Singida ndio home
JF-Expert Member
- Feb 23, 2012
- 3,192
- 3,353
Kwanza kabisa kuna waheshimiwa mashuhuri hawashiriki kampeni za Magufuli kama kina Salim Ahmed Salim(Waziri mkuu msaafu), Bilal (makamu wa rais) na hata Augustine Ramadhani(jaji mkuu mstaafu) na pigo baya zadi kufuatia operesheni TOROKA UJE, Kingunge amabaye ni bingwa wa mikakati ya ushindi nae kaenda kuipa tafu team itayohakikisha Edward Lowassa atakuwa Rais.
Sote tumeshuhudia katika mikutano ya Arusha, Tabora na Shinyanga watu wengi waliofurika uwanjani ni wale walioletwa na malori kitu ambacho ni kulazimisha watu wajae uwanjani, Pia wingi wa watu ni kutokana na kuwepo kwa kundi kubwa la wasanii maarufu kama kina Diamond ambao hutoa burudani bure kabisa kwenye mikutano ya hizi kampeni.
Imefikia kipindi vitu vinavyoahidiwa kwa sasa na Magufuli kama Afya, Maji na Ajira vipo nje ya ilani ya uchaguzi ya chama tawala, je vitatekelezwa nje ya ilani, Sote tunaoshuhudia kampeni zinazofanyika kila kona ya nchi hii tumeona ya kwamba Magufuli kwa sasa anafanya kampeni kama mpinzani hali inayoashiria upepo mbaya kwa chama tawala.
Kwa sasa Mheshimiwa Edward Ngoyai Lowassa ana ahadi ya kutoa elimu ya bure kutoka shule za msingi hadi vyuo vikuu na kufuta kabisa madeni ya mikopo ya wanafunzi waliosoma vyuoni wanayoilipa pindi wakianza kazi kwa upande wake Magufuli yeye ataboresha utoaji wa mikopo na wanafunzi wataendelea kuirudisha waanzapo kufanya kazi, October 25 ndio hio Tuchague kiongozi bora.
Sote tumeshuhudia katika mikutano ya Arusha, Tabora na Shinyanga watu wengi waliofurika uwanjani ni wale walioletwa na malori kitu ambacho ni kulazimisha watu wajae uwanjani, Pia wingi wa watu ni kutokana na kuwepo kwa kundi kubwa la wasanii maarufu kama kina Diamond ambao hutoa burudani bure kabisa kwenye mikutano ya hizi kampeni.
Imefikia kipindi vitu vinavyoahidiwa kwa sasa na Magufuli kama Afya, Maji na Ajira vipo nje ya ilani ya uchaguzi ya chama tawala, je vitatekelezwa nje ya ilani, Sote tunaoshuhudia kampeni zinazofanyika kila kona ya nchi hii tumeona ya kwamba Magufuli kwa sasa anafanya kampeni kama mpinzani hali inayoashiria upepo mbaya kwa chama tawala.
Kwa sasa Mheshimiwa Edward Ngoyai Lowassa ana ahadi ya kutoa elimu ya bure kutoka shule za msingi hadi vyuo vikuu na kufuta kabisa madeni ya mikopo ya wanafunzi waliosoma vyuoni wanayoilipa pindi wakianza kazi kwa upande wake Magufuli yeye ataboresha utoaji wa mikopo na wanafunzi wataendelea kuirudisha waanzapo kufanya kazi, October 25 ndio hio Tuchague kiongozi bora.