Na posho za vikao hivyo ni balaa, pampja na kutochukua hatua yoyote, wanaendelea kufyonza funds za siye walipa kodi, ile ni kama TV series yani, wana maana gani kama siyo kujionyesha tu na hakuna dead end au conclusion zenye mshiko!Wana JF kila siku tuanaskia madudu,ubadhilifua,Uzembe,Rushwa na Ufujaji wa Mali za Uma na kupotea uadilifu kwa Viongozi ambao unai buliwa na KAMATI za Kudumu Za Bunge,
Sasa ni Kipi kinachokataza watu hawa kuchuuliwa Hatua? Kwa Niaba ya Wagosi wenzangu Hapa Tanga sasa tumechoshwa na kuskia UOZO usiochukuliwa hatua kwa kuirekibisha au Kuwachukulia Hatua wahusika(MNATUCHEFUA)
Jamani sasa Basi tumechoka na vikao vyenu visivyo na Hatua za utendaji zaidi ya kutupasha tu Habari,kazi hiyo iacheni Magazeti..
Hata Maamuzi yenu Bungeni sasa hayana Mashiko na ndo Maana Uchaguzi uliopita watu wengi hawakujitokeza kupiga Kura...
Kuna upotoshaji mkubwa sana katika hizi kamati za bunge, zinazopitia mahesabu ya taasisi, mashirika, mawizara n.k. Kwanza siyo wabunge wanaoibua hizo hoja au upotevu kama wao wanavyotaka ijulikane. Wanai ibua hizo hoja ni Wakaguzi kutoka ofisi ya Mkaguzi mkuu. Na katika vikao hivyo, kinachofanyika ni kupitia vitabu vya mahesabu na taarifa za mkaguzi mkuu kwa mwaka uliopita. Hivyo wabunge hawaibui wanataka umaarufu tu wa kisiasa. Taarifa ya CAG huwa na taarifa mbalimbali zikiainisha upungufu uliojitokeza katika matumizi au utunzaji wa kumbukumbu. Kwa mfano wataandika masufuru ambayo hayajarejeshwa mil kadhaa, manunu ambayo hayana risiti mil kadhaa, na mambo mengine mengi, ambayo kimsingi siyo wizi au upotevu, bali tu ni baadhi ya nyaraka zinakuwa hazijawekwa sawa.
Baada ya vikao hivyo, taasisi husika hupewa muda wa kujibu na kufanyia kazi hoja mbalimbali na mwisho wa siku, kama mtu hakuwa amerejesha masurufu (imprest retirement), atajaza form na hoja kufutwa. Kama hakukua na risiti risiti itachukuliwa na kuwekwa kwenye jalada, hoja inafutwa na hatimaye hoja zoooote hufutwa na hakuna mtu anayekuwa na hatia.
Ni muhimu kujua kuwa kinachotajwa mara nyingi kama ufisadi au upotevu wa pesa huwa siyo kwamba watumishi wamechukua hizo hela na kuziweka mifukoni mwao, bali huwa ni aidha kitu kimefanyika lakini taratibu sasa hazikufuatwa, au retirement haijafanyika n.k.
Kamati hupaza sauti tu kujustify uwepo wao na posho zao.
Nilifanya kazi serikalini, ni kaamua kuacha baada ya kuona ubabaishaji ni mwingi. Kuna matatizo kadhaa. Kwanza mfumo wa utendaji serikalini is tooo manual, kiasi hata utunzaji wa kumbukumbu ni shida. Kwa hiyo wakati mwingine siyo kweli kuwa huwa hizi nyaraka hazipo, bali huwa ni vigumu kupatikana pale zinapohitajika kutokana na utunzaji kumbukumbu wa kizamani.Yote hayo uliyoyaorodhesha yanatokana na kuwa na wahasibu incompetent(VIHIYO). Kwa kuwa majibu hayo hutolewa kwa lugha ya kiingereza basi ripoti kutoka kwa baadhi ya wahasibu wetu hawa ni kituko!
Nadhani waruhusiwe kujibu hoja hizi kwa kiswahili!
Kuna upotoshaji mkubwa sana katika hizi kamati za bunge, zinazopitia mahesabu ya taasisi, mashirika, mawizara n.k. Kwanza siyo wabunge wanaoibua hizo hoja au upotevu kama wao wanavyotaka ijulikane. Wanai ibua hizo hoja ni Wakaguzi kutoka ofisi ya Mkaguzi mkuu. Na katika vikao hivyo, kinachofanyika ni kupitia vitabu vya mahesabu na taarifa za mkaguzi mkuu kwa mwaka uliopita. Hivyo wabunge hawaibui wanataka umaarufu tu wa kisiasa. Taarifa ya CAG huwa na taarifa mbalimbali zikiainisha upungufu uliojitokeza katika matumizi au utunzaji wa kumbukumbu. Kwa mfano wataandika masufuru ambayo hayajarejeshwa mil kadhaa, manunu ambayo hayana risiti mil kadhaa, na mambo mengine mengi, ambayo kimsingi siyo wizi au upotevu, bali tu ni baadhi ya nyaraka zinakuwa hazijawekwa sawa.
Baada ya vikao hivyo, taasisi husika hupewa muda wa kujibu na kufanyia kazi hoja mbalimbali na mwisho wa siku, kama mtu hakuwa amerejesha masurufu (imprest retirement), atajaza form na hoja kufutwa. Kama hakukua na risiti risiti itachukuliwa na kuwekwa kwenye jalada, hoja inafutwa na hatimaye hoja zoooote hufutwa na hakuna mtu anayekuwa na hatia.
Ni muhimu kujua kuwa kinachotajwa mara nyingi kama ufisadi au upotevu wa pesa huwa siyo kwamba watumishi wamechukua hizo hela na kuziweka mifukoni mwao, bali huwa ni aidha kitu kimefanyika lakini taratibu sasa hazikufuatwa, au retirement haijafanyika n.k.
Kamati hupaza sauti tu kujustify uwepo wao na posho zao.
se​rikali na bunge ni kitu kimoja ni mchezo wa kuigiza tu