SeriaJr TW
JF-Expert Member
- Oct 21, 2012
- 246
- 224
Shemu ya hotuba ya msemaji wa Kambi ya Upinzani kuhusu masuala ya fedha na Bajeti, Mh Silinde David inasomeka hivi...
"Mheshimiwa Spika, kabla sijatoa maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani kuhusu bajeti ya Serikali ya 2016/17, napenda kuweka rekodi sawa kuhusu upotoshaji unaofanywa na Wabunge wa CCM kwamba Wabunge wa Upinzani wanaisaini mahudhurio bungeni na kuchukua posho bila kufanya kazi. Napenda mkumbuke kwamba, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni imekuwa ikisisitiza kufutwa kwa posho za vikao kwa maana ya “Sitting allowance”, lakini serikali imekuwa ikipata kigugumizi, hivyo basi Kambi Rasmi inasema kama kweli Serikali ya Rais John Pombe Magufuli inania thabiti ya kubana matumizi ya Serikali basi inoneshe uthabiti huo kwa kuifuta posho ya vikao na fedha hizo zipelekwe kwenye miradi ya maendeleo hususani kuwapatia Watanzania maji safi na salama. Hata hivyo, tunashauri, wale wanaokaa bungeni bila kuchangia hata kwa maandishi na kuchukua posho, wafuatiliwe na wakatwe mishahara yao, kwa kuwa hawajafanya kazi na hansard itumike kuwabaini.
Mheshimiwa Spika, katika jitihada kuongeza mapato, Serikali katika bajeti hii imekusudia kukata kodi ya asilimia 5 kwenye kiinua mgongo cha wabunge. Kambi Rasmi ya Upinzani haina tatizo na pendekezo hilo, ila inaitaka Serikali kwenda mbali zaidi kwa kuifanyia marekebisho sheria ya mafao ya viongozi wa kisiasa ambayo kwa sasa imewapa misamaha ya kodi ya viinua mgongo viongozi wakuu wa kisiasa kama Rais, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Mawaziri, Spika, Naibu Spika, Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya ili sasa na wao walipe kodi hiyo. Hata hivyo, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inaikumbusha Serikali kwamba kiinua mgongo cha wabunge hutolewa mwisho wa uhai wa bunge husika, hivyo haioni mantiki ya kutoa pendekezo hili sasa kwa kuwa halina impact kwa bajeti ya 2016/17..."
"Mheshimiwa Spika, kabla sijatoa maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani kuhusu bajeti ya Serikali ya 2016/17, napenda kuweka rekodi sawa kuhusu upotoshaji unaofanywa na Wabunge wa CCM kwamba Wabunge wa Upinzani wanaisaini mahudhurio bungeni na kuchukua posho bila kufanya kazi. Napenda mkumbuke kwamba, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni imekuwa ikisisitiza kufutwa kwa posho za vikao kwa maana ya “Sitting allowance”, lakini serikali imekuwa ikipata kigugumizi, hivyo basi Kambi Rasmi inasema kama kweli Serikali ya Rais John Pombe Magufuli inania thabiti ya kubana matumizi ya Serikali basi inoneshe uthabiti huo kwa kuifuta posho ya vikao na fedha hizo zipelekwe kwenye miradi ya maendeleo hususani kuwapatia Watanzania maji safi na salama. Hata hivyo, tunashauri, wale wanaokaa bungeni bila kuchangia hata kwa maandishi na kuchukua posho, wafuatiliwe na wakatwe mishahara yao, kwa kuwa hawajafanya kazi na hansard itumike kuwabaini.
Mheshimiwa Spika, katika jitihada kuongeza mapato, Serikali katika bajeti hii imekusudia kukata kodi ya asilimia 5 kwenye kiinua mgongo cha wabunge. Kambi Rasmi ya Upinzani haina tatizo na pendekezo hilo, ila inaitaka Serikali kwenda mbali zaidi kwa kuifanyia marekebisho sheria ya mafao ya viongozi wa kisiasa ambayo kwa sasa imewapa misamaha ya kodi ya viinua mgongo viongozi wakuu wa kisiasa kama Rais, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Mawaziri, Spika, Naibu Spika, Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya ili sasa na wao walipe kodi hiyo. Hata hivyo, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inaikumbusha Serikali kwamba kiinua mgongo cha wabunge hutolewa mwisho wa uhai wa bunge husika, hivyo haioni mantiki ya kutoa pendekezo hili sasa kwa kuwa halina impact kwa bajeti ya 2016/17..."