kiongozi huyu wakiroho kuhusishwa na matukio ya uzinzi utambuka alishawahi kuhusishwa na tukio la uzinzi lililo muhusisha aliyekuwa mke wa Emanueli Mbasha(Flora Mbasha).
Tukio la uzinzi wa Gwajima nimezimwa katika hali yakumdhihaki Mwenyezi Mungu,Mimi Kessy Augustino natambua Hatari itakayonikabili mara baada yakwenda kinyume na Jeshi la polisi,kinyume na waziri wa mambo ya ndani,kinyume na askofu Kakobe na waumini wote wa makanisa ya ufufuo na uzima wanaomdhihaki Mungu kwakuudanganya Ulimwengu na kuudharaulisha ukristo ,kuuaminisha umma kuwa video ile imetengenzwa huenda nikawindwa au hata kuangamizwa kwa kuusema ukweli,huenda maisha yangu yatakuwa hatarini lakini naamini Mungu aliyewalinda Danieli,meshaki na Aberinego Atanilinda pia wote tuseme AMEEN KUBWA.
KWANINI TUNASEMA VIDEO HAIJATENGENEZWA
Ndugu zangu katika karne hii ya 21 bado haijawezekana kuedit video kama ambavyo tunaaminishwa na watetezi wa Gwajima.Mimi natoa changamoto, ile video kama imeeditiwa bhasi tuletewe original yake na kama hilo litashindikana bhasi wamuedit mtu mwingine kwenye hiyo hiyo video, hilo likiwezekana bhasi nitaomba waumini wa kanisa la ufufuo na uzima wanipige mawe hadharani mpaka nifariki dunia kama hilo pia likiwa gumu bhasi nitaomba nipigwe risasi hadharani.
UTETEZI WA KAKOBE NI DHIHAKA KWA MUNGU
Mtumishi wa Mungu kakobe wewe ni mtu mzima sana tena uliyedumu katika huduma kwa muda mrefu ni majuzi tu umetimiza miaka 30 yahuduma sikutegemea kabisa kama ungeweza kujihusisha na sakata hili zito,lakini umekuwa kiongozi wa kwanza kujitokeza hadharani kumtetea Gwajima naniwazi pia na wewe ulitizama video ile chafu ushaidi uliotupa umedhihirisha na wewe ulitenga muda kutizama Porno,kakobe alisikika akisema video ile ni feki kwakuwa binti hakuwa anaonekana!!Ndugu zangu utetezi huu ni batili ina maana leo hii ikarushwa muendelezo wa video binti akiwa anaonekana bhasi video itakuwa sahihi je unataka watanzania wafanye hivyo???Mchungaji kakobe kutumia madhabahu kutetea dhambi umemdhahaki Mungu unapaswa kutubu,pamoja na nayo tumsamehe mchungaji Kakobe umri umeshamtupa na technologia pia imemtupa mkono ni rahisi kuamini video ile imetengenezwa.
UTETEZI WA GWAJIMA DHIDI YA VIDEO YAKE YA NGONO NI KUUCHAFUA UKRISTO.
Sote tuliona na kusikia utetezi wa askofu Gwajima dhidi ya video yake chafu alisikika akisema anayeonekana kwenye video ni Baunsa na sio yeye,kwa akili za kawaida kauli hiyo haina ukweli wowote ubaunsa wa kwenye video ameuonaje wakati video inawaonyesha upande mmoja wa mtu ubavuni??kwanini askofu unatuona watanzania wajinga kiasi hichi lakini???Vilevile alituahidi siku ya Jumapili ungekuja Na ushahidi wakutosha dhidi ya mhusika aliyepanga mpango huo wakumchafua lakini jumapili akaishia kumualika kakobe asafishe dhambi yake, kama kweli haikuwa wewe Tulitegemea kuona vidhibitisho vyakutosha sana kama ambavyo alifanya kwa makonda kuwa ni kweli alipata zero,lakini tukio hili kubwa umeshindwa kabisa kabisa kujitetea .Kwanini Gwajima anataumia madhabau kusema uongo,Gwajima najua ukweli unaufahamu ilikuwa ni hekima nyingi kunyamaza au kukiri kosa nakuomba msamaha kwani wewe sio wa kwanza kufanya hicho kitendo,kusema uongo kupotosha umma kwakumchafua Kristo haikubaliki hata kidogo.
UTETEZI WA POLISI NI DHARAU KWA SERIKALI NA UBAGUZI KWA WATANZANIA
Tumeona jeshi la polisi lilikuwa kali kwa watangulizi wa Gwajima waliovujisha video chafu,wote tumemuona Wema Sepetu tabu alizopitia mara baada ya video yake akimkis(busu) mpenz wake hadharani kuvuja, alifunguliwa kesi na hadi leo bado inanguruma mahakamani,Kwa upande waGwajima imekuwa tofauti kabisa ingawaje kosa lake ni kubwa zaidi ila jeshi la polisi limekuwa upande wake?? kwanini jeshi la polisi litetee maovu kwanini isitende haki na kusimamia ukweli???Kwa utetezi huu jeshi la polisi imeidharau serikali inayosimamia na kutekeleza sheria zilizotungwa na Bunge letu tukufu,jeshi la polisi linakila sababu kuomba radhi kwa waTanzania
Napenda kutoa pongezi kwa taasisi zote za dini ikiwemo Roman katoliki,Waislamu pamoja na kanisa lakiludheri lakiinjili Tanznia(KKKT) Kwa kukaa kimya bila kutoa ufafanuzi wowote unaohusu video chafu ya Gwajima ukimya huu uliambatana na maombi makali yakumtaka Askofu Gwajima atubu dhambi hiyo na sio kuendelea kupotosha jamii,wamefanya busara kubwa kwani ukweli wanaujua na Hawakutaka kufanya dhihaka kwa Mungu muumba mbingu na nnchi,baada yakusema hayo naomba kwa heshima kubwa sote kwa pamoja Tumuombee Toba Askofu Gawajima na Mungu Awabariki sana.
Brazado,
Arusha.