Onesmo Kyauke
Member
- Feb 9, 2015
- 67
- 119
Kwanza nichukue nafasi hii kumpongeza Mh Rais kwa jitihada zake za kujaribu kupunguza matumizi ya serikali yasiyo ya lazima. Ultimatum mabovu limekuwa tatizo kubwa sana Tanzania kwani hata wageni wanatucheka kwa kukosa vipaumbele. Unakuta akina mama wajawazito wanalala chini, watoto wa shule wanakaa kwenye vumbi lakini wafanyakazi wa serikali wanatanua na magari ya bei mbaya na kulipana posho zisizo na lazima.
Kuna maeneo mawili ambayo ni mirija ya kula hela ya umma. Kwanza ni serikali kutohamia Dodoma hivyo mfanyakazi ambaye kituo chake cha kazi kipo Dodoma anakaa Dar hivyo serikali inaingia gharama kubwa kuwalipa hawa wafanyakazi ambao ni wengi.
Pili, posho. Tumesema sana kwamba wafanyakazi wanalipwa mishahara hivyo haiingii akilini kwamba mtu anapewa sitting allowance wakati muda wa kikao upo ndani ya muda wa kazi ambao tayari ameshalipwa mshahara.
Nini kifanyike? Nashauri serikali ya Dr Magufuli iamue kuhamishia makao makuu Dar au kuhamia Dodoma ili kupunguza matumizi ya umma. Pili, posho zote zifutwe ili serikali ipate fursa ya kuangalia upya mishahara ya wafanyakazi wote. Ni dhahiri kwamba posho za vikao zinanufaisha wakubwa peke yao huku wadogo wakiuguza maumivu.
Naomba kuwasilisha.
Onesmo
Kuna maeneo mawili ambayo ni mirija ya kula hela ya umma. Kwanza ni serikali kutohamia Dodoma hivyo mfanyakazi ambaye kituo chake cha kazi kipo Dodoma anakaa Dar hivyo serikali inaingia gharama kubwa kuwalipa hawa wafanyakazi ambao ni wengi.
Pili, posho. Tumesema sana kwamba wafanyakazi wanalipwa mishahara hivyo haiingii akilini kwamba mtu anapewa sitting allowance wakati muda wa kikao upo ndani ya muda wa kazi ambao tayari ameshalipwa mshahara.
Nini kifanyike? Nashauri serikali ya Dr Magufuli iamue kuhamishia makao makuu Dar au kuhamia Dodoma ili kupunguza matumizi ya umma. Pili, posho zote zifutwe ili serikali ipate fursa ya kuangalia upya mishahara ya wafanyakazi wote. Ni dhahiri kwamba posho za vikao zinanufaisha wakubwa peke yao huku wadogo wakiuguza maumivu.
Naomba kuwasilisha.
Onesmo