Dullo
JF-Expert Member
- Oct 24, 2009
- 251
- 64
Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Songea Peter Mboya akiwasalimia wananchi wa Kata ya Lizaboni wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya sokoni wa kumsaka Diwani wa Kata hiyo ambapo chama hicho kimemsimamisha Alanus Mlongo
Mwenyekiti wa Jimbo la Songea ambaye ni Diwani wa Kata ya Majengo Idd Abdalah akizungumza kwenye mkutano huo
Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Ruvuma Joseph Fuime akinada sera za chama hicho kwenye kampeni za uchaguzi zinazoendelea kata ya Lizaboni
Kutoka kulia ni Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Songea Peter Mboya, mgombea wa Udiwani wa Kata ya Lizaboni Alanus Mlongo, Mbunge wa Vitimaalum na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema Chiku Abwalo. Katibu wa Chadema Mkoa wa Ruvuma Dorphini Ghazia wakimsikiliza kwa umakini Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Ruvuma Joseph Fuime hayupo pichani wakati wa mkutano wa kampeni zinazoendelea kwenye Kata ya Lizaboni


Wananchi wakisikiliza viongozi wakati wa mkutano wa kampeni wa Chadema Kata ya Lizaboni uliofanyika kwenye viwanja vya Sokoni
Mbunge wa Vitimaalum na Mjumbe wa Kamati kuu ya Chadema Taifa Chiku Abwalo akiwahutubia wananchi wa Kata ya Lizaboni waliofika kwenye viwanja vya Sokoni kusikiliza mkutano huo.
Picha zote kwa hisani ya Stephano Mango, Songea