Wana JF kila siku tuanaskia madudu,ubadhilifua,Uzembe,Rushwa na Ufujaji wa Mali za Uma na kupotea uadilifu kwa Viongozi ambao unai buliwa na KAMATI za Kudumu Za Bunge,
Sasa ni Kipi kinachokataza watu hawa kuchuuliwa Hatua? Kwa Niaba ya Wagosi wenzangu Hapa Tanga sasa tumechoshwa na kuskia UOZO usiochukuliwa hatua kwa kuirekibisha au Kuwachukulia Hatua wahusika(MNATUCHEFUA).
Jamani sasa Basi tumechoka na vikao vyenu visivyo na Hatua za utendaji zaidi ya kutupasha tu Habari,kazi hiyo iacheni Magazeti..
Hata Maamuzi yenu Bungeni sasa hayana Mashiko na ndo Maana Uchaguzi uliopita watu wengi hawakujitokeza kupiga Kura...