Elitwege
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 5,154
- 10,809
Nenda Lugola nenda Lugola, sisi wanyonge tunakulilia.
Siku zote nabii hakubaliki kwao na ukitaka kuchukiwa sana basi simamia haki, Lugola alikuwa ni moja ya mawaziri makini waliosimamia haki Wizara ya Mambo ya Ndani.
Siri ya Lugola kuchukiwa na askari hadi kufikia hatua ya kushangilia alipotumbuliwa hizi hapa.
1. Kangi Lugola alikuwa waziri wa kwanza wa mambo ya ndani kufyeka kichaka cha rushwa kwenye magari ,ikumbukwe kabla ya Lugola kila kosa kwenye gari lilikuwa linatozwa shs 30,000!
Yaani gari haina indicator elfu 30
Gari halina rangi elfu 30
Tairi imeenda upande elfu 30
Yaani trafiki alikuwa na uwezo wa kukusome makosa 10x30,000 =300,000 hiyo anaondoka nayo asubuhi asubuhi tu!
Lugola aliamuru makosa yote hayo yako chini ya kosa moja tu la ubovu wa gari na mwenye gari anatakiwa alipe elfu 30 tu badala ya laki 3! Kwa hali hii askari wala rushwa (Chadema) watampenda Lugola?
2. Kabla ya Lugola ilikuwa ukiwekwa mahabusu weekend hutoki kwa sababu hamna dhamana, lakini waziri huyu shujaa alikuja kuamuru dhamana zitolewe hadi siku ya Jumapili!
Je kwa hali hii Polisi watapenda?
3. Ni Waziri shujaa Kangi Lugola aliamuru bodaboda zote ziondolewe kwenye vituo vya Polisi. Kumbukeni bodaboda zilikuwa zinarudikwa kwenye vituo vya polisi hadi kituo chenyewe kinakuwa hakionekani. Lengo la kitendo hiki ni kutengeneza mazingira ya rushwa na ufisadi ili askari wapige dili.
Kwa hali hii wanyonge watamchukia Lugola?
4. Kabla ya Lugola mabasi ilikuwa ni marufuku kuendelea na safari baada ya saa sita usiku. Hali hii ilileta usumbufu na gharama kubwa kwa abiria na kwenda kinyume na Sera ya viwanda na uchumi wa kati.
Lugola alifyeka kichaka hiki kwa kuwaambia askari wakae sawa magari yatembee usiku kucha na wananchi hawawezi kupangiwa muda wa kusafiri na majambazi.
Kwa hili wanyonge watamchukia Lugola?
5. Chini ya Waziri Lugola matukio ya utekaji, mauaji na ujambazi yalipungua sana nchini. Wote ni mashahidi wa hili muda wote mabasi yamesafiri usiku kucha hamna basi hata moja lililotekwa.
Kwa hili wanyonge watamchukia Lugola?
Nenda Lugola ila huenda kilichokuponza pia ni kuwa upande wa maslahi ya wananchi sana na kupuuza kulea rushwa za maaskari tulizozizoea tangu uhuru, lakini wahenga walisema tenda wema uende zako usingoje shukrani ila uwe na hakika Lugola siku ya kiama utavishwa taji na wanyonge.
Sent using Jamii Forums mobile app
Siku zote nabii hakubaliki kwao na ukitaka kuchukiwa sana basi simamia haki, Lugola alikuwa ni moja ya mawaziri makini waliosimamia haki Wizara ya Mambo ya Ndani.
Siri ya Lugola kuchukiwa na askari hadi kufikia hatua ya kushangilia alipotumbuliwa hizi hapa.
1. Kangi Lugola alikuwa waziri wa kwanza wa mambo ya ndani kufyeka kichaka cha rushwa kwenye magari ,ikumbukwe kabla ya Lugola kila kosa kwenye gari lilikuwa linatozwa shs 30,000!
Yaani gari haina indicator elfu 30
Gari halina rangi elfu 30
Tairi imeenda upande elfu 30
Yaani trafiki alikuwa na uwezo wa kukusome makosa 10x30,000 =300,000 hiyo anaondoka nayo asubuhi asubuhi tu!
Lugola aliamuru makosa yote hayo yako chini ya kosa moja tu la ubovu wa gari na mwenye gari anatakiwa alipe elfu 30 tu badala ya laki 3! Kwa hali hii askari wala rushwa (Chadema) watampenda Lugola?
2. Kabla ya Lugola ilikuwa ukiwekwa mahabusu weekend hutoki kwa sababu hamna dhamana, lakini waziri huyu shujaa alikuja kuamuru dhamana zitolewe hadi siku ya Jumapili!
Je kwa hali hii Polisi watapenda?
3. Ni Waziri shujaa Kangi Lugola aliamuru bodaboda zote ziondolewe kwenye vituo vya Polisi. Kumbukeni bodaboda zilikuwa zinarudikwa kwenye vituo vya polisi hadi kituo chenyewe kinakuwa hakionekani. Lengo la kitendo hiki ni kutengeneza mazingira ya rushwa na ufisadi ili askari wapige dili.
Kwa hali hii wanyonge watamchukia Lugola?
4. Kabla ya Lugola mabasi ilikuwa ni marufuku kuendelea na safari baada ya saa sita usiku. Hali hii ilileta usumbufu na gharama kubwa kwa abiria na kwenda kinyume na Sera ya viwanda na uchumi wa kati.
Lugola alifyeka kichaka hiki kwa kuwaambia askari wakae sawa magari yatembee usiku kucha na wananchi hawawezi kupangiwa muda wa kusafiri na majambazi.
Kwa hili wanyonge watamchukia Lugola?
5. Chini ya Waziri Lugola matukio ya utekaji, mauaji na ujambazi yalipungua sana nchini. Wote ni mashahidi wa hili muda wote mabasi yamesafiri usiku kucha hamna basi hata moja lililotekwa.
Kwa hili wanyonge watamchukia Lugola?
Nenda Lugola ila huenda kilichokuponza pia ni kuwa upande wa maslahi ya wananchi sana na kupuuza kulea rushwa za maaskari tulizozizoea tangu uhuru, lakini wahenga walisema tenda wema uende zako usingoje shukrani ila uwe na hakika Lugola siku ya kiama utavishwa taji na wanyonge.
Sent using Jamii Forums mobile app