Kampuni Hope Holdings ambayo inaendesha biashara mbalimbali katika Jiji la Dar es salaam, yatangaza nafasi 450

Donnie Charlie

JF-Expert Member
Sep 16, 2009
15,236
16,379
Kampuni Hope Holdings ambayo inaendesha biashara mbalimbali katika Jiji la Dar es salaam kama vile Mgahawa wa Papparoti, Super Market maarufu ya kuuza mazulia iitwayo Amal Carperts Mlimani City na Maduka ya FLO, Bottega Verde, Flormar, Skechers, Defacto na LC Waikiki, imetangaza nafasi 450 za kazi kwa Vijana mbalimbali wa Kitanzania.

Taarifa ya Kampuni hiyo kwa Vyombo vya Habari imesema aina za kazi zenye nafasi hizo 450 ni mbili ambazo ni Maafisa Mauzo na ya pili ni ya Watunza fedha (Cashier ) ambapo moja ya sifa za Waombaji ni kutakiwa kuwa na umri wa kuanzia miaka 30 hadi 40.

Sifa nyingine za Waombaji ni wawe na stashahada au shahada ya biashara, masoko, mauzo au cheti chochote kinachoendana na biashara na pia wawe na uwezo wa kuzungumza na Wateja na kushirikiana vizuri na Wafanyakazi wenzao.

Interview itafanyika kesho Jumatatu May 6 2024 kuanzia saa nane mchana ambapo Waombaji wote wanatakiwa kufika kwenye Interview hiyo eneo la Morocco Square, Kinondoni Dar es salaam wakiwa na copy ya CV zao na copy ya kitambulisho cha Taifa (NIDA) na kwa mawasiliano zaidi wanaweza kupiga namba 0768298857.

Chanzo
#MillardAyoUPDATES (twitter)
 
Back
Top Bottom